Saturday, May 5, 2012

Huwezi danganya kifo



Uzee ukiingia, kitu gani wangojea,
Vipi iwe ni hadaa, Jibrili kakujia,
Muda akakuachia, kuibadili tabia,
Watu utawahadaa, huwezi danganya kifo !

Muda akakuachia, kuibadili tabia,
Nawe unajihadaa, nguvu mpya kujitia,
Huna unalolijua, kiumbe unapotea,
Watu utawahadaa, huwezi danganya kifo !

Nchi utaiachia, wengine kuendelea,
Yako yakajaishia, kumbukumbu kubakia,
Ubaya ukizidia, zaidi kukumbukiwa,
Watu utawahadaa, huwezi danganya kifo !

Afrika inalia, uongozi kutokua,
Arijojo waelea, hawajui pakutua,
Mibabe tumeachia, damu tuanjimwagia,
Watu utawahadaa, huwezi danganya kifo !

Nusura hatutajua, bila Mola kumlilia,
Kisha kumshtakia, viongozi kutokuwa,
Yeye akatuandalia, bora watakaotufaa,
Watu utawahadaa, huwezi danganya kifo !

No comments: