Wednesday, October 31, 2012

Simama uhesabiwe

Mkono sasa tumia, juu ukaunyanyua,
Wito ukaitikia,  taifa kutumikia,
Uongofu lalia, ni nani wa kulifaa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Wakati ni huu hawa, wapaswa kuhesabiwa,
Kwa upande kuchagua, kusimama kutetea,
Heri ukiichagua, shari hutolichukua,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Bahari yachafuliwa, na wengi maharamia,
Meli wameidandia, wahofu mabaharia,
Ya heri tukiamua, nahodha tutamfaa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Nahodha tukimfaa, akili zitatulia,
Meli kujiongozea, hadi nanga tukatia,
Na wengine kuachia, wasoitaka balaa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Na salama Tanzania, ikazidi kubakia,
Ghasia kuziondoa, za wasya hasiria,
Mabomu kutochimbua, viazi tukidhania,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Rushwa imeshatapakaa, kama panya tumekua,
Paka tunamuhofia, mafichoni twaingia,
Kila anayeisikia sikio ajifumbia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Nani mwenye ushujaa, mhanga kujitolea,
Kama babu wa India, uzee kajipambua,
Kitalini kaingia, bure wakamzuia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Kila mtu ashangaa, wakubwa kando kulia,
Ngoma kati imekaa, pembeni waugulia,
Nani aliyetakiwa, ujemadari kuuvaa ?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Uongo ukitumiwa, mwisho ukweli ukawa,
Nani atatuelewa, timamu waliokuwa,
Guu limetangulia, kule tusikotakiwa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Musuli waliopewa, kwa kuwatunza hidaya,
Leo wafanya mabaya, hila wanaitumia,
Nyara watu wote kuwa, wapendavyo ndivyo huwa?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Haitojenga hadaa, nchi safi ilokuwa,
Viinimacho vikiwa, maruerue hujaa,
Turudi nyuma raia, na msokuwa raia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Kioo tumekikimbia, twezacho jiangalia,
Taasisi zazaliwa, bure hela kutumiwa,
Na kazi zilizopewa, rukusa zakataliwa ?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Sasa kihoro watia, wakubwa waugulia,
Kucheka najizuia, kila nikiwasikia,
Au yaweza ikawa, tuna 'bosi' tusomjua ?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Mwenzi ngao augua, kilemba kukikazia,
Kinamama ni bidhaa, leo wananunuliwa ?
Nini kilichobakia, nchi bado kupotea?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Wazee kwa yao njaa, waukubali udhia,
Nani wa kuwaangalia, wasiende nunuliwa,
Hali ilivyo ni mbaya, kapuni wataingia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Vijana tunawagawa, kwa fefha kuwarushia.
Huku tunachekelea, wanavyozipigania,
Masalale naitoa, Mola kutuhurumia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Wazazi gumba wakiwa, huko huko  twelekea,
Ndoano kuiachia, kazi kubwa itakuwa,
Yao yote wamefulia, nin kilichobakia ?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Watu wanaulizia, hivi hii ndiyo njia,
Nyerere katuachia, sisi kuifatilia,
Au tumeshapotea, twanda tusikokujua ?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Mishipa imetujaa, twazidi kung'ang'ania,
Twajua tumekosea, tayari twakoselewa,
Kukubali twaktaa, sawa tunajionea,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Sasa waliojaliwa, katikati waingia,
Samaki wanawavua, nchi kavu walokuwa,
Mipango tumefulia, baharini kwenda vua,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Mipesa waitumia, vijana kuwanunua,
Kisha pande tukagawa, hawa na wasiokuwa,
Kule macho twafumbia, huku twawakolea ?
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Dabo standadi mbaya, mbali hatutafikia,
Basi tulilodandia, tairi zajichimbua,
Bondeni twaelekea, na kingo kusikokuwa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Mamlaka zatakiwa, haki kuisimamia,
Vingine inapokuwa, kadhia naihofia,
Utu waja kujifia, Tanzania italia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Kiooni kujangalia, muda umeshawadia,
Tena bila kuchelewa, tusije kuadhiriwa,
Tutofautishe ubaya, na mazuri kuchagua,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Huu ni wangu usia, moyoni ninautoa,
Nchi hii kwangu ua, waridi lilotulia,
Kwa amani na umoya, bara linajipambia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Watu wangu wema huwa, ila wanapoonewa,
Kisha wakabaguliwa, kufanzwa kisichokuwa,
Moyoni wakiumia, mateke wataachia,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Walojuu watakiwa, haki kuisimamia,
Kuna vyombo vyaingia, haki sasa zinaua,
Macho mkiyafungua, ukweli mtautambua,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Naasa kutoamua, pasina kweli kujua,
Daudi alitubia, kosa alipotambua,
Vingine ikijakuwa, ujibari ni nazaa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Mola nakugeukia, Maulana ulokuwa,
Mtukufu na mjua, njia unazawadia,
Sahihi iliyokuwa, watuwe kutopotea,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!

Nasi twakuangukia, mustakimu kuijua,
Taifa kusaidia, salama likabakia,
Vizazi vikafatia, bila ya kuhujumiwa,
Simama uhesabiwe, nchi ilipokutaka!







Hawachambui nafusi

Za mola zake hidaya, katikati huishia,
Hauwezi kujaliwa, yote ukajipatiya,
Ni dhaifu tulokuwa, kidogo tunapatiwa,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Mpenzi malikupewa, nafusi  yakuambia,
Yataka kujisomea, msingi ukaujua,
Una uzuri ubaya, taa ukimulikia,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Ipo tena njema nia, ubaya ukikusudiwa,
Hata ukiumbuliwa, ktio waweza chimbua,
Kidgo unapopewa, kubali kuvumilia,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Kubali kuvumilia, huku unajinasua,
Kwa chache tu hatua, tajiri waweza kuwa,
Wengi wanapofulia, si budi nawe ukawa,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Huchuma aso na nia, na mwenye nia kufa njaa,
Dunia yake hidaya, mpendwa humgawia,
Lugha anayeiua, asili amalizia,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Thamani asiyejua, la nje hung'ang'ania,
Lake akaliachia, lifaalo kumjengea,
Kiumbe alolaaniwa, mwasisi hawezi kuwa,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Watu wasiojitambua, hapa wanajipitia,
Wakishashusha shahawa, na matumbo kuwajaa,
Zaidi kufikiria, kwao ni pata potea,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

UKiona historia, ni usipopatazamia,
Maombo yanapoanzia, nako yakatunukiwa,
Kukua na kuendelea, na koe yakaenea,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Tajiri alowazaa, fakiri huja jifia,
Na yatima hulelewa, tajiri akaja kuwa,
Na anayeonelewa, mkombozi huja kuwa,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Alotakiwa uawa, huja kukombolewa,
Usultani kutwaa, na milki kujiundia,
Kubwa na inayozagaa, dunia ikamtambua,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Kiswahili nacho pia, hatua itafikia,
Watatokea shujaa, kuja kukipigania,
Cha kwao wakatumia, bila ya kutegemea,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Hila wakazitambua, mkoloni kuzitia,
Lugha yake kutumia, hata isipowafaa,
Mfukoni huwatia, wakubwa akawalea,
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.

Watoto huwatukua, shuleni akawatia,
Mapema inavyokuwa, huko kwake malkia,
Nini utamuambia, yule alofadhiliwa ?
Hawachambui nafusi, somo lao kujifunza.





Yao wanapoyapanga



NAWAONEA huruma, akili wanaojitia,
Wakaifanza dhuluma, mbele kutofikiria,
Kielimu wanakwama, njia hawajaijua,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Hii ni kubwa kalima, milango inayofungua,
Mambo mengine adhama, stahi yahitajiwa,
Yasijeenda mrama, ikawa ni kulaumiwa,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Mambo yataka rindima, na mtoa wamjua,
Mpangaji mwenye hima, hakuna asichojua,
Huna siri kumnyima, aache kuitambua,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Majinaye ni Alima, ilmu aiandaa,
Nasi wote maamuma, lake tunalingojea,
Hata ukiona ngama, angani wanaoingia,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Akili kawaazima, za kwao wakajitia,
Hiyo ni yake rehema, vya kwake kuvitumia,
Hana anayemnyima, kutafuta akiamua,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Walio kwetu zahama, wasotaka tangulia,
Waturudishao nyuma, wengine kutegemea,
Hadimu hawajahama, wazaliwa Tanzania,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

NI watu wa kukoroma, na uongo kutetea,
Ila lililo na uzima, huwa wanalibagua,
Uungu wesha uazima, kitu gani kuwambia ?
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Huwa wazaa tuhuma, kuishi kama vichaa,
Vizuri ukiyasema, ubaya watautia,
Ukiwafunza kuchuma, wao watajiibia,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Watu wa kurudi nyuma, wengine huwasifia,
Ajabu yao tazama, yao watapuuzia,
Mchezo wao zahama, na adui kuhofia,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Watu wa kurudi nyuma, hawawezi tangulia,
Enzi zao za lawama, na mchawi kumgundua,
Kwao hufua hekima, wakaanika udhia,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Watu wa kurudi nyuma, lugha yao hufulia,
King'eng'e wakakisema, hata kisipotakiwa,
Maovu yanayofumwa, ulemavu huwatia,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Hukimbilia kukama, nyonyo hawajui njia,
Na teke likituama, samadi huangukia,
Akili ni kuazima, kama usipojaliwa,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Kama simba 'ngenguruma, vigumu kunisikia,
Watu wa kurudi nyuma, kushindwa wanakataa,
Wahakam wao mgema, nazi asiyeangua,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Hawaamini kiyama, hadi kinapotokea,
Watu wa kurudi nyuma, siku yao husinzia,
Jibrili hatokwama, nyepesi zake hatua,
Yao wanapoyapanga, Mola naye anapanga.

Huwa mithili kombora



MEPESI kuyasikia, yasiingie moyoni,
Ila yakishatukia, huupata usononi,
Kugalagala ikawa, dunia huitamani,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Ukweli utafukia, ukawa nayo yakini,
Hawawezi kugundua, yako wasiyoamini,
Njia ukakazania, na kujipamba thamani,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Ila siku hufikia, likaingia machoni,
Na urembo likatiwa, ujikute ulimboni,
Vipi utalikimbia, giza uliloaamini,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Magumu kuyaelewa, yabkiyo kweny mboni,
Kifikra nachelewa, hojaze kuziamini,
Nisije singiziwa, miye sikuwa makini,
Matoni wakiliona, huwa mithili kombora !

Uombeayo wengine



WENZAKO waliokuwa, wawaombea ubaya,
Siachi kukushangaa, na uzima kuhofia,
Manani kalikataa, niyo ni husda mbaya,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Uganga sijaupewa, ya keshosijayajua,
Mtabiri haijawa, dhalili mimi nikawa,
Ila nikiangalia, yapo ya kuashiria,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Kwa kuotesha ubaya, mbegu huwa zachipua,
Na mimea ikikua, huwezi tunga kuzaa,
Si zuri linalokuwa, linanitia kinaya,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Gizani tulipokuwa, hili halikuzagaa,
Ila toka kuingia, tivii sasalasambaa,
Watu wakiangaziwa, kuropoka ni tabia,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Nuruni wajishushua, kutamka lisofaa,
Akili wakidhania, hapo wameitumia,
Na pointi imeingia, goli wamejifungia,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Kumbe wazua nazaa, tendo likawachukia,
Ulimi kujililia, adhabu kuihofia,
Na moyo ukasinyaa, kwa huruma kuingiwa,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Kiumbe ukijaliwa, nakuasa nyenyekea,
Udogo ukajitia, na dhaifu  kuridhia,
Huna unalolijua, Mola pekee ajua,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Ya kesho yana tabia, vingine yakatokea,
Vile ulivyodhania, kinyume chake yakawa,
Hiyo aibu na haya, hapo utaikimbia ?
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Mabaya kuwaombea, wenzio wanaojaliwa,
Hayawezi saidia, yako mazuri yakwa,
Zaidi hushindiliwa, chini ukadidimia,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Ila kama hiyo dua, kulaani yakubaliwa,
Ubaya ukitendewa, lazima mja kulia,
Pengine watakusikia, shimoni wakakutoa,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Yusufu yalimtokea, nduguze kumfanzia,
Baya hakuwaombea, ila kaiomba dua,
Mwenyezi kumuokoa, kwa yoyote ile njia,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Utumwani kanunuliwa, huko kazidi kung'aa,
Na ukuu akapewa, wizara kusimamia,
Kaenzi walozaliwa, hata kuja wasaidia,
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Na wewe ungelikuwa, nini walifikiria,
Si shimoni 'ngewatia, ukaondoa udhia,
Mzaliwa ukamfaa, kwa baba mkarejea?
Uombeyao wengine, yasije kupata wewe !

Enzi hizi za vitendo



MANENO hayamezeki,  za vitendo enzi hizi,
Mizigo haibebeki, wahitajika watenzi,
Jamii ni ushiriki, kwenye kula nazo kazi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Imetaliki ashiki, watu wangoja mandazi,
Wamechoka unafiki, wa vitumbua vya nazi,
Waisubiri mikiki, na wao  wawe wakwezi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Hali hawaiafiki, mkao chini ya ngazi,
Ya juu hayaharibiki, wamejaa watengezi,
Huko hawaamainiki,  walo juu yake ngazi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Ya sasa hawabariki, yamejaa makunyanzi,
Lisemwalo si tawfiki, ni wali hauna nazi,
Si udugu si urafiki, hili haliwatandazi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Zinadhoofu milki, na kuzizima mapenzi,
Mioyo haishtuki, chazuka kigugumizi,
Wa hariri ni kaniki, na kingine hakiwezi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Wanazuka mamluki, kuuza kiso saizi,
Riziki kutamalaki, asiyotoa mwenyezi,
Uroho wayabariki, hata kwao viongozi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Wake hawaaminiki, wawadaka wachuuzi,
Fedha wanaomiliki, wakifanza manunuzi,
Wanoni ni washiriki, na wanyonge wana genzi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !

Hali yakwaa kisiki, manusura ni mwenyezi,
Nchi hairehemeki, yafulia matumizi,
Malengo hayabebeki, hawawezi viongozi,
Enzi hizi za vitendo, hayamezeki maneno !


Hii ni hotuba nzuri



NaONA wamehariri, kama wimbo imekuwa,
Mashallah tahariri, kila kitu inajua,
Ningelisema kafiri, ila neno nahofia,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Msomaji kakariri, hata walipokosea,
Inang'ara kwa dhahiri, ila feli haijatwaa,
Na nimeipata habari, watu walikisnzia,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Hotuba kama hariri, laini ilivyokuwa,
Ingelikuwa kadari, lake lingeshatimia,
Kuna vichaka na pori, msituni huishia,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Hii hotuba mahiri, ugonjwa unaujua,
Bali wesha daktari, ugenini wahamia,
Na walimu wadhukuri, kimbioni kukimbia,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Hotuba hii hodari, ila kilio yalia,
Wamezidisha hasiri, mkombozi kajikwaa,
Aogopa istifari, kwa israfu kutia,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Hotuba hii kadiri, njia inaitambua,
Isipokuwa yakiri, watuwe hawana nia,
Kuna  kitu wasubiri, na mimi sijakijua,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Hotuba hii shairi, siachi kujisomea,
Mteperevu fakiri, hekima najionea,
Na shair yazidi heri, ndilo nililiogundua,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Dariziye za fahari, na pindo zanakshiwa,
Ila kilicho sifuri, akili zinatibua,
Haujawa umahiri, ila riziki hutoa,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Tamathali zadhihiri, usawa zisizokuwa,
Dunia sasa hiari, mtu kitaka kujua,
Wapo walio fakiri, leo tajiri twajua,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Siasa si mahubiri, hotuba sasa za njaa,
Watu wanazighairi, shibe wataka sikia,
Pasipnayo ghururi, mishono watafumua,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Pepo zataka mahiri, pepezi zikifuatia,
Wakaijua hadhari, kule zinakoendea,
Na  maji haya ni zari, mtu huzama kakaa,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Hii ni mpya bahari, na weledi waijua,
Kuogelea hatari, akili usipotumia,
Mabavu ukivinjari, mwenyewe huja kulia,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Mivumo inabashiri, pepo wasiotulia,
Kuntu wameshadhihiri, si watu wa kung'olewa,
Hawahofu majibari, wanavifua vifua,
Hii ni hotuba nzuri, kama nyimbo yaimbika !

Kwanini upate dhambi



MJA mkosa subira, maisha wayachezea,
Yakusumbua harara, shetani kukuingia,
Haraka ukiparura, shida utavumilia,
Kwanini upate dhambi, tamaa ya siku moja ?

Mwendo huo wa hasara, weye uliochukua,
Unakosa maghufira, kila siku kurudia,
Tabaguni hadhira, laiti ungeyajua,
Kwanini upate dhambi, tamaa ya siku moja ?

Yakupoteza  papara, kutotaka kuishiwa,
Waona ni masihara, hauwezi kutulia,
Kufuru unaipara, ya kuja kukuumbua,
Kwanini upate dhambi, tamaa ya siku moja ?

Maisha budi dhamra, na dhiki kuvumilia,
Haramu ikakera, kwa kesho kuihofia,
Ukkifanya ajira, halali inakimbia,
Kwanini upate dhambi, tamaa ya siku moja ?

Halali huja kuzira, mbali nawe kukaa,
Na hiyo ndiyo bishara, pepo imeshapotea,
Duniani ni hasra, na akhera wafulia,
Kwanini upate dhambi, tamaa ya siku moja ?


Katikati usikae



 Yaamka Tanzania, bora yataka chagua,
Na mapema kuamua, na wewe utajaliwa,
Mwanga ukautambua, na giza kuligundua,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, wewe mtu wa rushwa, au rushwa wakataa ?

Kuna wanaokubalia, rushwa sasa wanalea,
Ukitaka kumbatia, hilo umeruhusiwa,
Ila baya linaua, na ni gumu kulilea,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, wewe mtu wa rushwa, au rushwa wakataa ?

Tume huru yatakiwa, kabla chaguzi kwingia,
Hakuna la kungojea, ila kufanza hadaa,
Ni rahisi kuamua, rais akiamua,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, tuanze badilika, au tungoje katiba ?

Kuna vyombo vya sheria, batili waichagua,
Liso haki laridhiwa, la haki kukataliwa,
Mwananchi ni kuamua, ni lipi unaridhia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, waitaka batili, au wataka halali ?

Watu wanawanunua, kwa kushoto na kulia,
Watakiwa kuamua, kama hili waridhia,
Na kama walikataa, sauti yako kutoa,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, waitaka batili, au wataka halali ?

Wazuka Watanzania, wenye uchu tamaa,
Uroho pia na njaa, kesho kwenda chaguliwa,
Na wanaloligembea, hakuna anayelijua,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Watu sawa kununua, au dhambi kununua ?

Kuna wanaotuambia, magari ni kuendelea,
Nyumbani twafa kwa njaa, kitu gani kutufaa,
Kama washangilia, kibwebwe kujifungia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, magari ustawi, au manufaa nyumba ?

Eti wanatuambia, vitu ni kuendelea,
Ulaji wauchochea, hata hela 'sipokuwa,
Madeni kuja tutia, kama Giriki tukawa,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, magari ustawi, au manufaa nyumba ?

Mafuta tukipatiwa, na madini yalokuwa,
Sera inayotufaa, ni elimu kugharamia,
Tutaujenga usawa, mbio pakuzianzia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, elimu yetu bure, au lazima kulipa?

Tiba inatuchengua, bure bora kuitoa,
Inaongeza usawa,  unyonyaji kupungua,
Debe ninaipigia, jamii kusaidia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, tiba yetu bure, au shuruti kulipa?

Michezo tunafulia, wote tunajionea,
Nani wa kugharamia, vijana wapate kua,
Ovyo tukiliacia, arijojo litapaa,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, tufadhili michezo, au tufadhili fisadi ?

Fedha shetani balaa, huru ukimuachia,
Minyororo kututia, tusokuwa na tulokuwa,
Yatakiwa kuamua, vipi tunachukulia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, fedha itutawale, au tutawale fedha?

Ubeluskoni nazaa, vituko tutashangaa,
Langu ninaloamua, watu pesa kukataa,
Hao ni maharamia, wanasiasa hawajawa,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, fedha itutawale, au tutawale fedha?

Wapo waliotulia, katikati wamekaa,
Tunawajua tabia, sio watu wa kutanua,
Na cheo wakipewa, kichwani hakitaingia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, fedha itutawale, au tutawale fedha?

Uongo tumechagua, mengine kujifanzia,
Imetuzidi hadaa, sasa inatuumbua,
Lazima kufikiria, bora tukaliamua,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, uongo wakubali, au wataka ukweli ?

Na bora kuliamua, ni uongo kukataa,
Mola hatoliridhia, ukweli tukiachia,
Taifa litadumaa, nidhamu tusipotia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, uongo wakubali, au wataka ukweli ?

Maisha tukiamua, busara inatakiwa,
Upande kuegemea, usiokuwa na mbawa,
Sera hizi nazijua, babu alikizitumia,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, wala na matajiri, au wala na fukara ?

Vijiji vinatakiwa, nchi yetu kukomboa,
Nyumba tukiwajengea, utalii utakuwa,
Akili tukitumia, mengi twaweza kuzua,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, waozssha vijiji, au walea vijiji ?

Ubia unatakiwa, kilimo kuendelea,
Vijji vikaingia, na tajiri walokuwa,
Wao jasho wakatoa, na mgeni ni vifaa,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, waozssha vijiji, au walea vijiji ?

Uvuvi hivyo ukawa, wanavijiji kupaa,
Pwani wanaokaa, kunakotisha kwa njaa,
Haya tukiyaamua, nchi itaendelea,
Upande upi chagua, wewe mkono waunga;
Katikati ukikaa, historia ya kuzika:
Je, waozssha vijiji, au walea vijiji ?

Isiwe adui wewe




Katika hii miaka, huwa usiyemdhania,
Nafusi kughalifika, mwingine kumdhania,
Na wajanja wazaliwa, hili wanalitumia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Chako atakuibia, yule akasingiziwa,
Yule ukimvamia, yeye anajichimbia,
Pupa ukiitumia, pabaya wenda ingia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Vyama vitakuambia, udini huyo kajaa,
Ukiivuta pazia, kumbe ndio walokuwa,
Yanapokuja tokea, mwengine asingiziwa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Wamezuka wa kuzua, waitwa mapakazia,
Uchuro wanautia, kuiharibu dunia,
Uoza kuusifia, na maradhi kuutia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Watu wananunuliwa, wengine kuwasingizia,
Imani wasiokuwa, mbwa mwitu wa dunia,
Kazi yao kutumiwa, makombo wakaachiwa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Njaa yao inachipua, hadi kuwa ukichaa,
Kitu kutofikiria, mitegoni huingia,
Jema wakliachia, uovu kuununua,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Watu wa kusingizia, na uongo kuufua,
Pasi kisha kuutia, mvaa akajivalia,
Zama zinawaachia, giza likajitandia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Wakubwa watatumia, waliokonda kwa njaa,
Dhima wakaichukua, wamiliki nao kuwa,
Na hicho wanachopewa, ni hadithi nakwambia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Kinamama huugua, uzuri kukimbilia,
Nje wakiangalia, dhahabu wakadhania,
Ndani wangeliujua, hilo wasingekaribia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Huchekwa lile la kulia, la kucheka wakalia,
Ilivyoota hadaa, na zaini kuchanua,
Ukiyaona maua, sumu yaweza ikawa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Neema watakwambia, sumu unalohofia,
Na wasomi wenye gia, digrii kuning'inia,
Ukweli watakuapia, bila ya kufikiria,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Kila aliye na njaa, rahisi hununuliwa,
Usomi kweli kajaa, lakini tumbo lalia,
Huikubali nazaa, hata uhai kutoa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Wakubwa huchaguliwa, kama ni mbovu kofia,
Matundu tele yajaa, kitu haiwezi zuia,
Wanaloliangalia, ni posho kuipokea,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Wajumbe wanunuliwa, kama gunia la mkaa,
Ni moto wa kupikia, chakula chake hadaa,
Kisha wanapo9vimbiwa, kutapika si kinyaa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Kamba inaning'inia, hakuna wa kuifwatia,
Katikati yaishia, yawezayo sadia,
Na mkoa na wilaya, ni mizigo imekuwa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Ni gesti za kulalia, maofisi yamekuwa,
Nani wa kufuatilia, yale yanayoamuliwa,
Kama vile wangojea, mamajusi kuingia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Nje wanaotakiwa, ofisini wamekaa,
Ustawi wangojea, wenyewe utatokea,
Maajabu yalokuwa, 'Gordon' kutokea,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Wengi kazi ni kunawa, wangoja kupakuliwa,
Kula kwao majaliwa, na ugumba ni tabia,
Kipato chadidimia, wakwambia kinakua,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Mengi watasingizia, na yote nayakataa,
Si kweli ninatambua, mengine wasingizia,
Hakika hawajajua, nasibu wajitajia,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Mimi ninalolijua, ni njaa inayokuwa,
Pande zote kuenea, wa chini wakaumia,
Na juu washikilia, kula kama vile jaa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Hali ikiendelea, Tsunami yakaribia,
Na wala sintoshangaa, makubwa kuyasikia,
Jumlisha na balaa, haitakuwa nazaa,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Isiwe adui wewe, unisingiziye miye,
Mnyonge unionee, wanene wakutumie,
Kuna ngwaa kuna ngwee, majibu yake ujuwe,
Isiwe adui wewe, wadanganya  yule kule ?

Silaha za sikuhizi



Zamia ukaijua, juu huachi kupaa,
Inakokwenda dunia, tekhohama silaha,
Mwana unapomlea, mpe nakupa nasaha,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Mengineyo ni udhia, maoboti watakiwa,
Njiani wakaingia, machozi wasiolia,
Pilipili wasojua, na kudhuru haijawa,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Sasa watu wanakaa, majumbani kutulia,
Vitufe wakatumia, ndege juu zikapaa,
Na kama walivyo njiwa, ujumbe wakachukua,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Wenda mbali kwa kupaa, silaha ndani zajaa,
Na huko ulikokaa, unaweza kufyatua,
Shabaha ukitumia, hakuna wa kubakia,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Mamake teknolojia, silaha zinazofaa,
Akili zinatumia, sio nguvu kutumia,
Na kila anayejua, hatua anachukua,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Elimu inatakiwa, si ujinga kuulea,
Nyuma anayebakia, atakuja kufulia,
Angani zinaingia, akili zajibangua,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Humhehimu dunia, mbinu anayezijua,
Ujinga anayelea, utumwa huendelea,
Kuamka yatakiwa, muda  kuusakazia,

Juhudi inatakiwa, wenetu kukumbatia,
Wapate teknolojia, na vyema kuitumia,
Pamwe na kuwa silaha, lugha itatujengea,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Tumuombeni Jalia, macho yetu kufungua,
Hili juu walijua, sikunyingi watumia,
Nanyi mliochaguliwa, mwatakiwa kuelewa,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!

Kitabu mkiingia, miraji mtaijua,
Ahlil kitabi radhia, nani asiyelijua,
Ila wanaojizuzua, na kujifanza wajua,
Silaha za sikuhizi, mamake teknolojia!



Chagueni cha sitini


HAMSINI na sitini, hasra kitawatia,
Wana mengi mahumuni, haramu yaliyouwa,
Ya kwao msiamini, siku moja mtalia,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Mimi ninakikataa, kundini ijapokuwa,
Najua nimeshafulia, siwezi watumikia,
Neema sintawaletea, ni ajizi na udhia,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Wa sitini wanafaa, hamsini  wafikia,
Na akili zatulia, uzee haujakaa,
Akili watatumia, wakiridhi teknolojia,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Hamsini chafikia, ngazi bora kitakuwa,
Hakina kusingizia, uhuru kutuletea,
Au waliochipua, ukada kutumikia,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Hhamsini wanafaa, hamsini twafikia,
Mstari kuutia, kizazi  kipya kikawa,
Ya nchi kuwaachia, sio kuyang'ang'ania,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Rais mtarajiwa, teknohama atajua,
Pepe anaitumia, kutuma na kupokea,
Karani hatoachia, kaziye kumfanzia,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Facebook kaingia, na jamvini hutulia,
Hoja zake anatoa, na wenzi kujisomea,
Dunia anaijua, na dunia yamjua,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Twitter aitumia, ofisini akikaa,
Na nyumbani kanunua, iPhone anaijua,
Na mitandao ajua, ndio itatukomboa,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Operesheni ajua, kiendeshi hutumiwa,
Asili anaijua, na bei aitambua,
Vifaa wakinunua, hawawezi tuibia,
Chagueni cha sitini, kabla kitasinzia !

Umuhimu aujua, viwanda kujiwekea,
Mitambo kufyatua, bila nje kununua,
Zana bora maridhawa, vyema kujitengenezea,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Kunyonya atakataa, kwa Obama na Mamaa,
Kiswahili kuinua, kote tukakitumia,
Na nchi kijijengea, siri ikajiwekea,
Chagueni cha sitini, kablaatasinzia !

Tatizo si uongozi



Utakwepo uongozi, huu ukiisha kazi,
Kwa hiyo ya uongozi, Katu hayatutatizi,
Ila ni ya viongozi, wanaofanza ajizi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Uongozi kama ngazi, ni kitu cha matumizi,
Asiyekuwa mjuzi, kuipanda kuna kazi,
Kuanguka kuko wazi, akashikwa kigugumizi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Watu wana zao hadhi, kwenye safu uongozi,
Kuna bora kiongozi, mradi kiti kaenzi,
Na uongozi azizi, unaisadifu ngazi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Muihesabu miezi, ya kutafuta walezi,
Fedha wasiokabidhi, ili waipate kazi,
Ila wanaomaizi, kufaa watu ndo kazi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Huwa hawajitangulizi, nyie huwa watangulizi,
Yao kwao sio wajenzi, hadi kwanza muwe wajenzi,
Chenu hawakinguzi, kuongeza ndio radhi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Yao hawayasogezi, hadi mnao ujenzi,
Kisha yakawa makazi, na riziki yawaezi,
Ndio hufata mapenzi, kutafuta utowezi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Hawakimbilii enzi, wanatafuta ujenzi,
Wawajenge kwa makazi, na utu ni yenu hadhi,
Kisha ndio wadarizi, mengine kujabarizi,
Tatizo si uongozi, tatizo ni viongozi !

Enzini wanaomwenzi



Msigeuke viazi, mbio kuota mizizi,
Ya wengine kuwa ngozi, nyie mkajidarizi,
Ya chini ikawa dozi, ya juu hamyawezi,
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Wenye fedha msienzi, katu hao si wajenzi,
Ni watu wa kujienzi, wepesi wa matanuzi,
Wanafanza uigizi, walipiwe matumizi,
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Ni wa rushwa waamuzi, mechi nyingi hawawezi,
Vya umma ni wadowezi, ila wakataa wizi,
Fahari ni yao njozi, na yote yaso azizi,
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Enzini wenye mapenzi, na umma kuhafidhi,
Ambao lao zoezi, ni jamii mapinduzi,
Wenyewe wasojienzi, ila fakiri waenzi,
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Hili lataka teuzi, na mazuri maamuzi,
Kukataa uenenezi, na ushauri wa juzi,
Eti kuachia ngazi, aipate mwanagenzi ?
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Wasitudhani machizi, au teja wapuuzi,
Wakayaona machozi,  imetuzidia dozi,
Nawaapia bazazi, ya kwao yote ni wazi,
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Si wa jana ni wa juzi, twalitoa pingamizi,
Watu wengine maradhi, nchi ikipata kazi,
Hufa kwacho kikohozi, cha uroho na uwizi,
Enzini wanaomwenzi, mtakikwepa kitanzi !

Bado kujitegemea




NANI amekuambia, doa kujitegemea,
Uongo ninakwambia, hiyo ni kubwa nazaa,
Hakika ya ujamaa, jambo hili ulijua,
Falsafa yatufaa, watu kujitegmea.

Komunisti si ujaamaa, tunapaswa kuelewa,
Wakiafrika ulikuwa, ni kuishi kijamaa,
Katika hilo tambua, ukwasi haujazuiwa,
Falsafa yatufaa, nchi kujitegmea.

Ila kinachotakiwa, sera zake kuandaa,
Pasiwe wa kufa njaa, watu wakachekelea,
Sasa inavyokuwa, ushindani twajionea,
Falsafa yatufaa, watu kujitegmea.

Washindana wajaliwa, na kucheka wasokuwa,
Mbio zingine udhia, za magari kununua,
Na majengo kuinua, mtu asikojikalia,
Falsafa yatufaa, nchi kujitegmea.

Israfu tunatia, na baraka kuengua,
Kiburi kimetujaa, na jeuri twatumia,
Hili halina ridhaa, adhabu naihofia,
Falsafa yatufaa, watu kujitegmea.

Demokrasi-jamaa, ndiyo inayotufaa,
Utajiri kuridhia, kwa umoja na wingi pia,
Ila tukayakataa, watu wetu kufa njaa,
Falsafa yatufaa, nchi kujitegmea.

Na mifumo kuibua, udhibiti maridhia,
Na miundo kuandaa, haki inayoridhia,
Kupata kutouziwa, na kukosa kuzuia,
Falsafa yatufaa, watu kujitegmea.

Watu wote twatakiwa, kwanza nyumba kupatia,
Inayofata hatua, fedha za kuwezeshea,
Kila mtu kuvumbua, lake la kujifanya,
Falsafa yatufaa, nchi kujitegmea.

Serikali yatakiwa, wajuzi kuwatumia,
Masoko kuyatambua. popote yalipokaa,
Na nini chatakiwa, jamii kuzalishia,
Falsafa yatufaa, watu kujitegmea.

Miaka imefikia, vitu kujitengezea,
Ni aibu kununua, trekta la Asia,
Amerika na Ulaya, watazidi kutwonea,
Falsafa yatufaa, nchi kujitegmea.

Mitambo ni kuamua, wenyewe kujiundia,
Nje tukitegemea, watakuja tuumbua,
Tuwe tunafikiria, kama vikwazo twawekewa,
Falsafa yatufaa, watu kujitegmea.

Bado kujitegemea, kubwa nuni Tanzania,
Hili tukizingatia, shuleni itarejea,
Na ada zikapungua, kwa jasho letu kutoa,
Falsafa yatufaa, nchi kujitegmea.


Ung'eng'e anayetia


TAHADHARI naitoa, kwa wasomi Tanzania,
Na wabunge nao pia, vikaoni wakikaa,
Kiingereza kutumia, lugha yenu mwabakia,
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Toka sasa kutambua, kamusi twandikiwa,
Lugha yetu kuijua, kila neno kutumia,
Vipi mnayatumia, maneno yasiyokuwa ?
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Kisomo shaka chatia, kila ninapowasikia,
Wasomi mngelikuwa, maneno mngeyajua,
Kila lugha kutumia, yake yanapotakiwa,
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Uvivu mkijitia, hadhi mnajishushia,
Ni watu wa kuilea, lugha yenu ilokuwa,
Nyie mnaichezea, na kufifanzia mzaha ?
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Kila nikiangalia, methali naikubalia,
Miti kweli pakijaa, wajenzi mtafulia,
Ndicho kinachotokea, hapa kwetu Tanzania,
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Kwani twayakimbilia, kitu yasiyotufaa,
Kisha tukayaachia, thamani yaliyokuwa,
Utadhania vichaa, au ndio twalaaniwa?
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Ung'eng'e sijakaaa, wenyewe kuutumia,
Nafasiye kuchukua, pale pakustahilia,
Ila sio kuchagua, lugha ya kujitegemea,
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !

Barru kutuangazia, Mushawari wa kung'aa,
Nuru machoni kutia, la kwetu kuangalia,
Si kidogo ilokuwa, kwayo mbali twafikia,
Ung'eng'e anayetia, kiswahilini abaka !


Vijana mkiamua



WINGI wenu twaujua, ndio wengi Tanzania,
Kura mkisajiliwa, nchi hii mwachukua,
Wakati umewadia, ajizi ni kuchelewa,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Mwtakiwa chini kaa, mikakati  kuizua,
Wengine mkiachia, mambo yenu kufulia,
Mida inshafikia, nchi yenu kuchukua,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Tena kwa demokrasia, bila nguvu kutumia,
Wajao kuwanunua, ya kwao kuitikia,
Mshiko kuuchukua, wengine mkachagua,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Chungueni yao nia, uzuri nauhofia,
Naamini wana mbaya, kitu wamedhamiria,
Utumwani kuwatia, vyao mkishajilia,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Ni mabwege mtakuwa, nafasi kutowaachia,
Mabavu wakatumia, nchi kujiongozea,
Ikawa kwetu balaa, kama ya Yugoslavia,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Hamsini wanafaa, umri walofikia,
Viongozi wenu kuwa, si zaidi kuzidia,
Akili zao ruia, bora hawataamua,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Ukubwa wanaunywea, na kokeni kuvutia,
Makubwa waazimia, hadi nchi kununua,
Mkenge mkiingia, watu wote twapotea,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Mirija yatapakaa, fukara kuwanyonyea,
Kisha zikazungushiwa, mikononi kurejea,
Kama vile wanapewa, chao wasichokijua,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Kila nikifikiria, nataka muweke nia,
Wengine kutowazuzua, wenyewe kujisimamia,
Ukubwa mmeingia, na sasa ni kuamua,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Makubwa kuyaamua, sasa kazi inakuwa,
Kwanza kuyafikiria, na kisha kujipimia,
Haki linalochukua, hilo kutolikataa,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Uwazi kuutumia, vyanzo vyote kuvijua,
Na nia ya wagombea, na waliowanunua,
Na nini wakusudia, nchi hii kufanzia,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Tarehe mkazitia, mambo kuyaangalia,
Na kama yasipotimia, kofia mkazivua,
Mkiipenda Tanzania, ni kisafi kuchagua,
Vijana mkiamua, nchi bora mtapata.

Mola ninawaombea, apate wabarikia,
Kweli mkiiamua, vingine haitakuwa,
Ni yenu demokrasia, budi kwenu kutumia,


KUTONUNULIWA




Wahariri mashujaa, nienzio Tanzania,
Nyaronyo namkumbatia, siwezi nikamuachia,
Mkataa kununuliwa, ni mhariri shujaa,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Wasiokuwa na njaa, vya watu wakababia,
Rahisi kununuliwa, wachovu kuwanunua,
Dhuluma wakailea, kiyama kuyajutia,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Dini sintoangalia, kote wananunuliwa,
Roho naiangalia, wito inayoitikia,
Haki kuisimamia, si shetani kumfaa,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Hawa kwangu ni shujaa, kwa nyingi huba na hawa,
Ninawapenda radhia, na heshima naitia,
Lao nitalisikia, na yao kujisomea,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Waongo waliokuwa, bwana kutumikia,
Kama mbwa kuja kuwa,  ovyo wanajibwekea,
Hao kwangu udhia, hata kama nawazaa,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Kwangu kina malkia, ukweli wanaujua,
Haki wanaitetea, na wanyonge kuwafaa,
Ila wanaotumiwa, kwangu mimi changudoa,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Fakiri ninajijua, wapi pakusimamia,
Kesho nimeshachagua, leo ninaiachia,
Wangu wanaonifaa,njia yangu kufatia,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Njiani wanaorudia, kuritadi wafanzia,
Siwezi wavumilia, wala kuwaangalia,
Nahesabu mfu wawa, kitu hawatatufaa,
Wahariri ushujaa, nyie kutonunuliwa !

Waandishi mkiamua




Kalamu mkiamua, bora itatupatia,
Ila mkinunuliwa, tunaenda kufulia,
Viumbe wenye hadaa, yao wanadhamiria,
Waandishi mkiamua, wahuni watakimbia !

Habarini kuwatia, bora watajidhania,
Kelele wakajitia, uchuzi waliokuwa,
Wao wanshanunuliwa, nanyi wanawanunua ?
Waandishi mkiamua, waja viongozi bora!

Hekima kuitumia, kwa mbele kuangalia,
Hawi asiyetambua, nini atatuibia,
Ikulu kukimbilia, fajiri latoka jua
Waandishi mkiamua, wahuni watakimbia !

Au leseni wapewa, ulinzi kuingilia,
Waliowatangulia, salama kujionea,
Hilo sintolielewa, lazima kufafanuliwa,
Waandishi mkiamua, waja viongozi bora!

Mwatakiwa kuchugua, watu walipoanzia,
Nini kiloamuliwa, na wakakubaliwa,
Sasa yanayotokea, dira ipi yachukua ?
Waandishi mkiamua, wahuni watakimbia !

Marikani kutuoa, Mchina atatwangalia,
Na Irani kumwatia, yake akajifanzia ?
Au Vietnam twawa, miaka inayoingia ?
Waandishi mkiamua, waja viongozi bora!

Vijipesa mkipewa, na vigari kutembelea,
Hivi mnajitambua, na yao mnayaelewa ?
Kipi wanachochukua, hadi wakawaridhia ?
Waandishi mkiamua, wahuni watakimbia !

Palipo na nzuri nia, gharama hapatingia,
Anayekaa kimya, wala mjinga hajawa,
Na kila munuliwa, kaziye ni kutumiwa,
Waandishi mkiamua, waja viongozi bora!

Mwatakiwa kuchagua, bora kitakachotufaa,
Hasara kisotutia, hadi amani kwachia,
Misingi mkililia, watu bora mtakuwa,
Waandishi mkiamua, wahuni watakimbia !

Saburi inatakiwa, si fedha kukimbilia,
Puani hukutokea, kesho ukazijutia,
Wana 'kija kuchinjiwa,na wewe kuhujumiwa,
Waandishi mkiamua, waja viongozi bora!

Saturday, October 20, 2012

S A D I K I






Sadiki yupo muumba, wa hii yetu dunia,

Viumbe ametuumba, yeye kututangulia,

Na ni kujitia kamba, kingine kuabudia,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki umekosea, na deni unadaiwa,

Hio ulichoamua, wala sawa haikuwa,

Mizani imefulia, uongo inakwambia,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki hujitambui, nafsi yakuchezea,

Na ulicho haujijui, kingine wakidhania,

Kila kukichwa matlai, washindwa kujitambua,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki wewe hujui, maho utayafungua,

Ukaitafuta rai, na ushauri kupewa,

Hakika ukijidai, utazidi kupotea,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki katika haki, utazika unafiki,

Usiwe ni mamluki, nafsi kutobariki,

Dhulumati hapendeki, malaika humshtaki,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki kwenye adili, hulka pasi mushkeli,

Ukaijua akili, ni chanzo cha ujahili,

Na pasinaye Adili, wewe kiumbe dhalili,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki bila ukweli, hubaki kiwiliwili,

Roho ikose fasili, ukianza udahili,

Makabiri zurtumuli, hudhihiri tu ukweli,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki huna imani, unaishi kwa rehani,

Yakini ni upofuni, uishio mskani,

Ukazungukwa na duni, wazidi kuvuta chini,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki ni meli wawa, na dira haukipewa,

Gizani umetokea, na gizani waelekea,

Na wanaokufuatia, lazima watapotea,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki hauelewi, moyo utafunguloiwa,

Nuru kwako haitui. pengine yaegemea,

Ni mapema asubuhi, nafsi unshapewa,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki kweli waua, ili yako kutimia,

Ujinga waununua, roho ukajiuzia,

Laiti ungelijua, katu haitatangulia,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki uongo dawa, vidonge unatumia,

Na teja umeshakua, bilavyo unaugua,

Upatacho hutumia, hata haramu kikiwa,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki umepgawa, ruhani akuchezea,

Maduguli kuibua, kichwani tukamtoa,

Mwenyewe ukijujua, uhuru utaujua,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki unapangua, cha kwako kukibomoa,

Na wanaokusaidia, si wazuri ni wabaya,

Wewe umeng'ang'ania, kama ndugu wamekuwa,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki huna kanuni, ovyo unajipitia,

Hautopata auni, bila kuacha udhia,

Unavaaje gauni, mwanamke hujakuwa,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki huna ratiba, mengi kwako ni kadhaba,

Imani yako haba, haitojaza kibaba,

Na huu kwetu msiba, twamgeukia Toba,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki una hamaki, kama mkizi samaki,

Na hauitaki iliki, mhemuko isolaki,

Kikulacho kikibaki, hapabakii rafiki,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki una kisasi, alicholaani Qudusi,

Kinacholea nuksi, kwa uchache wa durusi,

Iangale nafusi, maisha yana mikasi,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki sio bidhaa, kiumbe kununuliwa,

Kama ulikuwa ujuha, sasa kwanzia kataa,

Mola ukimrudia, haachi kukuangalia,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki yafa hekima, yafaa kuifufua,

Pasiyo kuna zahama, huizamisha dunia,

Na za kupikwa tuhuma, mwenyewe ukajiumbua,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki tupu busara, tupu labaki gunia,

Na duara walitia, kitu kisichotambua,

Unavyo visivyochanua, wala haviwi maua,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki unapotea, na hiyo si yako njia,

Kinyume unapitia, wenda kwingine tokea,

Na ukija uliziwa, uliko hawatajua,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki katika watu, usijifanye ni jitu,

Hatamki mtu kitu, yakawa ni kisu butu,

Kila analothubutu, huwa hachezi upatu,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Sadiki katika dua, Mola atakuafua,

Dhuluma anayejaliwa, na wake hudhulumiwa,

Na siku ikifikia, aibu huiogea,

Sadiki uyaamini, mtu bora utakuwa!



Tuesday, October 16, 2012

Laiti wangelijua



Laiti wangetambua, hili wangeazimia,
Watu wakawajengea, maadui kuwaua,
Watatu waliokuwa, ndiye wa kutegemewa,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Mengine kuwaachia, wenyewe watajifanzia,
Nyumba wakishajengewa, akili zitaingia,
Maajabu watazua, kwani wanafikiria,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Nchi kiwanja ikiwa, wote ni kujijengea,
Moja tu twaliwazia, na mengine kufifia,
Muda itatuchukua, maadui kuwaua,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Wa kwanza kumuondoa, ufukara atakuwa,
Kusepa ataridhia, afadhali  kumwachia,
Kisha akafuatia, maradhi mlaumiwa,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Kisha akafuatia, maradhi mlaumiwa,
Miundo mbinu ikiwa, uchafu inaondoa,
Usafi ukasambaa, ikawa ndiyo tabia,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Na muda utabakia, kinamama kujisomea,
Ujinga ukakimbia, huko unakokujua,
Na mama akishatambua, taifa zima hujua,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Halafu atafatia, maradhi mlaumiwa,
Nchi anayezingua, watu wetu wakavia,
Wengi wanaogua, washindwa kutuchangia,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Wao wasichoelewa, ni ajira mardhia,
Vijana kuajiriwa, kutengeneza vifaa,
Kila kimoja kikawa, mradi wa kujitegemea,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Udongo watachimbua, ajira kujipatia,
Ufinyanzi kuridhia, matofali kufyatua,
Na vigae navyo pia, wakawa wavitanzua,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Miti watainunua, Iringa kukachanua,
Milango wakaandaa, kwenye nyumba kuwekea,
Na madirisha kutoa, nakshi yaliyotiwa,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Taizi watachimbua, za vito zilizokuwa,
Sakafuni wakatia, nyumba zikapendezea,
Ni rahisi itakuwa, nchi hii kunyanyua,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Vijiji tutashitua, mara moja vikakua,
Usingizi kuondoa, wakazi kujiamkia,
Hili wakishangialia, kasi yao itakuwa,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Kasi yao itakuwa, ya kutaka endela,
Hakuna la kuzuia, umeme kudadavua,
Na maji wakachimbua, na bomba kwenda zitia,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Wapo wataopimia, maeneo kuhamia,
Eka wakaziandaa, si vidunchu kuachia,
Ili mtu kujilimia, vimbogamboga ikawa,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Viwili vitaanzia, au vitatu vikawa,
Vyumba vya kuingia, ibakie kutanua,
Mtu anavyoamua, ya kwake kuendelezea,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Ujasiriamali njia, watu wakaifuatia,
Hadi juu kufikia, na kheri kulikokuwa,
Wakawaka Tanzania, hadithi ikatimia,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?

Sasa kinachotakiwa, ni uchama kuua,
Sera wanaozikataa, ambazo zinatufaa,
Waache kujishaua, ugumba wakakataa,
Nyumba dawa mujarabu, laiti wangelijua ?


Wazee mwaaibika



WAADHIMU mnatakiwa, kwanza kuwa Watanzania,
Uchama ukafatia, na huko mnakotokea,
Vingine mkifuatia, vijana kutoelewa,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Tukilitoka mwajua, mbona dira mwakataa?
Hivi chini mmekaa, hali kuifikiria,
Au sawa mwadhania, vitu vinavyojiendea?
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Hadhi mnayotakiwa, si uchama kujaliwa,
Nyie ni Watanzania, kuongoza mwatakiwa,
Itikadi kuzipaa, juu juu kuelea,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Kila mnapofikiria, kufikiri Tanzania,
Vingine kutoamua, ila nchi kuifaa,
Vingine mkiamua, mtaiponza Tanzania,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Mafao mnayopewa, yanatoka Tanzania,
Sio chama chawafaa, hilo mngelitambua,
Wengine wakiingia, mkwara mtachukua,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Demokrasia dawa, bure mkiikataa,
Nyingine haitofaa, taifa litaumia,
Laiti mkiyajua, msimamo mtajua,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Siasa sio sanaa, kitu cha kujipitia,
Mtazamo watakiwa, na didra kuzitumia,
Vinginevyo 'kitokea, taifa wenda potea,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Budi mngepigania, bunge lenu kupatiwa,
La wazee wa kujua, nyadhifa mliopitia,
Katiba kuwatambua, maamuzi mkitoa,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Marais mmejaa, wa Bara na Zanzibar,
Mawaziri nao pia, ndani humo wangetiwa,
PIa wakuu wa mikoa, na wilaya walokuwa,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!

Na makatibu wakatua, wa wizara na mikoa,
Na mameneja wafaaa, bungeni wakaingia,
Kampuni walolea, na sifa kujipatia,
Kwa kuulea uchama, wazee mwaaibika!




Majoho si utukufu



Ukubwa si utukufu, waweza kuwa uhuni,
Na ndani kuna mikufu, ya hadaa na zaini,
Wako wengi maarufu, lakini kwa uhayawani,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Kuna mengine tarafu, kaibariki shetani,
Wakajitia shaufu, kuenziwa hadharani,
Lakini kwenye mabafu, wanaiziua imani,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Wanayaenzi machafu, hayo ndiyo madhumuni,
Katika yao madafu, hakunao ulaini,
Wasakao umaarufu, wautaka kuzaini,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Moyoni wana maghofu, ya haramu na shetani,
Hawanao uongofu, ila ni umajinuni,
Wadhani wana marefu, kumbe yafa ukingoni,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Hakika wa utukufu, huuoni duniani,
Twajaliwa udhaifu, na kujifanya yakini,
Tungelihoji maoni, mzuri haonekani,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Wataka yao sadifu, hata ya kimuumiani,
Wajitie wakunjufu, watu wakawazaini,
Yao yakishawakifu, mirija wakabaini,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Taifa likadhoofu, watu wakose amani,
Wachukiwe maarufu, kinyaa wawe kundini,
Ikawa mintaarafu, ni adawa kitalini,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!

Mwaisusa misahafu, haya mngelibaini,
Si ya jana ni arifu, yameanzia zamani,
Sasa mjitaarifu, mkarejea imani,
Majoho si utukufu, kuna mengine hadaa!


Kila mvaa kikoi



Utakuwa ni mafuu, kiumbe hujitambui,
Watu ukiwadharau, nao wangali ni hai,
Humjui wa nafuu, wakati ungali hai,
Mja usimdharau, kila mvaa kikoi!

Maisha sumu dharau,  kwa wengine haifai,
Hata ukipanda juu, ya chini huyakimbii,
Hata na wapanda nguu, kileleni hukinai,
Mja usimdharau, kila mvaa kikoi!

Majuto ni mjukuu, asiyesikia rai,
Usitafune tambuu, kwa mate kutujeruhi,
Huonekana bahau, na njia hautambui,
Mja usimdharau, kila mvaa kikoi!

Pumzi zetu kuukuu, tambaa la kukinai,
Mlima si kichuguu, japo wengi hawajui,
Hali sio dafrau, kuchagua hatujui,
Mja usimdharau, kila mvaa kikoi!

Wepesi wa kusahau, viumbe dunia hii,
Na haraka wa malau, hali neno hawajui,
Sambusa si kaukau, havilingani kwa bei,
Mja usimdharau, kila mvaa kikoi!

Ninaliachia dau, niendako sikujui,
Pepo hizi za nahau, niendapo kusabahi,
Naitafuta nafuu, mwenye nayo simjui,
Mja usimdharau, kila mvaa kikoi!


Nimealikwa karamu




WAMEZUKA chakaramu, mbinu wanazifahamu,
Wanialika karamu, sijui kinachogharimu,
Sio mimi ni kaumu, yatakiwa kujihimu,
Nimealikwa karamu, kula nyumba na magari !

Mualiko ni muhimu, ikulu wameshaazimu,
Na mimi sijifahamu, hivyo hivyo naazimu,
Ingawa huko kuzimu, nahisi wanalaumu,
Nimealikwa karamu, kula nyumba na magari !

Fikra hizi zidumu, au jama zisidumu ?
Vitu visivyo na damu, kuwa mlo wa karamu,
Kijani wamejihimu, mwilini wameazimu,
Nimealikwa karamu, kula nyumba na magari !

Kijani wameazimu, mwilini kwenda kaimu,
Na humo kwenye karamu, kitakuwa ni adimu,
Najiona mwenda wazimu, kukubali  ukarimu,
Nimealikwa karamu, kula nyumba na magari !

Tano sintowadhulumu, unatosha ukarimu,
Ninaiacha beramu, kutafakari salamu,
Mshumaa mashamushamu, waizimia kaumu?
Nimealikwa karamu, kula nyumba na magari !

Anayemanya Alamu, kwa hili kutogharimu,
Ila naiona haramu, yaathirika kaumu,
Njaa inatakadamu, pasina la kurehemu,
Nimealikwa karamu, kula nyumba na magari !

Bahati haina kwao



Aliyenayo hajui, kuidharau tabia,
Kazoea kama tui, kwenye wali kuitia,
Akawa haiwazii, hadi asiposikia,
Bahati haina kwao, kuhama matarajio!

Huingia pasi hodi, ndani ikakufuatia,
Wala sio kwa mrai, na nai kuipigia,
Wala haina ahadi, mara unaishtukia,
Bahati haina kwao, kupata matazamio!

Monday, October 15, 2012

V I J A N A L E O T A I F A



LAITI mkiamua, taifa leo vijana,

Hatua mtachukua, uoza kwondokana,

Nchi mkaifagia, kila kitu mkasana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Nchi inawangojea, kutumikia vijana,

Ndani mliochimbiwa, mso kitu cha maana,

Na nje mliokimbia, kuukataa utwana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Hamsini kutumia, sisi sasa si vijana,

Uzee unaingia,twafanana kama jana?

Kwa kuwa tunaachia, nchi inaumizana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Kazi tele zimejaa, tunaiona hiyana,

Ya kwanza yakuanzia, ni nyumba kujengeana,

Vijijini kuingia, kwa hali tukapambana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Wazee wanangojea, sadaka kupatikana,

Vijana ninawajua, Pongwe na Kimanzichana,

Nyenzo mkisaidiwa, nyumba zitaonekana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Na maji nayo pia, yaweza kupatikana,

Akili tukitumia, tukazingeneza zana,

Hizo za kununuliwa, ndizo zinazotubana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Miaka tulofikia, ni ya kutengeza zana,

Zote tunazotumia, maji yatapatikana,

Zoezi likaendelea, bila ya kukwamishana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Hadithi ukisikia, kukwama kupatikana,

Ni zana tumefulia, twangoja zitoke China,

Hali tukijitambua, kuunda yawezekana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Trekta ninajua, kuunda si kazi sana,

Moyo ndio watakiwa, na maono kuyaona,

Ombaomba kuzoea, hiana twafanyiana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Ardhi tutaifukua, tuweze kulima sana,

Chakula kujipatia, na kingine kuuuziana,

Marikani na Asia, nja tukatlizana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Uvuvi tunafulia, hapa pwani tunaona,

Samaki twashindwa vua, kwa udhia na hiana,

Misiri wameamua, jangwani wanapatikana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Misiri sasa wavua, jangwani kuna amana,

Yametuzunguka maziwa, sisi twasimangana,

Bahari twaiambaa, twavua pasipo zana ?

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Yote ukiangalia, uzee ndiyo hiana,

Kwaisha kufikiria, kwabaki kukimbizana,

Urais kufatia, haya, aibu hatuna,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Leo nimedhamiria, watu kuwachamba sana,

Utoto wanatutia, na upofu wa kutoona,

Wanaizuru dunia, hawana wanalovuna?

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Balozi tukiamua, hao wakawa vijana,

Elimu wataivua, na mbinu zenye kufana,

Wazee wajikalia, pipiefu kuivuns,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Balozi tukiachia, wakatawala vijana,

Ujuzi watahukua, kuja jenga mengi sana,

Nchi iwe yakimbia, si maktaimu kufwatana,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Wazee wang'ang'ania, tija wasipoitia,

Tukazidi kutambaa, badala ya kukimbia,

Ni udhia imekuwa, mwishowe unatakiwa,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Vijana ukiwalea, nyumba mnawaachia,

Waweze jisimamia, na hatua kuchukua,

Ya kwale wakiathiriwa, huja nyumba ikavia,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Vijana mmetimia, kwa wingi mmefikia,

Taifa mmeshakua, nchi inawasikia,

Hii ni demokrasia, idadi mshatimia,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !



Wenyewe mkizubaa, nchi watawaharibia,

Kifuu kitabakia, nazi nayo isokuwa,

Hata dafu maji kuwa, afadhali ingekuwa,

Vijana leo taifa, sio taifa la kesho !

M S I P O K I C H A G U A





Chama mkikiachia, kwenda kujipumzikia,

Haitakuwa nazaa, huenda mkabarikiwa,

Miaka kikaogea, na usafi kujitia,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



JIKI mkaitumia, kuyaondoa madoa,

Mizizi iliyokuwa, ya rushwa inayokomaa,

Halafu mkaondoa, na magugu kuyang'oa,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Kizazi kipya kutwaa, wazee mkawatoa,

Pembeni wakendakaa, wajukuu wakalea,

Sabini waliozaliwa, chama wakakichukua,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Muda huu watakiwa, chama kujajijengea,

Matawi mkafagia, uoza uliojaa,

Mbegu kujipandia, mpya zitakazokuwa,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Ubaya anayedhania, kifo hajakielewa,

Huku sio kujifia, bali upya kuzaliwa,

Wazee kama bidhaa, kwenye chama wamejaa,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Wazee kama bidhaa, na mzigo waliokuwa,

Kwenye chama wamejaa, ovyo wananunuliwa,

Ili hawa kuwaondoa, kushindwa kwenu ni njia,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Taifa kusaidia, nalo upya kujizaa,

safu zikapanguliwa, kilicho bora kwenziwa,

Yaliyovia manufaa, angalau kurejea,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



Hakuna cha kusifiwa, kila kitu wameua,

Kwao kilichobakia, ni sadaka kungojea,

Ombaomba wamekuwa, hatuwezi wategemea,

Hiki msipochagua, kikishindwa kupumzika:

Kikirudi nwachukua

na usafi kurejea

Nyie viongozi kuwa,

Tena kwa miaka mia!



WALIOPO WAMECHOKA



Wahitaji pumzika, akili kuzichochea,

Wameishachakarika, na wapambe wao pia,

Mengi yashindwa fanyika, watu wamejichokYea,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Wanafulia hakika, kifikra wanapotea,

Njia wanayoishika, ubayani yaelekea,

Nao hawana hakika, pazuri wanadhania,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Yanawapanda mahoka, maadui kuotea,

Na mabomu kutumika, watu wakawapofua,

Subira wanaizika, kwa maovu kuchimbua,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Kazi kulalamika, na uongo kuandaa,

Vijana mwahadaika, hawa wakiwanunua,

Azimio kutamka, uongozi kuchukua,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Wakati umeshafika, kilingeni kuingia,

Muongoze Afrika, kama Kabila kwanzia,

Nchi nzima ameshika, mtaishindwa mikoa?

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Ujana ni bora dawa, wazee mkitumia,

Wala sio kutumiwa, wakaganga yao njaa,

Kinyume mkiachia, mtakuja kujiua,

Wazee wameshachoka, sasa wanaganga njaa,



Wazee kazi yafaa, wajukuu kuwalea,

Ushauri wakatoa, na ya mbali kuwazia,

Ukuu ukiwaachia, hukataa kujifia,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Angola ukiangalia, haya utajionea,

Zimbwabwe nako pia, kizee ang'ang'ania,

Kwa haya kujikwepea, baibai kuwaambia,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Mikutanoni waingia, kuiganga yao njaa,

Akili zimepotea, vya uongo vinatiwa,

Na wakawakubalia, hasidi waliojaa,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Halmashauri waingia, ili ada kwenda pewa,

Watoto wakalipiwa, masomo kuendelea,

Waliwatuma Ulaya, hela zimeshawaishia,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Hapataisha udhia, hawa wakiendelea,

Ni watu wa kutumiwa, wengine wakadokoa,

Na macho tunajifia, vipi tutajionea,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Vijana wa Tanzania, umoja unatakiwa,

Uchama kuukimbia, udugu mkauzua,

Umoja wa Tanzania, vijana kujiundia,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Baba wanaofatia, na mama kuwalilia,

Kunyonya wasioachia, na jipya waiokuwa,

Hawa ni kuwaachia, iwafundishe dunia,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!



Kwa Mola nawaombea, muweze kufanikiwa,

Wazee kuwaondoa, ustawi mkauzua,

Na uvumbuzi nao pia, vifaavyo kugundua,

Waliopo wamechoka, waacheni wapumzike!

Enzi za upiga debe




VIJANA wa Tanzania, hivi sasa waamua,

Minyororo kuitoa, wazee kutumikia,

Uhuru kujipatia, na uongozi kutwaa,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Nchi waliochimbua, na dhahabu kuigawa,

Mashimo kutuachia, wala hai kufukiwa,

Wakageuka bidhaa, na nje kununuliwa,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Mikataba kukataa, na upya tukaanzia,

Uroho wasingekuwa, wote wangetunyanyua,

Nafsi kuwatangulia, leo wanajichukia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Wao walijifikiria, ya nchi wakaachia,

Imani hawakujaa, kesho yetu kwangalia,

Wao na walichozaa, ndicho muhimu kilikuwa,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Ufisadi waujua, huko ulikoanzia,

Mikono yashuhduia, kwavyo vipi kukataa,

Damu unatapakaa, wasema haujaua?

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Nchi wamezichukua, Uswizi kuzitupia,

Eti kimya wanakaa, lengo kulipotezea,

Wajua Watanzania, kumbukumbu hupotea,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Dowans wanawajua, TANESCO kuhujumiwa,

Siku walioyaanzia, unafiki kuutia,

Chama wanapalilia, sikumoja kuwafaa?

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Makampuni bandia, kazi yao ilikuwa,

Na mikataba kutia, uoza iliyokuwa,

Na wengine kutwambia, wataangusha mvua,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Mungu wakamchezea, kwa akili kujitia,

Wengi wanawanunua, na wao kununuliwa,

Nchi sokoni yatiwa, mchuuzi anangojewa,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Ndio ninawashtua, vijana kujizindua

Wazee mkiachia, vitani watawatia,

Roho zimekua mbaya, ukubwa kuulilia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Umungu wanajitia, wana kuwalimbikia,

Na vyeo kuwaptia, kina kilichozidia,

Mwalimu angeyajua, nchi asingewaachia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Maneno mengi watia, kumbukumbu isokuwa,

Machozi wanayotoa, ya mamba wamejaliwa,

Rohoni washangilia, kaondoka mjamaa,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Ubaya wanafukua, na mema kuyachimbia,

Mazuri wakidhania, yeye alishayajua,

Hugeuka ni ubaya, Dracula wa kuua,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Vijana wa Tanzania, wito kwenu nautoa,

Marufuku kutumiwa, watu debe kupigia,

Mwenzenu ni kuchagua, wa rika mliokuwa,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Mwenzenu ni kuchagua, wa rika aliyekuwa,

Mkaanza muandaa, nchi kuja ichukua,

Wakati umeshawadia, taifa kutopotea,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Ni haki kuwaondoa, wazee wasiofaa,

Ulafi waliojaa, uchu na kubwa tamaa,

Isiyoshibika njaa, sikuzote wanalia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Vyamani wanunuliwa, mfukoni wanatiwa,

Takataka wamekua, rahisi nchi kutoa,

Wageni kuwauzia, mkabaki mnalia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Wakati umewadia, miezi ya kuamua,

Rushwa mliopokea, kwenda kuishtakia,

Na waliochaguliwa, ngazi wakaziachia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Na kisha mkachagua, vijana kwenda gombea,

Rushwa mkiikataa, na usafi kuchagua,

Itaamka Tanzania, vijana kuwashangilia,

Enzi za upiga debe, hatima imefikia.



Mganga kajigangua






Qulu lany yuksibuna, lahuu laana huwa,

Aya iliyo bayana, tamko imeshatoa,

Sikuchelewa kuvuna, kupanda nawaachia,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!



Na dua alipokutana, mganga kajiumbua,

Kwa jicho twatazamana, mkubwa kanitajia,

Mwanaizaya mtwana, nikamhurumia,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!



Aliye na Maulana, malaika huwa'chia,

Vidole wakivikuna, udhia ukapotea,

Mie hofu kwangu sina, walinzi nawaachia,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!



Bure mnapotezana, katika hii dunia,

Moto mwaupuliza sana, wa kwenda kuungulia,

Kama haya mwayakana, afu nadra kupewa,

Mganga kajigangua, alipoikuta dua!





Saturday, October 13, 2012

CCM 2012



Hii leo itakuwa, tarehe inafikia,

Kumi na tatu tarihia, na miaka kesho pia,

Kumbukumbu kuitia, na bora kudadavua,

CCM ilishaaga, hii ya leo si ya jana !



Kuna kundi lanuia, uoza kzungushia,

Juu huko lakotea, na mema kusikokuwa,

Mikosi inakotokea, nuksani na balaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Waua demkrasia, ndiko wanakotokea,

Chama kinawavumilia, na yao kuyasikia,

Walitoa wanatwaa, kama walivyonuia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Uoza tuliachia, ndani ukajitandia,

Baba alipotwachia, hii ya sasa kadhia,

Wajumbe kununuliwa, na mifuko walojaa,

CCM ilishaaga, hii ya leo si ya jana !



Chama sasa kimekua, ni kinara wa rushuwa,

Kwa huko kweza ingia, nchi nzima kuenea,

Wenyewe tunalilea, bomu la kujilipua,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Fisadi tunawajua, ni swahiba wamekuwa,

Mwalimu atulilia, sisi tunashangilia ?

Kadhaa ya kutapeliwa, na nchi wanaonunua,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Hao wanaonunua, nao wameshanunuliwa,

Na bei yaoghofya, masikini wenye njaa,

Kiazi utadhania, wala ndizi haijawa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Ganzi imeshatiwa, na nyenzo waliotoa,

Kadhia kutapeliwa, na viranja wenye njaa,

Mikoa wainunua, shibe ilikopotea,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Chama tukakiachia, hasidi kukichukua,

Wapendao kuchafua, na wengine kufagia,

Matope wamekitia, na tope tunaogea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Hii si ilyokuwa, hiki ni kitu kipya,

Kama ktu chazaliwa, kipo kilichojifia,

Na zamani nagundua, uhai kishautoa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Kama kufa inshakuwa, yabaki kufufuliwa,

Ibra nazingatia, vigumu haitakuwa,

Ila pawe nayo nia, ukweli kutangulia,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Chama kimenipotea, mimi kilichonilea,

Na shuleni kunitia, bure nikajisomea,

Yatima sikuachiwa, mtaani kuteketea,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Chama nimekiachia, asili wasiojua,

Sasa wakichakachua, sio kile kimekuwa,

Hiki kabisa kipya, nami ninakikataa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Yusiligi nilikua, katibu kutumikia,

Msingi nilipokuwa, asili ninaijua,

Moshi -Arusha najua, kwa mguu nilitembea,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Moshi-Arusha tambua, kwa mguu niltembea,

Azimio kusifia, na Mwalimu kumjua,

Kauli ninayojua, si hiki kilichokuwa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Kauli sio sawia, wenzetu wanazotoa,

Watumia kusikia, washindwa kujionea,

Taifa linaugua, chama chetu kuugua,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Nani angetumia, fedha kujipalilia,

Mwalimu akamwachia, chamani akaingia,

Kinyume imeshakua, wapendwa wenye kujaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Wadhibiti watakiwa, chama kuja kichungua,

Ukweli tukaujua, na pumba kuziachia,

Na nje wakitokea, bora sana itakuwa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Wachawi wakawajua, walozi waliokuwa,

Wanaotuharibia, chama kilichojaliwa,

Na kukifanya udhia, watu wakakichukia,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Hivi vipi inakuwa, wachache kukubalia,

Chama kutuharibia, na jina kulichafua,

Ushindi ukapotea, kwa uoza kung'ang'ania?

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Au wawe ni jamaa, toka kwenye familia,

Udugu unatitia, magugu yanaingia,

Kama vile wafulia, mengine kuyasomea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Muda nimevumilia, ila sasa nayatoa,

Ndani wanaojitambua, chama waje kuokoa,

Njia kimeshapotea, na bado kinaendelea?

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Siasa ninayojua, chama bora huchukua,

Watu wake huchagua, kama mchele ikawa,

Jiwe kutokubakia, kwa hadhari kuondoa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Kelele tumechagua, si busara twatumia,

Vishindo tunavijua, mikakati yapungua,

Na vijiji vyaugua, ngome ya kutegemewa?

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Ya juu twaangalia, ya chini yanazolewa?

Na wajanja tumezaa, kweupe watuhadaa,

Sherehe wazitumia, uchafu kuufagia!

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Nendeni kwenye mitaa, watu mkawasikia,

Vijana wa Tanzania, na wazazi wao pia,

Lawama wanazotoa, salama haitakuwa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Tabaka tumeibua, na zinazidi kukua,

Kuna watu watumia, milioni kulelea,

Hali wengi wamejaa, mia inawakimbia,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Ghorofa tunapaua, nyasi zinaendelea,

Vijiji vinafulia, vyabakia kuogelea,

Matope wanajinywea, eti tumeendelea?

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Wengi ninawashangaa, giza kulalamikia,

Kuna Watanzania, taa wasiozijua,

Vijinga wanatumia, na moto wa kukokea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Kuna watu waingia, haramia wanakuwa,

Chama washikilia, wengine wanazuia,

Hodi ukijigongea, mlango hutofunguliwa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Matawi sasa rejea, taka za kurejelewa,

Kikundi kinachokua, hatamu kutoachia,

Kama kama kinavia, na hasara kinakuwa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Ushirikina wazua, watu ghafla kwugua,

Wengine wanajifia, ofisini wamekaa,

Watu wanakihofia, huku chini kuingia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Na juu nakuhofia, hadithi moja ikawa,

Imepotea ridhaa, masikini kuondoa,

Mizizi tumeing'oa, muhali mmea kukua,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Hoja zimejiozea, sasa tunazotumia,

Na mbinu zimeshapwaya, mpya zinatakiwa,

Mikakati kuifua, sasa budi itakuwa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Hiki kizazi kipya, ujanja kitazidia,

Palipochimbiwa si dawa, wao watapafukua,

Kilichofichwa si dia, wao watakifichua,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Na teknohama twavia, tovuti kutotumia,

Matawi yanasinyaa, yaambaa teknolojia,

Wakati umeshawadia, vitu hivi kutumia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Chama imara kikiwa, ni imara Tanzania,

Kudhoofu tukiachia, watu watatunyanyapaa,

Na hazina imejaa, chama hiki kuokoa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Sasa kinachotakiwa, ni vizuri kuchagua,

Watendaji nadhania, ni bora kuajiriwa,

Sio kuchaguliwa, ili miaka kukaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Hata gani kuchagua, nani atamwagilia,

Wote wanaokimbilia, unafsi tupu wajaa,

Yao wanakimbilia, sio chama kuokoa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Chama ninachokijua, sio tunachojionea,

Hiki ni chama kipya, kile kilishajifia,

Na kaburini kutiwa, toka Mwinyi kuingia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Dereva nyuma kakaa, adhani anatembea,

Kumbe kinchotembea, mengine yajipitia,

Siri wameigudnua, hili bovu limekua,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Wanalazimisha ndoa, umoja zisizokuwa,

Kauli ukisikia, amani hutoijua,

Na sasa twajionea, sinema yaendelea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Walzika ujamaa, kwa zao kubwa tamaa,

Wanyonge wamewatoa, wenye fedha wabakia,

Chama kimeshajiua, kwa viongozi kununuliwa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Ni jina limebakia, maudhui wameng'oa,

Ubaba umepakuliwa, na ubwabwa kupikia,

Kisha wamefunikia, na udugu kuutia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Chama kilichowatetea, wanyonge wa Tanzania,

Hamna, kimejifia, rangi tu zinabakia,

Mawaridi na maua, kila rangi kujitia,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Cha tajiri kimekua, watu waliowaibia,

Mafuta wayatumia, mwilini waliyotutoa,

Wenyewe kutukangia, hadi tunaungulia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Mkuu katuambia, kabla tutajifia,

Amin, twaitikia, mbona walishatangulia,

Wafu wameshabakia, ingawa wanatembea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Na nyie mnaongojea, jidude kujipasua,

Kugawika hadi kuwa, viwili vimetokea,

Ni ujinga mwatumia, chama kilishajifia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Gamba tu linabakia, makombo kukimbilia,

Wenye pesa kuachiwa, wazidi kukokotoa,

Uoza inshakuwa, samaki wajiozea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Kwani hamkulijua, mmoja ukimuachia,

Samaki kujiozea, pakachani kubakia,

Huoza wote pamoya, pasiwe wa kuokoa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Ndivyo ilivyotokea, fisadi walipobakia,

Magamba wakakataa, kamwe hawataondoa,

Uoza uksambaa, kinanuka Tanzania,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Nani watamchagua, kuoza akakataa,

Uozo sasa ni ndoa, ya Katoliki imekua,

Pete kidole kutia, kuachwa haitatokea,

CCM ilishakufa, kigawike chama gani!



Vijana wanafulia, uoza kuegemea,

Kelele wajipigia, za kwenda kujiozea,

Waamka Tanzania, uoza hawatachagua,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Mwalimu aliwausia, uoza kutochagua,

Na majina wawajua, na vyeo walivyokuwa,

Na tabia ilokuwa, imezidi endelea,

CCM ilishakufa, kigawike chama gani!



Na tabia ilokuwa, imezidi endelea,

Makilla katuambia, toka zamani najua,

Nasi hatukumsikia, na sasa tunajionea!

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Chama wanaongojea, eti kujifaragua,

KIkagawika kwa nia, na shabaha nisojua,

Hilo katu nakataa, leo halitatokea,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Kuna wazungu wa njaa, chakula wanakigawa,

Maana wamedhamiria, ya kwao kuyatungua,

Kwa kutumia majuha, nchini waliojaa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Ah, nchi yangu yaumia, na chama nakillia,

Ukiwa chaniachia, sina wa kutumainia,

Ndugu na zangu jamaa, sasa tumeondokewa,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Haukuwa ujamaa, bali siasa za sawa,

Na hili kulikataa, kitali kimeanzia,

Haki ikishauawa, hubatilika ridhaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Haukuwa ujamaa, ila mnyonge kufaa,

Neti ndogo ukitoa, mapapa tu utavua,

Ndilo linalotokea, chamani waliojaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Huridhishi yao njaa, ya kuzidi limbikia,

Wataka kujipanua, na kuimega dunia,

Mbio wanazikimbia, za utajiri kutwaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Olympiki twafulia, ubepari wa sinzia,

Umma unaoibia, wenyewe ukajifaa,

Pikipoketi twazaa, bila ya kujitambua,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Nchi tumeiachia, mirija inachimbiwa,

Na kupe watapakaa, kwa kushoto na kulia,

Mapenzi waliyojaa, mali asili kutwaa,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Twadhani watujengea, kumbe watubomolea,

Na ulinzi twautoa, waendelee bomoa,

Ni ajabu ilokuwa, utadhani ni ruia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Atuongoe Jalia, mtu kutotegmea,

Yeye kumgeukia, ndiyo tutafanikiwa,

Vingine ninawaambia, tunaenda kufulia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Kama Mungu twamchagua, binadamu wa dunia,

Mola hatatukatalia, huyo atatuachia,

Ila vyeka kuchukua, utupu tukabakia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Mwalimu kanibarikia, mkono kichwani kutia,

Mdogo nilipokuwa, na adhima naijua,

Jinsi nilivyojisikia, na hivi leo nalia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Huyu tunayemtegemea, aachiwe kutufaa,

Kiumbe ni muishiwa, hata kama bilionea,

Siki haitakawia, Ugiriki kufikia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Njo'ni msionunuliwa, chama chenu kuokoa,

Mashinani kuanzia, pia zote jumuiya,

Kifo kweli kitakuwa, hali mnaangalia,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Njooni na mashujaa, ukweli mnaojua,

Chama kukipigania, safu bora kuzizua,

Na kuondoa udhia, aibu nayo kinaya,

CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?



Vijana wa Tanzania, hofuni kununuliwa,

Wenyewe mtajiua, mashaka mkaingia,

Na chama cha kuanzia, wenyewe mnakijua,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Kamati zikinunuliwa, na halmashauri nayo pia,

Nini kitakachobakia, kuuzwa kwa Tanzania,

Ni mtego twawekewa, budi sasa kutegua,

CCM ilishakufa, kife tena chama gani?



Mkutano wabakia, mkuu uliokuwa,

Mifuko watachukua, wajumbe kuwanunua,

Tajiri waliokuwa, trilioni wavuna kwa saa,

Matajiri wameua, CCM tuliyoijua!





Ndimi nisiye na baba wala mama,

(Mwana TANU na CCM ya zamani.)



Shemeji wenye hasidi






Ndoa zao huwa viza, na kitu wasifaidi,

Shemeji wanaoiza, za wengine kuhasidi,

Hata wanaojifanza, ni wa kweli maabudi,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Uwapende kama udi, na ubani kufukiza,

Roho imejaa tadi, yako hawachi kukwaza,

Wakaidhania sudi, kwao watatengeneza,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Nduguwe watawaponza, wawageuze gaidi,

Huhodhi nguvu za giza, kuwapandisha mdadi,

Kisha wakawachuuza, dini yao kuritadi,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Hao sio maliwaza, bali ni ya moto radi,

Ni adui sio wenza, ndoa wanaifasidi,

Na ni mkubwa muweza, yote kwao ni nakidi,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Hawamwogopi abadi, japo ibada wafanza,

Nyoyoni wameshadidi, ubaya kwako kufanza,

Na siku huja abadi, wenyewe kujilemaza,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Roho mbaya yao jadi, ndilo wanaloliweza,

Uhuni na ukuwadi, nyumba yao hutengeza,

Hakika hawafaidi, hata Idi huwazoza,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Wenyewe hujimaliza, wakadhani wafaidi,

Wivu huwa wawaponza, unaozaa hasadi,

Na kila wanalofanza, liwe halitaradadi,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!



Hili sio muujiza, falaqi inaahidi,

Akili anayetunza, na imani kuhimidi,

Humuogopa Muweza, wakaihofu hasadi,

Shemeji wenye hasidi, ndoa zao huwa viza!





CCM 2012




Hii leo itakuwa, tarehe inafikia,
Kumi na tatu tarihia, na miaka kesho pia,
Kumbukumbu kuitia, na bora kudadavua,
CCM ilishaaga, hii ya leo si ya jana !

Kuna kundi lanuia, uoza kzungushia,
Juu huko lakotea, na mema kusikokuwa,
Mikosi inakotokea, nuksani na balaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Waua demkrasia, ndiko wanakotokea,
Chama kinawavumilia, na yao kuyasikia,
Walitoa wanatwaa, kama walivyonuia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Uoza tuliachia, ndani ukajitandia,
Baba alipotwachia, hii ya sasa kadhia,
Wajumbe kununuliwa, na mifuko walojaa,
CCM ilishaaga, hii ya leo si ya jana !

Chama sasa kimekua, ni kinara wa rushuwa,
Kwa huko kweza ingia, nchi nzima kuenea,
Wenyewe tunalilea, bomu la kujilipua,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Fisadi tunawajua, ni swahiba wamekuwa,
Mwalimu atulilia, sisi tunashangilia ?
Kadhaa ya kutapeliwa, na nchi wanaonunua,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Hao wanaonunua, nao wameshanunuliwa,
Na bei yaoghofya, masikini wenye njaa,
Kiazi utadhania, wala ndizi haijawa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Ganzi imeshatiwa, na nyenzo waliotoa,
Kadhia kutapeliwa, na viranja wenye njaa,
Mikoa wainunua, shibe ilikopotea,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Chama tukakiachia, hasidi kukichukua,
Wapendao kuchafua, na wengine kufagia,
Matope wamekitia, na tope tunaogea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Hii si ilyokuwa, hiki ni kitu kipya,
Kama ktu chazaliwa, kipo kilichojifia,
Na zamani nagundua, uhai kishautoa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Kama kufa inshakuwa, yabaki kufufuliwa,
Ibra nazingatia, vigumu haitakuwa,
Ila pawe nayo nia, ukweli kutangulia,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?
Chama kimenipotea, mimi kilichonilea,
Na shuleni kunitia, bure nikajisomea,
Yatima sikuachiwa, mtaani kuteketea,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Chama nimekiachia, asili wasiojua,
Sasa wakichakachua, sio kile kimekuwa,
Hiki kabisa kipya, nami ninakikataa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Yusiligi nilikua, katibu kutumikia,
Msingi nilipokuwa, asili ninaijua,
Moshi -Arusha najua, kwa mguu nilitembea,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Moshi-Arusha tambua, kwa mguu niltembea,
Azimio kusifia, na Mwalimu kumjua,
Kauli ninayojua, si hiki kilichokuwa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Kauli sio sawia, wenzetu wanazotoa,
Watumia kusikia, washindwa kujionea,
Taifa linaugua, chama chetu kuugua,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Nani angetumia, fedha kujipalilia,
Mwalimu akamwachia, chamani akaingia,
Kinyume imeshakua, wapendwa wenye kujaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Wadhibiti watakiwa, chama kuja kichungua,
Ukweli tukaujua, na pumba kuziachia,
Na nje wakitokea, bora sana itakuwa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Wachawi wakawajua, walozi waliokuwa,
Wanaotuharibia, chama kilichojaliwa,
Na kukifanya udhia, watu wakakichukia,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Hivi vipi inakuwa, wachache kukubalia,
Chama kutuharibia, na jina kulichafua,
Ushindi ukapotea, kwa uoza kung'ang'ania?
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Au wawe ni jamaa, toka kwenye familia,
Udugu unatitia, magugu yanaingia,
Kama vile wafulia, mengine  kuyasomea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Muda nimevumilia, ila sasa nayatoa,
Ndani wanaojitambua, chama waje kuokoa,
Njia kimeshapotea, na bado kinaendelea?
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Siasa ninayojua, chama bora huchukua,
Watu wake huchagua, kama mchele ikawa,
Jiwe kutokubakia, kwa hadhari kuondoa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Kelele tumechagua, si busara twatumia,
Vishindo tunavijua, mikakati yapungua,
Na vijiji vyaugua, ngome ya kutegemewa?
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Ya juu twaangalia, ya chini yanazolewa?
Na wajanja tumezaa, kweupe watuhadaa,
Sherehe wazitumia, uchafu kuufagia!
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Nendeni kwenye mitaa, watu mkawasikia,
Vijana wa Tanzania, na wazazi wao pia,
Lawama wanazotoa, salama haitakuwa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Tabaka tumeibua, na zinazidi kukua,
Kuna watu watumia, milioni kulelea,
Hali wengi wamejaa, mia inawakimbia,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Ghorofa tunapaua, nyasi zinaendelea,
Vijiji vinafulia, vyabakia kuogelea,
Matope wanajinywea, eti tumeendelea?
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Wengi ninawashangaa, giza kulalamikia,
Kuna Watanzania, taa wasiozijua,
Vijinga wanatumia, na moto wa kukokea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Kuna watu waingia, haramia wanakuwa,
Chama washikilia, wengine wanazuia,
Hodi ukijigongea, mlango hutofunguliwa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Matawi sasa rejea, taka za kurejelewa,
Kikundi kinachokua, hatamu kutoachia,
Kama kama kinavia, na hasara kinakuwa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Ushirikina wazua, watu ghafla kwugua,
Wengine wanajifia, ofisini wamekaa,
Watu wanakihofia, huku chini kuingia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Na juu nakuhofia, hadithi moja ikawa,
Imepotea ridhaa, masikini kuondoa,
Mizizi tumeing'oa, muhali mmea kukua,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Hoja zimejiozea, sasa tunazotumia,
Na mbinu zimeshapwaya, mpya zinatakiwa,
Mikakati kuifua, sasa budi itakuwa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Hiki kizazi kipya, ujanja kitazidia,
Palipochimbiwa si dawa, wao watapafukua,
Kilichofichwa si dia, wao watakifichua,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Na teknohama twavia, tovuti kutotumia,
Matawi yanasinyaa, yaambaa teknolojia,
Wakati umeshawadia, vitu hivi kutumia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Chama imara kikiwa, ni imara Tanzania,
Kudhoofu tukiachia, watu watatunyanyapaa,
Na hazina imejaa, chama hiki kuokoa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Sasa kinachotakiwa, ni vizuri kuchagua,
Watendaji nadhania, ni bora kuajiriwa,
Sio kuchaguliwa, ili miaka kukaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Hata gani kuchagua, nani atamwagilia,
Wote wanaokimbilia, unafsi tupu wajaa,
Yao wanakimbilia, sio chama kuokoa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Chama ninachokijua, sio tunachojionea,
Hiki ni chama kipya, kile kilishajifia,
Na kaburini kutiwa, toka Mwinyi kuingia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Dereva nyuma kakaa, adhani anatembea,
Kumbe kinchotembea, mengine yajipitia,
Siri wameigudnua, hili bovu limekua,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Wanalazimisha ndoa, umoja zisizokuwa,
Kauli ukisikia, amani hutoijua,
Na sasa twajionea, sinema yaendelea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Walzika ujamaa, kwa zao kubwa tamaa,
Wanyonge wamewatoa, wenye fedha wabakia,
Chama kimeshajiua, kwa viongozi kununuliwa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Ni jina limebakia, maudhui wameng'oa,
Ubaba umepakuliwa, na ubwabwa kupikia,
Kisha wamefunikia, na udugu kuutia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Chama kilichowatetea, wanyonge wa Tanzania,
Hamna, kimejifia, rangi tu zinabakia,
Mawaridi na maua, kila rangi kujitia,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Cha tajiri kimekua, watu waliowaibia,
Mafuta wayatumia, mwilini waliyotutoa,
Wenyewe kutukangia, hadi tunaungulia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Mkuu katuambia, kabla tutajifia,
Amin, twaitikia, mbona walishatangulia,
Wafu wameshabakia, ingawa wanatembea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Na nyie mnaongojea, jidude kujipasua,
Kugawika hadi kuwa, viwili vimetokea,
Ni ujinga mwatumia, chama kilishajifia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Gamba tu linabakia, makombo kukimbilia,
Wenye pesa kuachiwa, wazidi kukokotoa,
Uoza inshakuwa, samaki wajiozea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Kwani hamkulijua, mmoja ukimuachia,
Samaki kujiozea, pakachani kubakia,
Huoza wote pamoya, pasiwe wa kuokoa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Ndivyo ilivyotokea, fisadi walipobakia,
Magamba wakakataa, kamwe hawataondoa,
Uoza uksambaa, kinanuka Tanzania,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Nani watamchagua, kuoza akakataa,
Uozo sasa ni ndoa, ya Katoliki imekua,
Pete kidole kutia, kuachwa haitatokea,
CCM ilishakufa, kigawike chama gani!

Vijana wanafulia, uoza kuegemea,
Kelele wajipigia, za kwenda kujiozea,
Waamka Tanzania, uoza hawatachagua,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Mwalimu aliwausia, uoza kutochagua,
Na majina wawajua, na vyeo walivyokuwa,
Na tabia ilokuwa, imezidi endelea,
CCM ilishakufa, kigawike chama gani!

Na tabia ilokuwa, imezidi endelea,
Makilla katuambia, toka zamani najua,
Nasi hatukumsikia, na sasa tunajionea!
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Chama wanaongojea, eti kujifaragua,
KIkagawika kwa nia, na shabaha nisojua,
Hilo katu nakataa, leo halitatokea,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Kuna wazungu wa njaa, chakula wanakigawa,
Maana wamedhamiria, ya kwao kuyatungua,
Kwa kutumia majuha, nchini waliojaa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Ah, nchi yangu yaumia, na chama nakillia,
Ukiwa chaniachia, sina wa kutumainia,
Ndugu na zangu jamaa, sasa tumeondokewa,
CCM ilishakufa, kife tena mara ngapi ?

Haukuwa ujamaa, bali siasa za sawa,
Na hili kulikataa, kitali kimeanzia,
Haki ikishauawa, hubatilika ridhaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Haukuwa ujamaa, ila mnyonge kufaa,
Neti ndogo ukitoa, mapapa tu utavua,
Ndilo linalotokea, chamani waliojaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Huridhishi yao njaa, ya kuzidi limbikia,
Wataka kujipanua, na kuimega dunia,
Mbio wanazikimbia, za utajiri kutwaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Olympiki twafulia, ubepari wa sinzia,
Umma unaoibia, wenyewe ukajifaa,
Pikipoketi twazaa, bila ya kujitambua,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Nchi tumeiachia, mirija inachimbiwa,
Na kupe watapakaa, kwa kushoto na kulia,
Mapenzi waliyojaa, mali asili kutwaa,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Twadhani watujengea, kumbe watubomolea,
Na ulinzi twautoa, waendelee bomoa,
Ni ajabu ilokuwa, utadhani ni ruia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Atuongoe Jalia, mtu kutotegmea,
Yeye kumgeukia, ndiyo tutafanikiwa,
Vingine ninawaambia, tunaenda kufulia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Kama Mungu twamchagua, binadamu wa dunia,
Mola hatatukatalia, huyo atatuachia,
Ila vyeka kuchukua, utupu tukabakia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Mwalimu kanibarikia, mkono kichwani kutia,
Mdogo nilipokuwa, na adhima naijua,
Jinsi nilivyojisikia, na hivi leo nalia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Huyu tunayemtegemea, aachiwe kutufaa,
Kiumbe ni muishiwa, hata kama bilionea,
Siki haitakawia, Ugiriki kufikia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Njo'ni msionunuliwa, chama chenu kuokoa,
Mashinani kuanzia, pia zote jumuiya,
Kifo  kweli kitakuwa, hali mnaangalia,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Njooni na mashujaa, ukweli mnaojua,
Chama kukipigania, safu bora kuzizua,
Na kuondoa udhia, aibu nayo kinaya,
CCM ilishakufa, kife tena mara

ngapi ?

Vijana wa Tanzania, hofuni kununuliwa,
Wenyewe mtajiua, mashaka mkaingia,
Na chama cha kuanzia, wenyewe mnakijua,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Kamati zikinunuliwa, na halmashauri nayo pia,
Nini kitakachobakia, kuuzwa kwa Tanzania,
Ni mtego twawekewa, budi sasa kutegua,
CCM ilishakufa, kife tena chama gani?

Mkutano wabakia, mkuu uliokuwa,
Mifuko watachukua, wajumbe kuwanunua,
Tajiri waliokuwa, trilioni wavuna kwa saa,
Matajiri wameua, CCM tuliyoijua!


Ndimi nisiye na baba wala mama,
(Mwana TANU  na CCM ya zamani.)