Tuesday, February 28, 2012

Minyororo ya migogoro

Tenda zingine kama wizi

WATU wanasumbuliwa, kwa sheria za udhia,
Wakubwa mliyoamua, ni maudhi yamekuwa,
Mwatakiwa angalia, au wote tutalia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Tenda mnawapatia, hadhi wasiofikia,
Na wanayojifanyia, wizi sasa inakuwa,
Mapema msipwatoa, wakazi watawatoa:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

La magari chukulia, zima linalotembea,
Pembeni ukiegeshea, waja kulifungia,
Minyororo wakatia, brekidauni kuchukua,
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Laki mbili wachukua, haijui manispaa,
Au ni yao sanaa, kwa nyuma wanapokea?
Hili watu waumia, kilio nawalilia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Mkataba naujua, hamsini ulikuwa,
Dalali anachochukua, thelathini kutimia,
Na jiji huambuliwa, ishirini ya bandia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Ni nani anayeliwa, hapa ukiangalia,
Mwenyewe unamjua, sitaki kumwongelea,
Taahira asipokuwa, hasira hatoilea?
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Tenda zilishatolewa, takataka kuzizoa,
Na hao waliopewa, leo hoi wamekua,
Fedha bado yaingia, huduma zayoyomea:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Stendi ukiingia,Mwislamu ulokuwa,
Huwezi jisaidia, aibu tupu imejaa,
Kweli tunaendelea, hali kama hii ikiwa:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

GOGORO nawamwagia, facebook mwanijua,
Tulonge kuwaondoa, huduma bora ikawa,
Mkiuchoka udhia, basi leo mtanaambia:
TENDA sasa kama wizi, watoazo manispaa,
Wanawalani wakazi, diwani na viongozi,
Kweny miji ni ushuzi, usumbufu na udhia,
Wengine wafanze kazi, wasochuma kudokoa,
Ufungaji minyororo,
Unayo kubwa kasoro,
Kwa wengi ni kubwa kero,
Inazusha migogoro,
Ila wapenda ugoro,
Ukubwa waliojaliwa!
GARI sio korokoro,
Vipo lifungwe mnyororo,
Brekidauni uharo,
Maskani za mtaro,
Na yadi ni vichochoro,
Eti lenda hifadhiwa!
Kumbe hii kubwa njaa,
Viongozi yasumbua?

Februari 28, 2012.
Dar es Salaam. Tanzania.
East Africa.

No comments: