Saturday, May 5, 2012

Kiswahili ni mzizi


Nimeyaona Asia, Ulaya ni mazoea,
Lugha wanajivunia, hata kidogo wakiwa,
Nyengine kutotumia, ila nje wanapokuwa,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Chao wanajivunia, bila ya kusimamiwa,
Na kisha waongezea, vya wengine kuvijua,
Ubingwa kujipatia, kwayo na yale ya dunia,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Asili waangalia, urithi kutopotea,
Pia rahisi ikawa, watoto kujifunzia,
Lughani wakichipua, mengi sana huyajua,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Leo hapa Tanzania, maneno yanapotea,
Ndege wetu kuwajua, wazima utawaumbua,
Sembese watoto kuwa, hawana wanalojua,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Wanyama nao pia, wawili watatu wajua,
Samaki waliojaa, bahari nayo maziwa,
Wangapi watakwambia, majina waliyopewa?
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Miti na mingi mimea, hakuna anayejua,
Utacheka nakwambia, mjini ukiulizia,
Afadhali inakuwa, kijijini wanajua,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Maumbo yake dunia, wengi utata hukuwa,
Bure utajisumbua, hakuna anayejua,
Na hawa wategemea, kitu kuja kuvumbua?
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Mizizi yake mmea, asili hutegemea,
Ndipo inapokuwa, kwa yote yanayokuwa,
Elimu ikiwa pia, muhimu kuzingatiwa,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Watafeli nadharia, kwa lugha kutoijua,
Watoto kuwakandia, ya uongo yalokuwa,
Walimu kuwazulia, hata wasiyofikiria,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kiswahili kutumia, kufundisha nadharia,
Kwa undani kuelewa, yote yanayozungumziwa,
Haya wakishayajua, Kama China tutakuwa,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Tuitenge nadharia, na lugha kufundishia,
Maabara kufungua, shuleni na vyuo pia,
Lugha kuzikazania, mbili tatu wakajua,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Ndege wengi tutaua,kwa jiwe moja kutumia,
Sayansi wakaijua, na lugha kuzing'amua,
Hata Kiarabu pia, na Kichina kutumia,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Mashariki inafaa, tuanze kuangalia,
Isiwe tunachelewa,
Wenzeetu wakatangulia,
Lugha yetu kujitia, lakini kutokutufaa,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Viongozi watakiwa, uzito kuuchukua,
Wafanze kuyaamua, mapema inavyokuwa,
Nami sintoshangaa, wengine kutangulia,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kiingereza balaa, ujanja wanatumia,
Lugha yetu kuiua, na yao kuendlea,
 Na sisi kamamajuha, mtegoni twaingia,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Nyerere alianzia, lugha kasaliti pia,
Mwinyi alipofatia, naye akazainiwa,
Mkapa hakujitambua, wala hatajitambua,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kikwete asipojua, humo humo kufatia,
Kiswahili kukiua, na elimu nayo pia,
Ndicho kilichobakia, na ndiyo yanayotokea,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Ila mtunzi najua, rais wa Tanzania,
Kweli atakayekuwa, Kiswahili ataamua,
Kila ngazi kutumia, na nchi ikaendelea,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kwenye kapu watupiwa, wote waliotangulia,
Takataka watakuwa, kati yetu historia,
Nafasi waliipewa, ila hawakuitumia,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Yajifia Tanzania,
Na pengine kung'olewa
Utamaduni huvia
Taifa lije lemaa
Asili ikapotea
Uvumbuzi nao pia
Watu wabakie kuwa
Vya wengine watumia
Pasiwe kitu kimoya
Wao wanachogundua!


Kuthubutu hapakua, na kujaribu wapwaya,
Hakuna walilojaliwa, kuliweza na kujua,
Waigaji wabakia, ni wasanii bandia,
Kiswahili ni mzizi, ukikatwa mti hufa:
Twaizika Tanzania,
Hali hai yapumua
Kwa kutokujitambua
Na kesho yetu kujua
Wakubwa wanunuliwa,
Cha watu kung'ang'ania
Wengine wajihadaa
Dawa ngeni wakidhania
Kumbe muda wapotea,
Milele nyuma kubakia,
Hamsini yaishia,
Itapita pia mia,
Hapahapa twabakia !


TTRKPP LIMITED 2012

No comments: