Monday, August 20, 2012

Idadi kuitambua





Kila mwenye nia mbaya, dini ameikamia,
Idadi kutokuijua, siri kutoifichua,
Katoliki wawanunua, kwao sasa ni bidhaa,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Ukweli wanaujua, wataka kuufikia,
Musuli kuzitumia, waumini wakavia,
Tunawahakikishia, kazi yao kufulia,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Mataifa yaamua, idadi budi kujua,
Na sisi kujielewa, yetu tukajipangia,
Na chetu kilichokuwa, tuweze kupigania,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Wakuu wa kuteuliwa, wakoloni wa mikoa,
Kazi wachangamkia, bwana wao kumfaa,
Islamu wawasumbua, haki yao kutetea,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Dhuluma najionea,Waumini wafanziwa,
Ya kwao wakaonea,na hatiani kutiwa,
Nchi twaisukumia,kule kusikotakiwa,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Mola tunawaombea, wazidi kujipepea,
Bendera ikasambaa, na upepo kutwaliwa,
Mbele iende chakaa, kufanza isichojua,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa?

Manani twakuachia, dini kuiangalia,
Siridhie kuzuiwa, imani kuendelea,
Nafasi kuichukua, ilokuwa yaibiwa,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa?

Daraja kujipandia, la juu tukajitia,
Islamu twanuia, ya kwetu kupigania,
Wakati ukifikia, hakuna wa kuzuia,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa?

No comments: