Mwana waweza mficha baba
Uwe mke wa ndoa au kahaba
Kijana akibalehe, aijue janaba
Mwali kivunja ungo bila ngariba
Huuliza baba, Huulizwa baba
Namtaka baba, Twamtaka baba
Ikawa adhaba, Japo wala na kushiba
Mzigo kubeba, ukamlilia naye wako toba
kuiepa shuruba, ili waache mama kukukaba
Ukajua nasaba, imejaa yake mahaba
Huwezi ukawa baba, mama wa mengi mahaba
Maana baba ni baba, nawe ni wake swahiba
Sio suala la haiba, hili ni la watu nasaba
Huwezi pengo kuziba, hata uzidishe mahaba
Utaifanya ghiliba, watoto wakakukaba
Hukuona wewe juba, nafusi yao unaiziba
Wakutafutie kiroba, ndani iwe ni yako ghuba
Na ya kwangu kwenu tiba, kutoitupa nasaba
Mbwani kiumbe hushiba, na mengine matlaba,
Haya kwao kama shaba, dhahabu kwao nasaba
Nasaba kwao mahaba, na chachandu ndiye baba!
Februari 4, 2012
Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment