Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kwa kilicho chetu wananchi wewe ukatuibia
Katiba na sheria ukaanza wazi kuchezea
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kwa mamlaka na madaraka ya watu kutwaa
Nawe ukajidai wananchi eti walikuachia
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kwa katiba ya historia wewe kuipindua
Ukubwa ukachukua ambao haujapewa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kwa mafisadi kuwatetea na kisha kuwalea
Moyo radhi hautakuwa na sintoyafurahia
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kwa rushwa kila kona ukawa unairidhia
Haki za wanyonge sokoni zote kununuliwa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Na wabunge tuliyowapa kofia wakaivua
Ya serikali wakawa waivaa na kisha kuitetea
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Ikawa watuchuua kila kipindi kutununua
Na bei wakawa waijua rahisi tulivyokuwa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Ikawa watuchuua kila kipindi kutununua
Na bei wakawa waijua rahisi tulivyokuwa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kama Mbeya kujakua watu bure wauawa
Pasiwe wa kusaidia wala hatua kuchukua
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Watu ukajaamua wenye mali waliokuwa
N wanyonge na fukara wao ni viatu wakawa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Siwezi miye kwa hakika nikaja kushangaa
Mbeya wakijaamua mkoa wa Zambia kuwa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Utadhani si Tanzania mkoa huu ulivyokuwa
Yote mwanzo uliojaliwa yamekwishasambaratika
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Watu ukajaamua wenye mali waliokuwa
N wanyonge na fukara wao ni viatu wakawa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kwa viongozi mbalimbali kuja kupagawa
Wakaamua ya nazaa, wakaacha ya manufaa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Wenyewe tukianza kuibiana kwa zetu hadaa
Na kutumia kuhalalisha kwa katiba na sheria
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Kulipa wasiozalisha, wazalishao kufa njaa
Kisha wananchi Tanzania watumwa wetu wakawa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Uongozi kuja oza na wauvaao ikawa wanafubaa
Wakatwaa na kuchukua, bila chochote kutwingizia
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Ubunifu na uvumbuzi ukazidi baadaye kuvia
Tusiwe na cha kuzalisha tunachojivunia
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Wanasiasa kujifanya kila kitu wanajua
Wataalamu kudharau na kutokuwatumia
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Viongozi kula kwanza kila siku wakaamua
Hata makombo wakatwaa na wengine kugawia
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Viongozi wengi wakawa sasa wananunuliwa
Na Wazungu wa Amerika nao pia wa Ulaya
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Siasa nazo utendaji kila siku kuja kuingilia
Wanasiasa wakaingilia mengine wasiyoyajua
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Tanzania, Tanzania, Tanzania, Tanzania
Usiache na mimi ije siku nikakuchukia
Nchi ikazidi kupotea na ustawi ukawa wadidimia
Nchi kugeuka ya njaa, jaa, mikosi, nuksi na balaa
Nitalia
Utalia
Tutalia
Kujutia
Ya hatia
Tanzania!
Februari 4, 2012
Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment