Haukuwa na hatuokuwa
Ijapo nafasi ulishaipewa
Kiumbe jema hukujaliwa
Ila mabaya umeumbiwa
Shetani amekuchukuwa
Kama kifaa unatumiwa
Naye si rahisi ukajaliwa
Minyororoni ukajitowa
Yawa kama umelaniwa
Kwa pako pema kukimbiwa
Ukakimbilia kwenye mabaya!
Wajifanya usilokuwa
Nuksi hapo ndio zaanzia!
Sunday, February 26, 2012
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment