Monday, August 20, 2012

Haambiliki





Tukwambie kitu gani, mtu usiyesikia,
Umetushusha thamani, uduni ukatutia,
Hayatoki mdomoni, maneno yakukwambia,
Tukwambie kitu gani, na wewe ni kiziwi.

Sikulaumu mwandani, najua unatumiwa,
Kakuingia shetani, mikono aitumia,
Na akili zi mfukoni, mfuko wamuachia,
Tukwambie kitu gani, na wewe ni kiziwi.

Mikono hatuungani, njia mbali twatumia,
Nakupisha mjivuni, uvune unachopewa,
Yangu yabaki moyoni, kuliko ya kukwambia,
Tukwambie kitu gani, na wewe ni kiziwi.

No comments: