Monday, August 20, 2012

Mola tunakulilia





Aibisha viongozi, waongo waliokuwa,
Ainisha wadokozi, fedha yetu kutwibia,
Uwageuze mchuzi, ugali tukaulia,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Wakatie jinamizi, na mate kuwaokea,
Wenye siafu na nzi, wazima waliokuwa,
Kisha wape makohozi, chai yao kujinjwea,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Tai zao ziwe vitanzi, uani kujinyongea,
Na pasiwe fumanizi, mtu kuja waokoa,
Hawa si watu azizi, thamani wamejitoa,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Utupe yako hirizi, dhuluma kutoingia,
Madanzi na makumazi, usoni ukawatia,
Na vidole vife ganzi, ujanani kulemaa,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

No comments: