Wednesday, August 29, 2012

USITUPE VIONGOZI


USITUPE VIONGOZI ....


KAMA wapo waondoe, safu zikasafishika,
Kisha usitujalie, mamlakani kuwaweka,
Nasi utuhurumie, tusiwe wa kuteseka,
Usitupe viongozi, waliokuwa fisadi!

Marafiki na mashoga, jamaa hao dhihaka,
Kaumu Lutu kubwaga, yakini kusalimika,
Wageuze ni maboga, na tembo kukanyagika,
Usitupe viongozi, marafiki na mashoga!

Wazungu waabuduo, na Usa-haa nao pia,
Tuwe tuwatapikao, yakwao tukayazoa,
Wawe wabakiao, ni rafiki wa kukaa,
Usitupe viongozi, waabuduo Wazungu!

Vijiji vinaugua, nani kuviangalia,
Hata maji wachimbua, badala ya kufungulia,
Huu mkubwa ukiwa, viongozi kama hawa,
Usitupe viongozi, vijiji wasiojali!

Wenyewe wajipendelea, wao na zao jamaa,
Wazee wawatezea, uzeeni kuumia,
Ahadi wakazitoa, hamsini zisokuwa,
Usitupe viongozi, wazee wasiotunza!

Huwatumia vijana, kufata yao mapenzi,
Ila kutenda ya maana, kwalo hawana ujuzi,
Maisha duni waona, vijana kukosa kazi,
Usitupe viongozi, vijana wasiothamini!

Waliojaa hadaa, kuwazaini raia,
Mola kutotujalia, na kama wapo ondoa,
Hii ni ya umma dua, Muumba wetu sikia,
Usitupe viongozi, wadanganyao wananchi!

Wala rushwa ni balaa, hasa chama kupitia,
Hawaoni ni udhia, nchi watajiuzia,
Watumwa raia kuwa, upya wakatawaliwa,
Usitupe viongozi, ambao ni wala rushwa!

Tuepushe na balaa, kwa kuwadi kujaliwa,
Na wezi wenye ubia, vya nchi wakachomoa,
Ni vibaka walokuwa, ukubwa wautumia,
Usitupe viongozi, wanaokula na wezi!

Ubabe wanaotumia, huja kuzusha ghasia,
Hasira ikipasua, hakuna wa kutuokoa,
Kila mtu kukimbia, kwenye moto tukatua,
Usitupe viongozi, ubabe wanaojitia!

Saini wanazitia, wakubwa waliokuwa,
Fedha wakazidokoa, benkini zilizokaa,
Na dhahabu kuitwaa, binafsi ikawafaa,
Usitupe viongozi, benki kuu waibao!

Kuna walevi wajaa, irabu ni kutumia,
Shilingi wakiijua, huko watachokonoa,
Na akiba kuitoa, ikaenda kupotea,
Usitupe viongozi, walevi wa kutumia!

Wasiokuwa na haya, nao sasa wamejaa,
Aibu imeshawagwaya, na soni yawakimbia,
Waweza kujifanyia, hata usofikiria,
Usitupe viongozi, hayawani walokuwa!

Raia wanaoibia, uwaangaze Jalia,
Katu kutokuwaachia, ovyo wakatutendea,
Ufakiri kututia, na nusura kutojua,
Usitupe viongozi, raia wanaoua!

Dhuluma tunazijua, hai walotufanzia,
Na marehemu kadhia, hata nao waijua,
Hawa kiwaangazia, utaijua hidaya,
Usitupe viongozi, dhuluma waliojaa!

Wanaabudu dunia, vichaa waliokuwa,
Wao wakajidhania, milele wataikaa,
Na kufa kutoridhia, wengine wakawaua,
Usitupe viongozi, waabuduo dunia!

Ving'ang'anizi balaa, hawafai Tanzania,
Nafasi waliotwaa, watake tena rudia,
Hao ni kuwafagia, pembeni wakazolewa,
Usitupe viongozi, ving'ang'anizi wakubwa!

Mabomu wanaotumia, kupiga ovyo raia,
Na dola kuitumia, vibaya isivyokuwa,
Mkoloni bora kuwa, hao ni wa kuwaondoa,
Usitupe viongozi, raia waumizao!

Akili waliofubaa, kuzua wasiojua,
Mirija wakaachia, vya kwetu ikajinywea,
Sisi kutojipatia, chungu chetu kikajaa,
Usitupe viongozi, wasojua kutafuta!

Wafuliao kuchuma, hawafai uongozi,
Mengi sana watasema, ila hawawezi kazi,
Nje hawa kuwatoma, tupate wenye ujuzi,
Usitupe viongozi, wasioweza kuchuma!

Migodi wanaouza, badala ya sisi kuchimba,
Sawa na bure kuuza, hao lazima kuchamba,
Nchi tukaigeuza, kwa nje tukawasomba,
Usitupe viongozi, vito bure wauzao!

Nchi wanaoikwaza, kwa kila kitu kuwa upya,
Mipango kuichakaza, kabla haijatumiwa,
Kila siku kuanzia, nyuma ya tulipoishia,
Usitupe viongozi, upya mambo waanzao!

Waficha fedha Uswizi, hawa sio maswezi,
Ya kwao hatuyawezi, miili hufa kwa ganzi,
Ni mikubwa midokozi, wanazidi majambazi,
Usitupe viongozi, fedha waficha Uswizi!

Watumiao uchama, watufanzia zahama,
Nchi inaikosa kalima, demokrasia kukwama,
Sasa tunarudi nyuma, kwa kujenga uhasama,
Usitupe viongozi, watumiao uchama!

Vitisho wavipikao, hawajui kupakua,
Ni moto wauwashao, na chuki kujipandia,
Wapo roho watoao, yao kuyapigania,
Usitupe viongozi, kutawala kwa vitisho!

Dinichini wawekao, wao juu kujiona,
Hawa kama malimao, kazi wisha kikamua,
Inani haiko kwao, dunia yawahadaa,
Usitupe viongozi, dini waicheza shere!

Waongo waliokuwa,imani huiondoa,
Kukesha kuaminiwa, ovyo kusikitikiwa,
Hakuna wa kuwasikia, kila kitu hufulia,
Usitupe viongozi, waliokuwa waongo!

Waizi na haramia, mbali kutuepushia,
Nchi najisi watia, tohara haitakuwa,
Huyazusha mabalaa, nchi yote kuenea,
Usitupe viongozi, waliokuwa waizi!

Waipendao zinaa, ni haramu kutwachia,
Nchi laana yakaa, malaika kukimbia,
Mioto twajiwashia, ya kushoto na kulia,
Usitupe viongozi, ambao ni wazinifu!

Nchi wanayoiuza, twaomba kuangamiza,
Dakika kutowatunza, mabaya wakafanyiza,
Ya kwao ukayakwaza, Tanzania kutopoteza,
Usitupe viongozi, taifa wanaouza!

Kisasi waliojaa, Muntakimu umbua,
Wewe ndiwe muamua, wengine wanajitia,
Kisasi unakijua, wao kuwageukia,
Usitupe viongozi, waliojaa kisasi!

Dikteta ni balaa, ya Amini twayajua,
Joka tunamtambua, ndani kwake kumvaa,
Kisha tukamuondoa, na nje kumtupilia,
Usitupe viongozi, ambao ni dikteta!

Wataniao raia, kwa katiba kuwaibia,
Kisha wao kujitia, ndio juu walokuwa,
Hukumu ukiitoa, twajua yakutarajia,
Usitupe viongozi, katiba wapinduao!

Muamuzi kiamua, hakuna cha kubakia,
Na watu huwajalia, wakautoa udhia,
Hata kwa zao hadaa, bado tu wakafulia,
Usitupe viongozi, waliojaa hadaa!

Ambao kama bidhaa, dukani kununuliwa,
Yakini hao nazaa, isiwe tukajaliwa,
Mbali kutuepushia, na waliopo ondoa,
Usitupe viongozi, bidhaa waliokuwa!

Wote wanaoteuliwa, ni wenyewe wajifaa,
Na bwana kutumikia, wala si raia kufaa,
Uchungu hawajajua, mwana hawajamzaa,
Usitupe viongozi, ambao huteuliwa

Manyang'ayu karaha, kama Kenya ilivyokuwa,
Sasa kwetu waingia, vipi twawavumilia?
Mbepari mjamaa, kiongozi Tanzania?
Usitupe viongozi, ambao ni manyang'au!

Ubepari waingia, wazaini ujamaa,
Mizizi wajichimbia, juu waliokuwa,
Ardhi kujiuzia, cha mbele wakapatiwa,
Usitupe viongozi, waenzio ubepari!

Ubora wanaojitia, yao kuonea haya,
Imani kuwapotea, utumwa wakajitia,
Hawa si wa kutufaa, ni watu wa kutumiwa,
Usitupe viongozi, wanaojiona ni bora!

Pesa wanaotumia, watu kujinunulia,
Kisha wakachaguliwa, kwa hila kuitumia,
Ni dhuluma na nazaa, kutokuivumilia,
Usitupe viongozi, watu wanaonunua!

Wajanja wanaojitia, kumbe wajinga wajua,
Kamba ni kuwaachia, wenyewe kujinyongea,
Hauwezi kushangaa, maana yao wajua,
Usitupe viongozi, wajifnayao wajanja!

Wasiopenda kusoma, na daima maamuma,
Maamuzi kujitoma, bila  kujua kalima,
Hawa meli yao kuzama, ni kitu kilo adhama,
Usitupe viongozi, wasiopenda kusoma!

Wenye chuki na husuda, huroga kuneemeka,
Ni la kwao kwa kaida, hawawezi chukulika,
Hata wakiwa makada, hai bora kuwazika,
Usitupe viongozi, wenye chuki na husuda!

Uungu wanaotaka, na riziki kuitoa,
Wamalize kwa hakika, kama hawatakujua,
Jambo lako la hakika, na wahaka haijawa,
Usitupe viongozi, miungu wajifanyao!

Majibari na jeuri, njia yao waijua,
Firauni ni amiri, aliyekukutezea,
Ukamtia kabari, na yake kupotezea,
Usitupe viongozi, jeuri waliojaa!

Dharau waliojaa, na kiburi kujitia,
Yao yapate sinyaa, na maradhi kutwaa,
Heri kutoifungua, na shari kuwagawia,
Usitupe viongozi, dharau waliojaa!

Wenye njaa Tanznia, viongozi walokuwa,
Ni maradhi waugua, hebu kuwapatilizia,
Mbali waende ishilia, nchi  hawawezi kuifaa,
Usitupe viongozi, wenye njaa isoisha!

Utajiri waabuduo, kuwaacha ni radhia,
Mitaji tutafutayo, mashaka sije kutiwa,
Uhai tukiwa nao, hata nasi hujichumia,
Usitupe viongozi, waabuduo utajiri!
Usitupe viongozi, wasiosema ukweli!

Kutunza wasiojua, hawafai Tanzania,
Ubadhirifu wajaa, uchungu hawajatiwa,
Vya kwetu wavitumia, na akiba waing'oa,
Usitupe viongozi, iktisadi wasojua!

Kukopa wamezoea, deni watuongezea,
Tunalibeba jamaa, vijukuu kuachia,
Si haki inavyokuwa, wengine twawaonea,
Usitupe viongozi, waishio kwa kukopa!

Kodi wanaotafuna, hawafai Tanzania,
Yafaa nao kwachana, haki tukajitendea,
Huu si wetu muamana, tunaibeba balaa,
Usitupe viongozi, kodi wanaoitafuna!

Elimu wasioenzi, nyuma wanaturudisha,
Sio wetu wanagenzi, wanaizaya nasema,
Linatakiwa zowezi, pembeni kuwasukuma,
Usitupe viongozi, elimu wasioenzi!

Michezo wasiojali, ila maneno kuzidi,
Hao si marijali, kadari waikaidi,
Hawataki afadhali, vijana homa kuzidi,
Usitupe viongozi, michezo wasiojali!

Afya wanaokwaza, watu kuzidi ugua,
Si watu wa kuweza, ni lazima kuondoa,
Tasnia waitatiza, ukubwa kung'ang'ania,
Usitupe viongozi, afya wasiojali!

Wala wao wakashiba, sisi makombo watwachia,
Chajaa chao kibaba, chetu chazidi pungua,
Na ni wao mrahaba, sisi twazidi ugua,
Usitupe viongozi, wala, tukala makombo!

Keki wakiipakua, kubwa wanajigawia,
Sababu wakizitoa, vigumu kutuingia,
Uongozi kujifaa, wala sio kutufaa!
Usitupe viongozi, kubwa wala,chache yetu!

Masikini waumia, hali kwao sasa mbaya,
Mikakati watumia, wenye nacho kuwafaa,
Fakiri aliyekuwa, azidi kupotezewa,
Usitupe viongozi, wasiofaa maskini!

Wanakula ya fakiri, wao wanaochagua,
Mnyonge kweli kafiri, nani wa kumfaa,
Maisha yake ni shari, na majuto kujutia,
Usitupe viongozi, walao vya mafakiri!

Wengine tukichagua, aibu wajionea,
Imani yao kufaa, ubaya wakaamua,
Mbegu bora kichipua, wao wanazichimbua,
Usitupe viongozi, imani wanaokejeli!

Mapagani wanakuwa, hofu hawana moyoni,
Shetani kawachagua, yake yawe ni ubani,
Na wao wameamua, wadhani wa salamani,
Usitupe viongozi, ambao ni mapagani!

Walimu wanaokwaza, dira wanaipoteza,
Maumivu twayakuza, na nchi twailemaza,
Kitu gani tutaweza, labda iwe miujiza,
Usitupe viongozi, wanaokwaza walimu!

Wadharau daktari, wao bora kujiona,
Hili hawajalihariri, ni kosa tena kubwa sana,
Haujengi ufahari, mengi tutapotezana,
Usitupe viongozi, daktari wasothamini!

Na wenye njaa ya sifa, watengezee kashfa,
Uwe wa bure wadhifa, kila pembe una nyufa,
Na kukosa maarifa, iwe ni yao masafa,
Usitupe viongozi, wapendao kusifiwa!

Watakao abudiwa, shiriki wanaizua,
Nawe dawa waijua, dozi ungewapatia,
Ndiwe mwenye kuamua,tuepushie Tanzania,
Usitupe viongozi, watakao abudiwa!

Imani ninailea, nawapatia usia,
Mko huru kuamua, kupu'za au kusikia,
Mola namshuhudia, mmoja aliyekuwa,
Usitupe viongozi, watenga dini na siasa!

Magharibi yatuvaa, na upofu kututia,
Yao kufuatilia, yetu tukayaachia,
Utamani Afrika, ni imani kutangulia,
Usitupe viongozi, watenga dini na siasa!

Wenye heri huamua, imani kuichangia,
Wala si kuitumia, mwenyewe kujifagilia,
Na kisha uakdhania, salama utabakia,
Usitupe viongozi, watenga dini na siasa!


Uranium wachezeao, mabahau kutufanza,
Ili wachume wao, mbali wanaojitunza,
Hakika kina mfamao, hawafai  maliwaza,
Usitupe viongozi, uranium wachezeao!

Sensa wanaochezea, na takwimu kuzipika,
Hila wanayoitia, na uongo kuzagaa,
Na vitisho kuvitia, Muomba akaona haya!
Usitupe viongozi, sensa wanaochezea!


Tunu kuombea uwazi, uwajibikaji, haki za binadamu,
usawa, demokrasia na utawala na menejimenti bora Tanzania na Afrika!
-Mwandishi.








USITUPE VIONGOZI


USITUPE VIONGOZI ....


KAMA wapo waondoe, safu zikasafishika,
Kisha usitujalie, mamlakani kuwaweka,
Nasi utuhurumie, tusiwe wa kuteseka,
Usitupe viongozi, waliokuwa fisadi!

Marafiki na mashoga, jamaa hao dhihaka,
Kaumu Lutu kubwaga, yakini kusalimika,
Wageuze ni maboga, na tembo kukanyagika,
Usitupe viongozi, marafiki na mashoga!

Wazungu waabuduo, na Usa-haa nao pia,
Tuwe tuwatapikao, yakwao tukayazoa,
Wawe wabakiao, ni rafiki wa kukaa,
Usitupe viongozi, waabuduo Wazungu!

Vijiji vinaugua, nani kuviangalia,
Hata maji wachimbua, badala ya kufungulia,
Huu mkubwa ukiwa, viongozi kama hawa,
Usitupe viongozi, vijiji wasiojali!

Wenyewe wajipendelea, wao na zao jamaa,
Wazee wawatezea, uzeeni kuumia,
Ahadi wakazitoa, hamsini zisokuwa,
Usitupe viongozi, wazee wasiotunza!

Huwatumia vijana, kufata yao mapenzi,
Ila kutenda ya maana, kwalo hawana ujuzi,
Maisha duni waona, vijana kukosa kazi,
Usitupe viongozi, vijana wasiothamini!

Waliojaa hadaa, kuwazaini raia,
Mola kutotujalia, na kama wapo ondoa,
Hii ni ya umma dua, Muumba wetu sikia,
Usitupe viongozi, wadanganyao wananchi!

Wala rushwa ni balaa, hasa chama kupitia,
Hawaoni ni udhia, nchi watajiuzia,
Watumwa raia kuwa, upya wakatawaliwa,
Usitupe viongozi, ambao ni wala rushwa!

Tuepushe na balaa, kwa kuwadi kujaliwa,
Na wezi wenye ubia, vya nchi wakachomoa,
Ni vibaka walokuwa, ukubwa wautumia,
Usitupe viongozi, wanaokula na wezi!

Ubabe wanaotumia, huja kuzusha ghasia,
Hasira ikipasua, hakuna wa kutuokoa,
Kila mtu kukimbia, kwenye moto tukatua,
Usitupe viongozi, ubabe wanaojitia!

Saini wanazitia, wakubwa waliokuwa,
Fedha wakazidokoa, benkini zilizokaa,
Na dhahabu kuitwaa, binafsi ikawafaa,
Usitupe viongozi, benki kuu waibao!

Kuna walevi wajaa, irabu ni kutumia,
Shilingi wakiijua, huko watachokonoa,
Na akiba kuitoa, ikaenda kupotea,
Usitupe viongozi, walevi wa kutumia!

Wasiokuwa na haya, nao sasa wamejaa,
Aibu imeshawagwaya, na soni yawakimbia,
Waweza kujifanyia, hata usofikiria,
Usitupe viongozi, hayawani walokuwa!

Raia wanaoibia, uwaangaze Jalia,
Katu kutokuwaachia, ovyo wakatutendea,
Ufakiri kututia, na nusura kutojua,
Usitupe viongozi, raia wanaoua!

Dhuluma tunazijua, hai walotufanzia,
Na marehemu kadhia, hata nao waijua,
Hawa kiwaangazia, utaijua hidaya,
Usitupe viongozi, dhuluma waliojaa!

Wanaabudu dunia, vichaa waliokuwa,
Wao wakajidhania, milele wataikaa,
Na kufa kutoridhia, wengine wakawaua,
Usitupe viongozi, waabuduo dunia!

Ving'ang'anizi balaa, hawafai Tanzania,
Nafasi waliotwaa, watake tena rudia,
Hao ni kuwafagia, pembeni wakazolewa,
Usitupe viongozi, ving'ang'anizi wakubwa!

Mabomu wanaotumia, kupiga ovyo raia,
Na dola kuitumia, vibaya isivyokuwa,
Mkoloni bora kuwa, hao ni wa kuwaondoa,
Usitupe viongozi, raia waumizao!

Akili waliofubaa, kuzua wasiojua,
Mirija wakaachia, vya kwetu ikajinywea,
Sisi kutojipatia, chungu chetu kikajaa,
Usitupe viongozi, wasojua kutafuta!

Wafuliao kuchuma, hawafai uongozi,
Mengi sana watasema, ila hawawezi kazi,
Nje hawa kuwatoma, tupate wenye ujuzi,
Usitupe viongozi, wasioweza kuchuma!

Migodi wanaouza, badala ya sisi kuchimba,
Sawa na bure kuuza, hao lazima kuchamba,
Nchi tukaigeuza, kwa nje tukawasomba,
Usitupe viongozi, vito bure wauzao!

Nchi wanaoikwaza, kwa kila kitu kuwa upya,
Mipango kuichakaza, kabla haijatumiwa,
Kila siku kuanzia, nyuma ya tulipoishia,
Usitupe viongozi, upya mambo waanzao!

Waficha fedha Uswizi, hawa sio maswezi,
Ya kwao hatuyawezi, miili hufa kwa ganzi,
Ni mikubwa midokozi, wanazidi majambazi,
Usitupe viongozi, fedha waficha Uswizi!

Watumiao uchama, watufanzia zahama,
Nchi inaikosa kalima, demokrasia kukwama,
Sasa tunarudi nyuma, kwa kujenga uhasama,
Usitupe viongozi, watumiao uchama!

Vitisho wavipikao, hawajui kupakua,
Ni moto wauwashao, na chuki kujipandia,
Wapo roho watoao, yao kuyapigania,
Usitupe viongozi, kutawala kwa vitisho!

Dinichini wawekao, wao juu kujiona,
Hawa kama malimao, kazi wisha kikamua,
Inani haiko kwao, dunia yawahadaa,
Usitupe viongozi, dini waicheza shere!

Waongo waliokuwa,imani huiondoa,
Kukesha kuaminiwa, ovyo kusikitikiwa,
Hakuna wa kuwasikia, kila kitu hufulia,
Usitupe viongozi, waliokuwa waongo!

Waizi na haramia, mbali kutuepushia,
Nchi najisi watia, tohara haitakuwa,
Huyazusha mabalaa, nchi yote kuenea,
Usitupe viongozi, waliokuwa waizi!

Waipendao zinaa, ni haramu kutwachia,
Nchi laana yakaa, malaika kukimbia,
Mioto twajiwashia, ya kushoto na kulia,
Usitupe viongozi, ambao ni wazinifu!

Nchi wanayoiuza, twaomba kuangamiza,
Dakika kutowatunza, mabaya wakafanyiza,
Ya kwao ukayakwaza, Tanzania kutopoteza,
Usitupe viongozi, taifa wanaouza!

Kisasi waliojaa, Muntakimu umbua,
Wewe ndiwe muamua, wengine wanajitia,
Kisasi unakijua, wao kuwageukia,
Usitupe viongozi, waliojaa kisasi!

Dikteta ni balaa, ya Amini twayajua,
Joka tunamtambua, ndani kwake kumvaa,
Kisha tukamuondoa, na nje kumtupilia,
Usitupe viongozi, ambao ni dikteta!

Wataniao raia, kwa katiba kuwaibia,
Kisha wao kujitia, ndio juu walokuwa,
Hukumu ukiitoa, twajua yakutarajia,
Usitupe viongozi, katiba wapinduao!

Muamuzi kiamua, hakuna cha kubakia,
Na watu huwajalia, wakautoa udhia,
Hata kwa zao hadaa, bado tu wakafulia,
Usitupe viongozi, waliojaa hadaa!

Ambao kama bidhaa, dukani kununuliwa,
Yakini hao nazaa, isiwe tukajaliwa,
Mbali kutuepushia, na waliopo ondoa,
Usitupe viongozi, bidhaa waliokuwa!

Wote wanaoteuliwa, ni wenyewe wajifaa,
Na bwana kutumikia, wala si raia kufaa,
Uchungu hawajajua, mwana hawajamzaa,
Usitupe viongozi, ambao huteuliwa

Manyang'ayu karaha, kama Kenya ilivyokuwa,
Sasa kwetu waingia, vipi twawavumilia?
Mbepari mjamaa, kiongozi Tanzania?
Usitupe viongozi, ambao ni manyang'au!

Ubepari waingia, wazaini ujamaa,
Mizizi wajichimbia, juu waliokuwa,
Ardhi kujiuzia, cha mbele wakapatiwa,
Usitupe viongozi, waenzio ubepari!

Ubora wanaojitia, yao kuonea haya,
Imani kuwapotea, utumwa wakajitia,
Hawa si wa kutufaa, ni watu wa kutumiwa,
Usitupe viongozi, wanaojiona ni bora!

Pesa wanaotumia, watu kujinunulia,
Kisha wakachaguliwa, kwa hila kuitumia,
Ni dhuluma na nazaa, kutokuivumilia,
Usitupe viongozi, watu wanaonunua!

Wajanja wanaojitia, kumbe wajinga wajua,
Kamba ni kuwaachia, wenyewe kujinyongea,
Hauwezi kushangaa, maana yao wajua,
Usitupe viongozi, wajifnayao wajanja!

Wasiopenda kusoma, na daima maamuma,
Maamuzi kujitoma, bila  kujua kalima,
Hawa meli yao kuzama, ni kitu kilo adhama,
Usitupe viongozi, wasiopenda kusoma!

Wenye chuki na husuda, huroga kuneemeka,
Ni la kwao kwa kaida, hawawezi chukulika,
Hata wakiwa makada, hai bora kuwazika,
Usitupe viongozi, wenye chuki na husuda!

Uungu wanaotaka, na riziki kuitoa,
Wamalize kwa hakika, kama hawatakujua,
Jambo lako la hakika, na wahaka haijawa,
Usitupe viongozi, miungu wajifanyao!

Majibari na jeuri, njia yao waijua,
Firauni ni amiri, aliyekukutezea,
Ukamtia kabari, na yake kupotezea,
Usitupe viongozi, jeuri waliojaa!

Dharau waliojaa, na kiburi kujitia,
Yao yapate sinyaa, na maradhi kutwaa,
Heri kutoifungua, na shari kuwagawia,
Usitupe viongozi, dharau waliojaa!

Wenye njaa Tanznia, viongozi walokuwa,
Ni maradhi waugua, hebu kuwapatilizia,
Mbali waende ishilia, nchi  hawawezi kuifaa,
Usitupe viongozi, wenye njaa isoisha!

Utajiri waabuduo, kuwaacha ni radhia,
Mitaji tutafutayo, mashaka sije kutiwa,
Uhai tukiwa nao, hata nasi hujichumia,
Usitupe viongozi, waabuduo utajiri!
Usitupe viongozi, wasiosema ukweli!

Kutunza wasiojua, hawafai Tanzania,
Ubadhirifu wajaa, uchungu hawajatiwa,
Vya kwetu wavitumia, na akiba waing'oa,
Usitupe viongozi, iktisadi wasojua!

Kukopa wamezoea, deni watuongezea,
Tunalibeba jamaa, vijukuu kuachia,
Si haki inavyokuwa, wengine twawaonea,
Usitupe viongozi, waishio kwa kukopa!

Kodi wanaotafuna, hawafai Tanzania,
Yafaa nao kwachana, haki tukajitendea,
Huu si wetu muamana, tunaibeba balaa,
Usitupe viongozi, kodi wanaoitafuna!

Elimu wasioenzi, nyuma wanaturudisha,
Sio wetu wanagenzi, wanaizaya nasema,
Linatakiwa zowezi, pembeni kuwasukuma,
Usitupe viongozi, elimu wasioenzi!

Michezo wasiojali, ila maneno kuzidi,
Hao si marijali, kadari waikaidi,
Hawataki afadhali, vijana homa kuzidi,
Usitupe viongozi, michezo wasiojali!

Afya wanaokwaza, watu kuzidi ugua,
Si watu wa kuweza, ni lazima kuondoa,
Tasnia waitatiza, ukubwa kung'ang'ania,
Usitupe viongozi, afya wasiojali!

Wala wao wakashiba, sisi makombo watwachia,
Chajaa chao kibaba, chetu chazidi pungua,
Na ni wao mrahaba, sisi twazidi ugua,
Usitupe viongozi, wala, tukala makombo!

Keki wakiipakua, kubwa wanajigawia,
Sababu wakizitoa, vigumu kutuingia,
Uongozi kujifaa, wala sio kutufaa!
Usitupe viongozi, kubwa wala,chache yetu!

Masikini waumia, hali kwao sasa mbaya,
Mikakati watumia, wenye nacho kuwafaa,
Fakiri aliyekuwa, azidi kupotezewa,
Usitupe viongozi, wasiofaa maskini!

Wanakula ya fakiri, wao wanaochagua,
Mnyonge kweli kafiri, nani wa kumfaa,
Maisha yake ni shari, na majuto kujutia,
Usitupe viongozi, walao vya mafakiri!

Wengine tukichagua, aibu wajionea,
Imani yao kufaa, ubaya wakaamua,
Mbegu bora kichipua, wao wanazichimbua,
Usitupe viongozi, imani wanaokejeli!

Mapagani wanakuwa, hofu hawana moyoni,
Shetani kawachagua, yake yawe ni ubani,
Na wao wameamua, wadhani wa salamani,
Usitupe viongozi, ambao ni mapagani!

Walimu wanaokwaza, dira wanaipoteza,
Maumivu twayakuza, na nchi twailemaza,
Kitu gani tutaweza, labda iwe miujiza,
Usitupe viongozi, wanaokwaza walimu!

Wadharau daktari, wao bora kujiona,
Hili hawajalihariri, ni kosa tena kubwa sana,
Haujengi ufahari, mengi tutapotezana,
Usitupe viongozi, daktari wasothamini!

Na wenye njaa ya sifa, watengezee kashfa,
Uwe wa bure wadhifa, kila pembe una nyufa,
Na kukosa maarifa, iwe ni yao masafa,
Usitupe viongozi, wapendao kusifiwa!

Watakao abudiwa, shiriki wanaizua,
Nawe dawa waijua, dozi ungewapatia,
Ndiwe mwenye kuamua,tuepushie Tanzania,
Usitupe viongozi, watakao abudiwa!

Imani ninailea, nawapatia usia,
Mko huru kuamua, kupu'za au kusikia,
Mola namshuhudia, mmoja aliyekuwa,
Usitupe viongozi, watenga dini na siasa!

Magharibi yatuvaa, na upofu kututia,
Yao kufuatilia, yetu tukayaachia,
Utamani Afrika, ni imani kutangulia,
Usitupe viongozi, watenga dini na siasa!

Wenye heri huamua, imani kuichangia,
Wala si kuitumia, mwenyewe kujifagilia,
Na kisha uakdhania, salama utabakia,
Usitupe viongozi, watenga dini na siasa!


Uranium wachezeao, mabahau kutufanza,
Ili wachume wao, mbali wanaojitunza,
Hakika kina mfamao, hawafai  maliwaza,
Usitupe viongozi, uranium wachezeao!

Sensa wanaochezea, na takwimu kuzipika,
Hila wanayoitia, na uongo kuzagaa,
Na vitisho kuvitia, Muomba akaona haya!
Usitupe viongozi, sensa wanaochezea!


Tunu kuombea uwazi, uwajibikaji, haki za binadamu,
usawa, demokrasia na utawala na menejimenti bora Tanzania na Afrika!
-Mwandishi.








Monday, August 20, 2012

Vichanga haviyawezi

Vichanga haviyawezi

Vichanga vipe makuzi, uji na kisha ubwabwa,
Miezi inavyoenzi, vikaupata ukubwa,
Huvifanyia rawazi, kuja kushika makubwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Katika za kwetu enzi, vidogo vyapewa ukubwa,
Vilozea mchuuzi, na ugali vikakabwa,
Vikaachia machozi, kwa maneno wakagombwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Wanatumia hirizi, kuupata ukubwa,
Na njia bado ziwazi, msamba huja kuzombwa,
Kwenye videvu mchuzi, vindevu vikenda lambwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Ukubwa kama ujuzi, kiumbwe hilo kaumbwa,
Asiyekuwa mlezi, kawaidaye kukunbwa,
Mambo akayadarizi, kwa tambo zisizotambwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Huyafanza mazoezi, wachawi wasije bambwa,
Wakaruka kwa mizizi, na matawi kujigamba,
Kiazi hakiwi ndizi, hukikataa mgomba,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Vichanga haviyawezi, ya sasa ya kupambwa,
Uongo pia uwizi, ni nakshi za kurembwa,
Wazee wana ajizi, kwa njaa yao wafumbwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Yote yao maamuzi, na mtu mkono hulambwa,
Wakapewa upuuzi, kwa machimbo wakachimbwa,
Wakabakia doezi, vya watu kuja kuchambwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.


Namdiriki mjuzi, bwana aliye mkubwa,
Mmiliki mwenye enzi, na sultani mkubwa,
Anipatie malezi, na dunia kutorembwa,
Vichanga haviyawezi, mambo haya ya wakubwa.



Dini mkizibagua





Mamlaka mkipewa, haki budi kutambua,
Kisha kutokuegemea, upande mmoja mkawa,
Taifa litaugua, na msibani kwingia,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Nchi haina ubaya, viumbe ndio wabaya,
Hasa wanaotumiwa, na watu kununuliwa,
Ovyo wakajifanzia, na kinyesi kujitia,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Haki wakainunua, na mengine kuchukua,
Ukubwa wakajitia, na utakatifu pia,
Kumbe uoza wakawa, na nchi kuisumbua,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Shilingi huitumia, heshima kujipatia,
Na vyeo wakavipewa, kisomowasichojua,
Na kazi wasizozijua, kila siku kupangiwa,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Vipofu kazi hupewa, macho za kutarajia,
Na viziwi nao pia, kazi za kusikizia,
Kicheko kuanguliwa, ikitazama dunia,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Mola mwenye kutambua, dini ameziachia,
Madhehebu kujigawa, na yao kujifanzia,
Ukweli yaliokuwa, na waongo nao pia,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Ya kwako ni kujifanyia, wengine kutoingilia,
Vingine inavyokuwa, ubaya mwauchimbua,
Viongozi wa ridhaa, hili watalikataa,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.

Juu mnapokalia, ya chini kuangalia,
Kwa haki pia usawa, msije kuchakachua,
Na nchi ikaugua, na watu kuja umia,
Dini mkizibagua, huvuna matunda haya.


Tupo kama tusiopo




Tupo tusiokuwepo, nje wametutolea,
Hatukujua kiapo, wala hukumu kuambiwa,
Si mtaji ni mkopo, eti sisi twaambiwa,
Tupo kama tusiopo, hili budi likakoma.

Wakiliunda jopo, sisi ndio tusiopo,
Na kamati za mapopo, nako hatutakuwepo,
Halmashauri za kopo, nazo humo si waliopo,
Tupo kama tusiopo, hili budi likakoma.

Ni tupo kama hatupo, wao wapo kama wapo,
Na dijito zilizopo, ndipo wao wapewapo,
Islamu lake lipo, nalo ni la kutokuwepo,
Tupo kama tusiopo, hili budi likakoma.

Tukiyatupa makopo, tutakuwa hatuwepo,
Ila kelele za jopo, sikio ziingiapo,
Ndipo wao wajuapo, tupo kama vile tupo,
Tupo kama tusiopo, hili budi likakoma.


Wizara hii kiraka





Nafasi hii mashaka, tena mkubwa wahaka,
Kitu kisichobebeka, ibidi kulazimika,
Kwa nguvu kuchukulika, ma watu kuathirika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Umbeya inaushika, na tuhuma za kuzuka,
Vyomo inavyoshika, dhuluma inafanzika,
Boriti imewatoka, machoni inamulika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Hawaoni kwa hakika, boriti ilipokalika,
Ila tukitazamika, ya kwetu waimulika,
Wakayazusha mahoka, na riziki kufungika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Tunamuomba rabuka, ya kwao kuangazika,
Hata wakishughulika, matumbo yakatumbuka,
Na uzushi kuwazika, mihadi ikijafika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Macho tunayeleka, mbinguni yapepesuka,
Kumuomba mstahika, ya kwetu kutoponzeka,
Na yao yakadhurika, nyumbani na walikoshika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Walii nayatamka, makubwa yatawafika,
Tawba wasipotaka, nao wakarehemeka,
Wajue walikotoka, na tunakokwenda si hakika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Ila wakierevuka, iwe kwao ni mashaka,
Waishi kwenye wahaka, na mipango kufumuka,
Waja wakijanjaruka, dua zitakubalika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Tumevichoka viraka, matakoni kufurika,
Hakuna la kuongezeka, ila ni kupaparika,
Na wakubwa kuwasuka, nywele wasiosukika,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.

Yangu yanakamilika, fursa nimetosheka,
Wasia nimeshika, kumpa anayetaka,
Na wote wasiotaka, naziondoa baraka,
Wizara hii kiraka, wabebwaji wabebeka.



Hivi sio ugaidi ?





Mjinga ninauliza, fisadi si ugaidi,
Kweli mkinieleza, utapungua mdadi,
Uchawi nikaapuuza, kwenda kuutaradadi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Mali yetu twapoteza, Waswizi wazifaidi,
Nini kinachotujuza, kuwa hawa si gaidi?
Hamuwezi nieleza, vingine nitakaidi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Wanaizaya wazoza, shetani kutaradadi,
Kila kitu wamaliza, wengine kuwa kuwadi,
Kina babu na ajuza, watakuja zifaidi?
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Maisha yanateleza, kwetu sisi ni magadi,
Wanatuona uoza, kwa nchi kutofaidi,
Ya kwao wakayakuza, kwa mtaji na miradi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Ni Mola wetu muweza, Muntaqimu kaahidi,
Zawadi atawatunza, kikomo bila idadi,
Ya kwao akayabeza, na wana wasifaidi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Zetu wanazipoteza, wakadai za gaidi,
Wakawa wajipooza, na kula pasi idadi,
Muumba atawazoza, wajitungie nakidi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Juhudi wakihimiza, wao wapandda mdadi,
Siku wanazisogeza, kwenda kula yao iddi,
Azizi ndiye muweza, kaida atakaidi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Tungali twawatazama, ja Huudi na Thamudi,
Sku zao za kuzama, ikifikia mihadi,
Hakuna la kulalama, wala amri kutohidi,
Fedha zetu za Uswizi, hivi sio ugaigi?

Fakiri aweza jenga



DINI hii ya neema, Mola kaisabilia,
Ukitakia nakama, mwenyewe ukaumia,
Hata zichache tuhuma, kichaa ukaugua,
Fakiri aweza jenga, rais akafulia.

Imani hii heshima, kiumbe ukijaliwa,
Inaamrisha mema, na maovu kukataa,
Na walio na hekima, hawaachi kwitikia,
Fakiri aweza jenga, kafiri akabomoa.

Dini hii ya rehema, usafi yazingatia,
Wafwatao waadhama, haki huipigania,
Inakataa dhuluma, na watu kuwaonea,
Fakiri aweza jenga, tajiri akaagua.

Dini hii ya salama, amani imejaliwa,
Ila shetani kakwama, uzushi anauzua,
Ugaidi wanalalama, Islamu tumekua,
Fakiri aweza jenga, japo katu hana kitu.

Historia kitazama, wao wamechokonoa,
Kwingine kwenda kuzama, kwao kusikokuwa,
Mafuta wakishakwama, ugaidi wanazua,
Fakiri aweza jenga, rais akafulia.

Na nyinginezo tuhuma, Islamu wasingizia,
Viongozi maamuma, uongo wakauvaa,
Wakaikosa heshima, na utu wao kuvia,
Fakiri aweza jenga, kafiri akabomoa.

Ewe mwingi wa rehema, mtambulifu Halimaa,
Kwako twaegemea, huruma na yako afua,
Kuiipitisha karama, yao ukayatengua,
Fakiri aweza jenga, tajiri akaagua.

Zimetuchosha dhuluma, haki tunaililia,
Ngao zako twaazima, ya kwao kuwarudia,
Sisi tubaki wazima, na wao wakaugua,
Fakiri aweza jenga, japo katu hana kitu.


Mkoa hawawakilishi



Hao watu wa kupewa, zawadi wanachukua,
Haki kukutendea, naona haitakuwa,
Humwabudu mteua, kama Mungu kumwofia,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Udugu wanatumia, na uchama kuitia,
Bendera ikipepea, wao inawapepea,
Si huru tulokuwa, katika yetu mikoa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Kampenzi zanunua, kapuni zikawatia,
Sababu nchi kuvia, ni wakuu wa mikoa,
Ya watu kutoyajua, chama kukifikiria,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Wengine wanatumiwa, watu yao kuibiwa,
Madini yaliyojaa, na haki za kidunia,
Kisha wawashindilia, na risasi kutumia,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Viwanja huvichukua, wenyewe kujigawia,
Na mashamba nayo pia, kupona haitakuwa,
Yote wanayamavia, ubepari kuchipua,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Ndani wanawatumia, na nje kuwauzia,
Haki kwao sio nia, ila nia kujilia,
Hawatetei raia, mkubwa wamtetea,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Watu wawashambulia, upinzani kama wawa,
Kwao demokrasia, ni ufalme kuridhia,
Wameila hadaa, kutapika wakataa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Si wema walokuwa, Mtwara ukiangalia,
Dini zinawatumia, wakijidai watawa,
Mambo wawafanyia, ndugu zaburi yajua,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Imani wakihofia, watu watawaonea,
Yao wakayakataa, na uzushi kuwazushia,
Mola haachi chukia, akawaona udhia,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Bure tu hujifutua, kwa dola kuitumia,
Dua tukiwaombea, ulemavu wauvaa,
Waumini mwatakiwa, mamb haaya kuyajua,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Dini ikijitambua, mbali nao itakaa,
Serikali hufatia, Mungu anatangulia,
Jihadi tunajua, ni amri tumepewa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Kiumbe ukijifia, dini yao kutetea,
Peponi utaingia, mambo mema kuridhiwa,
Mola kumsabilia, ni chaguo lake huwa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Ubwana wanajitia, na utwana kututia,
Tunu inayowafaa, madarakani kung'oa,
Wengine tukachagua, viongozi wetu kuwa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Huwachukia Kafidi




Viumbe waliokuwa, ukubwa wakijitia,
Ya Mola kuyaumbua, na yao kushindilia,
Katu hatowaridhia, jahanama watapewa,
Huwachukia Kafidi, dini wanaotezea!

Njia pana huachia, watumia wasojua,
Yake kumuharibia, na yao yakatengenea,
Tena yasiyomfaa, na uzushi yalokuwa,
Huwachukia Kafidi, dini wanaoonea!

Huwa anawachezea, paka, panya kumfanzia,
Huru akamuachia, mbali kupiga hatua,
Kisha akamnyakua, mdomoni kumtia,
Huwachukia Kafidi, dini wanaotezea!

Wakwaza kujitambua, ukweli kutojisomea,
Waambiayo kusikia, kisha wakayaabudia,
Ukweli wangeujua, upya wangelizaliwa,
Huwachukia Kafidi, dini wanaoonea!

Waabudu kusinzia, na hadithi kusikia,
Akili wazihofia, hawawezi kutumia,
Dhambi wakajimegea, na mchuzi kujilia,
Huwachukia Kafidi, dini wanaotezea!

Na mchuzi kujilia, uliojaa hadaa,
Wahidi kumchengua, kwa ushirikina ubia,
Wao wakajidhania, kila sawa kimekua,
Huwachukia Kafidi, dini wanaoonea!

Zamani kawaambia, ishara kuzitambua,
Uongozi kutokwaa, akii zinapovia,
Bali zinapotanzua, ukweli zikalilia,
Huwachukia Kafidi, dini wanaotezea!

Waishio kwa kusikia, neno wameshapotea,
Hekaya wazichukua, mashiko yasiyokuwa,
Uongo zilizotiwa, na uhalali kuuawa,
Huwachukia Kafidi, dini wanaoonea!

Kwako nakukimbilia, mtenzi wa kutanzua,
Haki kuniangazia, na wengine kuokoa,
Firdausi kwingia, matunda tukajilia,
Huwachukia Kafidi, dini wanaotezea!

Neno nimeshawaambia, ila hamtoyasikia,
Kubaya mtaemea, hadi roho kutolewa,
Watakaojionea, ukweli watatambua,
Huwachukia Kafidi, dini wanaoonea!

Siwezi kujizuia



VYOTE ninavyotamani, umejaliwa mwandani,
Tabia ninayothamini, na uzuri wa usoni,
Mwili ulio sakini, na ngozi ilo laini,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Ni ndoto yangu amini, nikiiota zamani,
Ruia zenye hisani, nikiwaza urulaini,
Kiasi mwangu moyoni, nikajiona jangwani,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Msafiri duniani, vijijini na mjini,
Wengi natia machoni, ila hawawi moyoni,
Hadi nilipobaini, utokako mafichoni,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Sijalisema kinywani, na kuachia saini,
Cheche zikiwa rohoni, utauliza amini,
Kisha ukaja nyumbani, na wala si mitaani,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Nilishachoka moyoni, viumbe sikutamani,
Moto waisha njiani, japo pepo zi makini,
Kisichopo moyoni, sio ashiki mwilini,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Nimelipenda jasmini, ua lisilo nuksani,
Harufuye ni makini, inatembeza puani,
Ukitupa kitandani, miski utazaini,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Nalitauta yakini, lilipo kwenye bustani,
Mche wake niauni, kuja kupanda nyumbani,
Harufu yake niwini, niwapo mwengu chumbani,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Jasmini, asmini, jinalo nalitamani,
Nasibu siiamini, kukupata kilaini,
Ndio niko matesoni, akilini na moyoni,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!


Sijui kutengeneza





Mifuko nikishajaza, naipeleka Uswizi,
Siwezi kutengeneza, akili hainitunzi,
Mwepesi kulimbikiza, ila si mtengenezi,
Sijui kutengeneza, budi kuficha Uswizi.

Hulazimu kwenda tunza, palipo watengenezi,
Riba wakaipandikiza, mali nyingi nikahodhi,
Urithi nikautunza, binafsi changu kizazi,
Sijui kutengeneza, budi kuficha Uswizi.

Siwezi kuwaeleza, ya halali au wizi,
Mola kajipendekeza, mimi amenihifadhi,
Ninahofu wanawenza, mnaleta uchokozi,
Sijui kutengeneza, budi kuficha Uswizi.

Nyie nini mngefanza, bahati mngeiridhi,
Mwajitia mngepuuza, fedha nje ziwe wazi,
Au hazina kuoza, kule pasipo na kazi ?
Sijui kutengeneza, budi kuficha Uswizi.

Mkichagua viazi





Mkiachagua viazi, hamuwezi kula ndizi,
Uchaguzi una kazi, tena makubwa maamuzi,
Si kitumbua na andazi, mdoni ukakitia,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Mkipokea viazi, chipsi kupata kazi,
Hii ni nchi ya wazi, si uzuzi na uvumbuzi,
Maisha yake uchizi, taslima na hirizi,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Kimetokota kizazi, cha uongo na ajizi,
Kimefulia ujuzi, wala sio chapakazi,
Yawaathiri malezi, hawana maandalizi,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Ni nchi yenye upuuzi, na kuukosa uwazi,
Akili zimebarizi, na bongo za uduwazi,
Kutamba kwa udokozi, na wengine mang'amuzi,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Sio mabli na ushenzi, na ujirani na nzi,
Vichwa vyetu kama nazi, kuunga tui la mchuzi,
Ndio mwisho maamuzi, kwingine ni mauguzi,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Yatakiwa mapinduzi, kupisha kipya kizazi,
Mapya kitakachoenzi, na kufanza maenezi,
Wakawa watangulizi, si kudorora kiizi,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Yaishe ya ulanguzi, na thamani bila kazi,
Tukageuka wajenzi, nchi ikapanda ngazi,
Tuukatae ushenzi, mbu pia na mainzi,
Mkichagua viazi, hakika mwapata viazi.

Vinara wa kupotezea





Wajua kupotezea, kwa kuwa wanahusika,
Rada tumeyang'amua, sasa wanapotezea,
Hakuna mwenye hatia, eti watu tunaambiwa,
Vinara wa kupotezea, washindwe na walaniwa!!

Fisadi weshapotezea, chembani wameingia,
Pesa waliojizolea, yote chama imetwaa,
Mfukoni kuitia, kasri kujijengea,
Vinara wa kupotezea, washindwe na walaniwa!!

Na wengine watembea, kwenye wilaya na mikoa,
uongo kusimulia, hadithi zisizokuwa,
Ujinga tumejaliwa, nasi tunawakubalia,
Vinara wa kupotezea, washindwe na walaniwa!!

Ujinga mkiachia, pabaya mtaingia,
Vipofu wameamua, shimoni kwenda watia,
Nanyi nyuma mwafatia, huku macho mwafungua,
Vinara wa kupotezea, washindwe na walaniwa!!

Kawafungueni macho


Wakaanga vijijini, kwa mafuta yao wenyewe,
Hutiwa kikaangoni, kwa vikanga na vikoe,
Na fulana za kijani, waume ziwanunue,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Wengi wangali gizani, tongotongo wazitoe,
Wahofia upinzani kutofaa wadhanaie,
Kumbe wana mumiani, ndani wamuaminiye,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Vijijini mashakani, kwenye hesabu watoe,
Na sensa kwao utani, ni nani awanyanyue,
Wawatambua mjini, hisani wazitukue,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Maji hamna kijijini, ardhi budi ukamue,
Umeme u mipangoni,Bahati wautumie,
Wanauona wayani, juu yao upitie,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Toka mwaka wa sitini, pale pale wabakie,
Ubaguzi naamini, lazima uondolewe,
Afrika ya kusini, ndo ule waukatae,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Vijijini mikoani, ndio sana walowee,
Hawana lenye thamani, mzazi hana wanawe,
Wakimbilia mjini, wakabakia wazee,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Wamelala vijijini, usingizi muwatoe,
Muwajaze akilini, mfumo wauelewe,
Waingie kwa makini, vyamani wavitumie,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Wavitumie makini, yao yafanikiwe,
Waiongeze thamani, watu bora wachague,
Kuukuza upinzani, huenda kuwasaidie,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Jambo hili ni yakini, kwingine wakatembee,
Wajifunze kwa hisani, kesho yao waijue,
Msiwaache kundini, nje wakatembelee,
Macho kawafungueni, wamelala vijijini!

Jimbo hili jimbo langu


Jimbo hili langu jambo, uchuzi pia kijambo,
Waswahili wana mambo, huzungumza matumbo,
Na wengine huwa nyimbo, zikaimbwa na mgambo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Wazama wenye majimbo, na pepo zaenda kombo,
Wana vikopo vya kimbo, maji kukinga vitambo,
Huenda papo kwa hapo, kuyashibisha matumbo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Hata wakinuka shombo, wadai kilivyo chombo,
Wakajipasua tembo, kwa kuufata mkumbo,
Hajafumbiwa fumbo, mjinga mwenye kitambo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Wameyauza machimbo, toka rombo na urambo,
Ardhi bila malambo, watu wapigwa kikumbo,
Ahadi sasa ni wimbo, maneno kuwa mafumbo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Mchapwa kashika fimbo, mpiga kupigwa kumbo,
Sasa wauza urembo, hata kwa akina gumbo,
Jimbi halijawa jambo, jogoo haimbi wimbo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Kanyi husema isembo, kwa lugha ni wenye shombo,
Mnasa kala ulimbo, kidaka kubaki nembo,
Hujengi nchi kwa pambo, ni nondo na mitarimbo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Wasema hajanywa tembo, bali hiyo yake tambo,
Mamaye mama wa kambo, hakumzaa kwa tumbo,
Kalijali lake umbo, ukweli tuseme tumbo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Namaliza wangu wimbo, kumwimbia mwanakombo,
Maudhui yangu jambo, na halinihusu jimbo,
Nakshi nao urembo, kwangu nahofu ulimbo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Wanielewa wa Bombo, na kote kwenye machimbo,
Wanihesabu Urambo, hata pia kule Rombo,
Mjinga mfumbie fumbo, mwerevu huzusha tambo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Husifu kula makombo, ukawa mzuri wimbo,
Kichwani kuweka nembo, mviringo na kitumbo,
Haliwi likawa tembo, walevi wanuka shombo,
Jimbo hili jimbo langu, upinzani siutaki.

Popo wanahangaika





Popo na nduguze hoi, hawajui pa kutua,
Wanalinda maslahi, yasiye yakapotea,
Wauthamini uhai, vitu wanapojaliwa,
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Wazungumzia rai, mojawapo kufikiwa,
Bila ya kupiga nai, na filimbi kusikiwa,
Huku nusu wanadai, unyama unawafaa,
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Nusu hawajitambui, ni ndege wanadhania,
Hawapai asubuhi, ila jioni wapaa,
Mbawa zao maslahi, mbinguni zawachukua,
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Wasema wanajamii, wanyama waumbuliwa,
Kwa kahawa nazo chai, nje wanachukuliwa,
Na sababu hawajui, na wapi wenda kukaa,
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Na sababu hawajui, na wapi wenda kukaa,
Je, watakuwa ni hai, au waenda kuliwa,
Nchi kama haifai, vipi watajirudia?
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Unyama hauwafai, nchi unawakataa,
Heri kuwa ndege mui, maslahi kupatiwa,
Na hii ndiyo rai, wajamaa wasikia,
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Nafusi hawajijui, kazi yao kudandia,
Gauni na sarawilii, haziwezi kutulia,
Waitafuta nikahi, mabibi kuwanunua,
Popo wanahangaika, wajiunge pande gani ?

Chuoni hawachanui, ukubwa waliopewa,
Chini hawaangalii, macho juu wao huwa,
Watamani nani hii, na udugu usiozaa,
Popo wanahangaika, wajiunge kundi gani ?

Mola tunakulilia





Aibisha viongozi, waongo waliokuwa,
Ainisha wadokozi, fedha yetu kutwibia,
Uwageuze mchuzi, ugali tukaulia,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Wakatie jinamizi, na mate kuwaokea,
Wenye siafu na nzi, wazima waliokuwa,
Kisha wape makohozi, chai yao kujinjwea,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Tai zao ziwe vitanzi, uani kujinyongea,
Na pasiwe fumanizi, mtu kuja waokoa,
Hawa si watu azizi, thamani wamejitoa,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Utupe yako hirizi, dhuluma kutoingia,
Madanzi na makumazi, usoni ukawatia,
Na vidole vife ganzi, ujanani kulemaa,
Mola tunakulilia, waovu kuvumilia!

Matapishi wayazoa




Nimeshtuka kugundua, matapishi wanazoa,
Kwenye sahani kutia, na kisha kuyapakua,
Kama kipya kilokuwa, kikawa chapakuliwa,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Kama kipya kilokuwa, kikawa chapakuliwa,
Na watu wakatengewa, kama mlo kujilia,
Masalo kilipotiwa, uoza haukunukia,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Harufu yake ni mbaya, kila mtu asikia,
Masalo wanayatia, harufu kuiondoa,
Ila kwa wanaojua, siri wanaifukua,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Hadaa wanatumia, nyuma yetu kupitia,
Wakubwa wanunuliwa, kamatini walokuwa,
Halmashauri yavia,wastani kutokuwa,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Wajumbe wanunuliwa, mkutano kuingia,
Uoza kuuchagua, kuongoza Tanzania,
Kuhami waliokuwa, na walivyotuibia,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Kwa wengi wetu kinyaa, kwao wao yawafaa,
Ujinga wautumia, kuwadhihaki raia,
Miaka ilobakia, wataeneza sanaa,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Wataeneza sanaa, vifavyo kuvifufua,
Ahadi walizotoa, wizi wakautumia,
Urongo kudanganyia, watu wakaaminia,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Vijijini wanajua, wajinga watapakaa,
Huko wanawaendea, uongo kwenda wambia,
Kuwa sumu inafaa, sasa chai imekua,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Kuwa sumu inafaa, kama chakula kuliwa,
Ya uoza ulokuwa, kidonda ndugu kinyaa,
Rais kutupatia, kumalza Tanzania,
Matapishi wayazoa, wafanza tena chakula.

Wenye pesa Tanzania




Fedha wameitamia, vifarana kuangua,
Wanasiasa wapewa, kesho kutoangalia,
Na vingine wagaiwa, upofu wakawatia,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Benki waliokwapua, na fisadi kuzipewa,
Madeni walioyatwaa, kwa ujanja na hadaa,
Na miradi kuizua, fedha zinakochanua,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Upofu wanawatia, wanaowashtakia,
Na wengine wanaua, kwa yao kukataliwa,
Shetani ajivunia, nchi kuja kuiua,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Matumbo wajishonea, mawili mawili wavaa,
Nafasi ikitokea, lingine huongezewa,
Jetha kawatunukia, hulka yake kutwaa,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Viongozi wanunua, mfukoni wakati,
Na kushoto na kulia, paredi wanatembea,
Ubepari waingia, hata nguo tutavua,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Na wakubwa wenye njaa, uziwi wameingia,
Zama walizozijua, leo wanafiikiria,
Mradi wajipatia, posho wanayopewa,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Hakuna wa kulilia, nchi yake Tanzania,
Kila mmoja kawania, ya kwake kupigania,
Mwalimu kutondokea, balaa zinazaliwa,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Hakuna alobakia, nchi kuigombania,
Kila mmoja awazia, ya kwake yakamfaa,
Na nchi kutochanua, mradi ajipatia,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Na Mola kawaachia, madhambi kujichumia,
Hadi milima ikawa, na toba kutoijua,
Hatimaye kuwavaa, kuwapa yao hidaya,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Ya ovyo wafatilia, ya utu kutoyajua,
Masikini wanalia, michezo washangilia,
Ushindi usiokuwa, wala neema kupewa,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Nchi wanajigawia, na keki ya Tanzania,
Wazawa pipi kupewa, shukrani wakatoa,
Yao yazidi lemea, washindwa kuyachukua,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Siku ninaingojea, machozi kuyaachia,
Taulo ninaandaa, machozi kujifutia,
Tena la kuogeea, kubwa sana lililokuwa,
Wenye pesa Tanzania, wangojea kutawala.

Idadi kuitambua





Kila mwenye nia mbaya, dini ameikamia,
Idadi kutokuijua, siri kutoifichua,
Katoliki wawanunua, kwao sasa ni bidhaa,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Ukweli wanaujua, wataka kuufikia,
Musuli kuzitumia, waumini wakavia,
Tunawahakikishia, kazi yao kufulia,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Mataifa yaamua, idadi budi kujua,
Na sisi kujielewa, yetu tukajipangia,
Na chetu kilichokuwa, tuweze kupigania,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Wakuu wa kuteuliwa, wakoloni wa mikoa,
Kazi wachangamkia, bwana wao kumfaa,
Islamu wawasumbua, haki yao kutetea,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Dhuluma najionea,Waumini wafanziwa,
Ya kwao wakaonea,na hatiani kutiwa,
Nchi twaisukumia,kule kusikotakiwa,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa ?

Mola tunawaombea, wazidi kujipepea,
Bendera ikasambaa, na upepo kutwaliwa,
Mbele iende chakaa, kufanza isichojua,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa?

Manani twakuachia, dini kuiangalia,
Siridhie kuzuiwa, imani kuendelea,
Nafasi kuichukua, ilokuwa yaibiwa,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa?

Daraja kujipandia, la juu tukajitia,
Islamu twanuia, ya kwetu kupigania,
Wakati ukifikia, hakuna wa kuzuia,
Idadi kuitambua, vita kubwa inakuwa?

Kaitoeni boriti





Boriti kaitoeni, iliyo mwenu machoni,
Hili mkilibaini, kweli hamtozaini,
Itaisha yaniyani, na visa vya mumiani,
Kaitoeni boriti, mje mbongele njiti.

Ya kwenu kayaoneni, kama yana walakini,
Kisha mje ugenini, kusiko kwenu nyumbani,
Muifanze tathmini, haki inayodhamini,
Kaitoeni boriti, mje mbongele njiti.

Na wa kweli waumini, hupenda nyingine dini,
Hasa wakiwa wahidani, mmoja wamuamini,
Lengo kuu la imani, sote kwingia peponi,
Kaitoeni boriti, mje mbongele njiti.

Kiumbe anayehini, hil tusimuamini,
Hakika ni yake dini, mwenyewe kaleta ndani,
Halifai duniani, mpenziwe ni shetani,
Kaitoeni boriti, mje mbongele njiti.

Kama sivyo majinuni, wameoza akilini,
Wafanyao ni uhuni, shetani awazaini,
Uone wao undani, hukuta hawajiamini,
Kaitoeni boriti, mje mbongele njiti.

Wana mengi maovuni, na mengine mafichoni,
Ndoa hawakuahini, wanazaa duniani,
Usafi kimtihani, waishia sifurini,
Kaitoeni boriti, mje mbongele njiti.

Haambiliki





Tukwambie kitu gani, mtu usiyesikia,
Umetushusha thamani, uduni ukatutia,
Hayatoki mdomoni, maneno yakukwambia,
Tukwambie kitu gani, na wewe ni kiziwi.

Sikulaumu mwandani, najua unatumiwa,
Kakuingia shetani, mikono aitumia,
Na akili zi mfukoni, mfuko wamuachia,
Tukwambie kitu gani, na wewe ni kiziwi.

Mikono hatuungani, njia mbali twatumia,
Nakupisha mjivuni, uvune unachopewa,
Yangu yabaki moyoni, kuliko ya kukwambia,
Tukwambie kitu gani, na wewe ni kiziwi.

Haviishi kumlevya...







Haviishi kumlevya, kiumbe mpenda vya bure,
Kidogo akishachovya, huganda kiherehere,
Na wamtakao wajuvya, kwao mvinyo bwerere,
Kama mpenda vya bure, haviishi kumlevya.

Humpa wakemlevya, kisha kumteza shere,
Kama asali huchovya, kisha kula msongere,
Mitego wakaigavya, kumnasa ja tetere,
Kama mpenda vya bure, haviishi kumlevya.

Kuna meli inazama





Anga nikizitazama, kuna meli inazama,
Upepo unaovuma, chaja kidogo kiyama,
Baharini watakwama, na maziwani kuzama,
Upepo huu wavuma, kuna meli inazama.

Nchi haina uzima, mitumba ndiyo salama,
Bunge lenye taadhima, kwalo hilo wafurama,
Wamenunua lawama,tena ni watu wazima,
Upepo huu wavuma, kuna meli inazama.

Upepo unaroroma, na bahari kungurama,
Na maziwa yazizima, hakuna tena salama,
Na mizuka yaungama, kuvuna kwao rehema,
Upepo huu wavuma, kuna meli inazama.

Njaa yao yawatuma, yasopemwa kuyapema,
Salama inayoyoma, ikabakia zahama,
Na kwao zote tuhuma, zaenda kwa wasoungama,
Upepo huu wavuma, kuna meli inazama.

Shilingi ina medali



Shilingi Olympiki, medali imeileta,
Dhahabu wameafiki, tutunzwe kumeremeta,
Ni kweli siwadhihaki, ikulu wanayateta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Baibai mamluki, watu wanashangilia,
Mapenzi sio riziki, na upendo twafulia,
Tumebakia mashabiki, Uswizi kuzimiliki,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Mtanzania mnafiki, aishi kwenye kiota,
Nchini hayaaniki, ila nje yanaota,
Ufalme twaashiki, na ujamaa twasuta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Kulimbikiza mikiki, kila mtu anatweta,
Inawapanda ashiki, nchi wapate pepeta,
Waenziwe kwa milki, ya wenye kiu na njaa,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Waisifia kaniki, eti kwayo twatakata,
Wao wanazimiliki, suti zenye kutokota,
Friji zinazodiriki, ndani huwa zakokota,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Shilingi amediriki, medali ameileta,
Maisha kuwa hilaki, na utumwa kuuleta,
Wakubwa wayabairiki, na kuyapaka mafuta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Na wala sinayo chuki, mimi siye wa kupata,
Haitakati kaniki, dobi siwezi msuta,
Walo wangu marafiki, wataenzi golgota,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Wasema wastahiki, chaguo mola kaleta,
Kweli tunastahiki, taabu kuzikamata,
Tukabakia mabaki, historia kufuta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Waema kaleni keki, kama mkate hamjapata,
Na wala hawadhihaki, hakika si wanaoota,
Hawanao uhakiki, yetu yanavyotokota,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Shilingi yangu rafiki, medali unaileta,
Ila kwetu sisi dhiki, maisha yanatokota,
Kwenda usingestahiki, salama tungeipata,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Akaunti za Uswizi



Sio wasiolijua, hilo wameazimia,
Hazina kuchukuliwa, na benki kuu pia,
Kama mbegu zilokuwa, nje kwenda kupandiwa,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Uchaguzi kiingia, ziende kuchukuliwa,
Na faida kubakia, mwenye jina kujilia,
Kama mnalikaataa, tuone mtu kushtakiwa,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Chama mnakijua, cha njaa kilojaliwa,
Kinajua kutumia, kutafuta chafulia,
Wabakia kuogea, na taka kuzifagia,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Makada wanachagua, vya watu kuvichukua,
Nchi wakaitumbua, ila chama kukifaa,
Ila wengi wahadaa, kingi wakakichukua,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Safu ukiangalia, madini zinatokea,
Hata nayo gesi pia, na petroli zajaa,
Na wanyama kuua, na nje kujiuzia,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Benki kuu watumia, ni ya chama imekuwa,
Gavana wamtumia, hawezi akakataa,
Ndio maana apewa, vinono akajilia,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Hazina wazichukua, hata na wizara pia,
Ni chama chasaidiwa, ili kutoenguliwa,
Kumbe watu wajilia, chenyewe kikafulia,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Mbali sana waanzia, toka makapa kwingia,
Kabla yalijifia, mwalimu kuwaumbua,
Yeye alipojifia, baraka kwao ikawa,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Awamu wanaizaya, ndiyo hii inapaa,
Benki kuu ilizoa, na hazina nako pia,
Mfukoni wakatia, rais kawakubalia,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Nao tunawatambua, Arusha wanatokea,
Na Tabora nako pia,chungu walituvunjia,
Kitu kutokubakia, ufakiri kuenea,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Ndio wanaokusudiwa, urais kuachiwa,
Wa fedha kuzawadia, burushi aliyekuwa,
Ambao wanazichimbua, fedha za Watanzania,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Madini wamevamia, trilioni wachukua,
Simu wamezikamia, bilioni zawafaa,
Na mafuta nayo pia, hisa wanazipakua,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Umeme walihadaa, kampuni kuzizua,
Madeni zikatutia, kulipwa siri ikawa,
Hilo linaendelea, huku sisi twaumia,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!

Wengine kuruhusiwa, Uswizi kuzichimbia,
Taifa kame likawa, hakuna cha kutumia,
Watu wafa watembea, kwa kiu kali na njaa,
Akaunti za Uswizi, chama kukisaidia!



Taifa pasipo baba


Taifa bila wazazi, mambo huenda mrama,
Kumebakia walezi, tena wasiojituma,
Na bahari ya machozi, wana wake wanalia,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Waliopo viongozi, ya watu yarudi nyuma,
Ubinafsi wanaenzi, kwa vitendo na kalima,
Wanajiona waju'zi, nasi hatuna hekima,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Washikilia upuuzi, yenye heri kuyazima,
Na tuhuma za uwizi, zakua kama mlima,
Kulindana ndio kazi, kwa 'ushahidi' hakuna,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Wenyeviti waloenzi, wanaikosa karama,
Wakiahini kizazi, kwa kuupenda uchama,
Kwa njaa nayo hifadhi, mabaya hawatasema,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Kaondoka mwenye hadhi, Mwalimu mwenye kusema,
Vichuguu vyenye ganzi, viko chini ya kilima,
Lenye heri kujajizi, lategemea rehema,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Maisha sasa makazi, na malazi kuyapema,
Na wauza maandazi, huwa hawana rahma,
Huna enzi bila wizi, usio nayo alama,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Baba dunia si mkazi, tumebakia yatima,
Kwa yake makubwa mapenzi, kaiongelea hatima,
Kati yetu wajuuzi, tunaziona alama,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Tunamuomba Mwenyezi, kutuepusha nakama,
Kwa kuwapata viongozi, wa kuzilinda dhuluma,
Ila yaje mapinduzi, kuiondosha nakama,
Taifa pasipo baba, yatima waongezeka!

Ombaomba kwenye suti




Wanashangaa umati, ombaomba kujionea,
Ana tai kwenye suti, na viatu vya kupaa,
Aonekana smati, watu wanamkimbia,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Akiitoa sauti, wadhani anatania,
Sasa kizungumkuti, kichwa kajiinamia,
Huyu ndiye mahuluti, ubepari-ujamaa,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Mavazi kayadhibiti, watu wajua kajaa,
Akisema haileti, watu wadhani kichaa,
Na hakuna katikati, ukweli wa kumwambia,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Anapopiga magoti, kusali wanadhania,
Mhubiri madhubuti, wengine washadidia,
Masikini hawateti, wasije kumuumbua,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Ana gari la spoti, na bembeya kubembea,
Uswizi kaficha noti, wenye njaa kawaibia,
Na bungeni hawalileti, siri yao wanajua,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Kimo chake nusu futi, milingoti atumia,
Ukimuona shurti, kucheka huwa tabia,
Kwenye mvua hatoti, mwamvuli kauchukua,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Wanamuita steti, hati asiyepatiwa,
Kuingia kuna geti, mahala anapokaa,
Tukutuku huileti, lazima itazuiwa,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Wameshamtuku cheti, ombaomba kumjua,
Wakiangalia kabati, ndarahima zimejaa,
Kuomba hawamsuti, wataka kumtumia,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Ah, nchi isiyo bahati, na unafiki kujaa,
Kitanda cha asherati, na nyinginezo balaa,
Halali hauikuti, ni haramu imejaa,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Naiangaza tovuti, ukweli ukasambaa,
Dhana hii ni katiti, kimo haijagaiwa,
Na kwangu halitakati, ni chafu lilokuwa,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Naamini mkakati, waliomo wafulia,
Na kuingiliwa kati, ushauri wakataa,
Wanailea boriri, kijiti wakiumbua,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!

Nipe shehe Mtengeti, nami ninakuachia,
Tano zaidi sileti, ujumbe unshatulia,
Kumbe Mista Raiti, kufika amechelewa,
Ombaomba kwenye suti, ajabu ya Tanzania!


Wajinga wakijanjuka



Ninasema la hakika, mwisho njiani wafika,
Taa inayomulika, hatimaye kuzimika,
Nuru ikatoweka, gizani kuhamanika,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Wajinga waerevuka, na haki yao kutaka,
Sauti inazunguka, na kilio kusikika,
Waliolala waamka, na chao wanakitaka,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Ushindani waumuka, kuupinga ni dhihaka,
Kwa dola kushughulika, raia wakapigika,
Ni ujinga mwautaka, mambo yataharibika,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Demokrasia injika, na chungu kukorogeka,
Nusu nusu ni dhihaka,chakula hakitapikika,
Mzongao mtapwika, na wengine kutapika,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Wajinga wakijanjuka, hadaa huhadaika,
Waliokuwa mateka, kwa bei kununulika,
Ikawa ni kuzuzuka, na kifafa kuanguka,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Umma uliotukuka, unataka madaraka,
Na waporao mamlaka, waziwazi kumulikwa,
Wananchi wana hakika, wao ndio Tanganyika,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Mabaya yaepushika, sauti zikisikika,
Imani zilizowateka, mamluki kuwaweka,
Pembeni zikaondoka, taifa likatukuka,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Ya kundi mkiyashika, umoja utavunjika,
Baragumu lasiikika, na bubu wanatamka,
Haki yao si dhihaka, misuli itatumika,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Uongozi wa dhihaka, haunalo la hakika,
Hubeza ya kuanguka, na kuacha ya kuruka,
Ila Mola akitaka, kila kitu hutoweka,
Wajinga wakijanjuka, mjanja hupapatika !

Bunge hili bunge gani ?




Bunge hili nchi gani, nani wake waumini,
Ninaishi mashakani, sijui la kina nani,
Naona ni majinuni, imani haimo ndani,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Dua wanamwomba nani, wanapokuwa bungeni,
Chao ni kitabu gani, cha sala sio ilani,
Nguzo yao nguzo gani, na ibada yao nini ?
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Islamu mwachaguani, kuwakilishwa bungeni,
Watu hao watu gani, walioishiwa imani,
Wanafata ya moyoni, wala si ya imani,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Anajua majinuni, sheria nazo kanuni,
Wangelikuwa makini, Ijumaa kuamini,
Wakayadai kundini, siku hiyo siyo nuni,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Mchana uwe wa dini, wafanye kazi jioni,
Kawahadaa shetani, hawapiganii dini,
Wanafiki naamini, ishara wazibaini,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Nani amesema dini, na siasa haviivani,
Hilo mimi siamini, chama chetu tusaini,
Wakikataa nchini, kiende kichinichini,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Bunge hili la wahuni, vimini wanatamani,
Tunaapa asilani, sisi kama waumini,
Kuyaiga ya kinuni, tunaenda kitalini,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Miaka ninabaini, twaenda uchaguzini,
Islamu waumini, chagueni muumini,
Wengine wapige chini, tuongezeke bungeni,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Ninamuomba Manani, awajaze waumini,
Ushujaa wabaini, kupigania yao dini,
Tumebaki unyongeni, kuanzia Ujerumani,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Mola tunakuamini, umetujalia dini,
Kuilinda ni auni, kundi hili la amani,
Tutie shime moyoni, tuwaondoe wahuni,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Tutie nguvu rohoni, yetu yote tubaini,
Tukawalipa wahaini, kwa gharama ya uhaini,
Na kuwalipa hisani, kila mtoa hisani,
Bunge hili bunge gani, ladharau Ijumaa ?

Serikali ya kisasi




Funda saikolojia, kichwani ipae kaa,
Ubaya wazaa ubaya, mnapaswa kutambua,
Ukiwa unayemtia, ukiwa atakutia,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Kisasi mwana balaa, kwa haramu kazaliwa,
Haki huwa hakataa, sheria wkatukua,
Hasara wakaizaa, mapacha inayozaa,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Umma mkiuchezea, nao utawachezea,
Wa kuzaa wanazaa, na wao wa kuzaliwa,
Mama asiyemjua, mama humshambulia?
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Aibu ikipungua, uovu hujifungua,
Ni mimba isiyotoa, jema lililojaliwa,
Viroboto huangua, kila kona kuenea,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Watu ukishawagawa, na hawa kupendelea,
Usawa ukapwelea, kwa wengine ni udhia,
Huja wakajichokea, ahera kuichagua,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Haki anayeijua, haachi kuipigania,
Dhuluma ukiitia, wazidi kuwacharua,
Haki wakaililia, kwa udhi na uvumba kuwa,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Jino na kucha kutiwa, maamuzi kuamua,
Pepo wakashuhudia, na msaada kuutoa,
Bendera zikaamua, pande moja kupepea,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Hekima hutonunua, wala bure ukapwa,
Walo nao kufichua, kazi kubwa sana huwa,
Huzungukwa na nazaa, na rahisi kujilia,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Jambo hawatakwambia, lakuweza kukufaa,
Sifa watakusifia, na vilemba kukutia,
Ukija kumang'anyua, kokwa jino hulitoa,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Hali yataka kiasi, kwa pamba si kwa mikasi,
Kamlole muasisi, kwishi pasi wasiwasi,
Ila kwenye kinamasi, huwa maji ya mkosi,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Serikali ya kisasi



Funda saikolojia, kichwani ipae kaa,
Ubaya wazaa ubaya, mnapaswa kutambua,
Ukiwa unayemtia, ukiwa atakutia,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Kisasi mwana balaa, kwa haramu kazaliwa,
Haki huwa hakataa, sheria wkatukua,
Hasara wakaizaa, mapacha inayozaa,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Umma mkiuchezea, nao utawachezea,
Wa kuzaa wanazaa, na wao wa kuzaliwa,
Mama asiyemjua, mama humshambulia?
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Aibu ikipungua, uovu hujifungua,
Ni mimba isiyotoa, jema lililojaliwa,
Viroboto huangua, kila kona kuenea,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Watu ukishawagawa, na hawa kupendelea,
Usawa ukapwelea, kwa wengine ni udhia,
Huja wakajichokea, ahera kuichagua,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Haki anayeijua, haachi kuipigania,
Dhuluma ukiitia, wazidi kuwacharua,
Haki wakaililia, kwa udhi na uvumba kuwa,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Jino na kucha kutiwa, maamuzi kuamua,
Pepo wakashuhudia, na msaada kuutoa,
Bendera zikaamua, pande moja kupepea,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Hekima hutonunua, wala bure ukapwa,
Walo nao kufichua, kazi kubwa sana huwa,
Huzungukwa na nazaa, na rahisi kujilia,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Jambo hawatakwambia, lakuweza kukufaa,
Sifa watakusifia, na vilemba kukutia,
Ukija kumang'anyua, kokwa jino hulitoa,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.

Hali yataka kiasi, kwa pamba si kwa mikasi,
Kamlole muasisi, kwishi pasi wasiwasi,
Ila kwenye kinamasi, huwa maji ya mkosi,
Serikali ya kisasi, ni mama yake maasi.



Hakuna dhambi ya chama



Wao wakikutumia, ubaya kutufanyia,
Kasumba kuiondoa, juu unahujumiwa,
Kiumbe unapoua, ni wewe uliyeua,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Ukinifanza kulemaa, chanzo nakutambua,
Watu kuwalingania, hofu hii wakatia,
Chombo ni kisafi huwa, damu inajifutia,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Dhambi inajifutia, kwa senti uanzopewa,
Ujinga ukitumia, motoni unajitia,
Nani wa kukuoa, hata wazazi hufulia,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!


Uongo ukiutia, dhambi unaichukua,
Hata kama wasemea, chama kilichokuwa,
Au serikali kua, sauti ya kutumia,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Uwizi ukituibia, hazina vilivyokuwa,
Benkini ukazitoa, wachache kwenda tumia,
Dhambi unaichukua, wala si chama tambua,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Uoza ukisifiwa, na wewe unalaniwa,
Haki ukiisiginia, nyayo zenda kuungua,
Kwa mawe ya mkaa, tayari umewekewa,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Wakubwa wakiamua, uliza na kulijua,
Haki lisilokuwa, kiumbe ni kulikataa,
Mzazi tumeambiwa, si kwa yote kumsikia,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Mzazi tumeambiwa, si kwa yote kumsikia,
Dhambi akituambia, ni budi kulikataa,
Mwenyewe kumuachia, njia zake akajua,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Uslama nausia, salama mtabakia,
Dini wasioijua, inafaa kurejea,
Kubaya mwaelekea, tiketi bure mwapewa,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Mazuri nawatakia, viumbe mojaliwa,
Wakakamavu mkawa, ila njia mwapotea,
Dhuluma manielea, dafrari kuchafua,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Kwa haki mkirejea, mavuno mtaachiwa,
Bora yaliyojaliwa, mikosi isiyokuwa,
Na wana mnaozawa, wasiwe wa kulaaniwa,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Yarabi nawaombea, hao wasiojijua,
Njia waliopotea, wabaya wawatumia,
Isafishe yao njia, peponi kuelekea,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi ni yako mwenyewe!

Yarabi nawaombea, hao wasiojijua,
Njia waliopotea, wabaya wawatumia,
Isafishe yao njia, peponi kuelekea,
Hakuna dhambi ya chama, dhambi yako bianfsi.


Sheria za kijahili



Sheria za kununua, majaji waliokuwa,
Upande kuegemea, kwingine kutosikia,
Udhalimu unakuwa, kuzifata si sheria,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Wao wakikutumia, ubaya kutufanyia,
Kasumba kuiondoa, juu unahujumiwa,
Kiumbe unapoua, ni wewe uliyeua,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Ukinifanza kulemaa, chanzo nakutambua,
Watu kuwalingania, hofu hii wakatia,
Chombo ni kisafi huwa, damu inajifutia,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Dhambi inajifutia, kwa senti uanzopewa,
Ujinga ukitumia, motoni unajitia,
Nani wa kukuoa, hata wazazi hufulia,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Uongo ukiutia, dhambi unaichukua,
Hata kama wasemea, chama kilichokuwa,
Au serikali kua, sauti ya kutumia,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria

Uwizi ukituibia, hazina vilivyokuwa,
Benkini ukazitoa, wachache kwenda tumia,
Dhambi unaichukua, wala si chama tambua,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Uoza ukisifiwa, na wewe unalaniwa,
Haki ukiisiginia, nyayo zenda kuungua,
Kwa mawe ya mkaa, tayari umewekewa,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Wakubwa wakiamua, uliza na kulijua,
Haki lisilokuwa, kiumbe ni kulikataa,
Mzazi tumeambiwa, si kwa yote kumsikia,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Mzazi tumeambiwa, si kwa yote kumsikia,
Dhambi akituambia, ni budi kulikataa,
Mwenyewe kumuachia, njia zake akajua,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Uslama nausia, salama mtabakia,
Dini wasioijua, inafaa kurejea,
Kubaya mwaelekea, tiketi bure mwapewa,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Mazuri nawatakia, viumbe mojaliwa,
Wakakamavu mkawa, ila njia mwapotea,
Dhuluma manielea, dafrari kuchafua,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Kwa haki mkirejea, mavuno mtaachiwa,
Bora yaliyojaliwa, mikosi isiyokuwa,
Na wana mnaozawa, wasiwe wa kulaaniwa,
Sheria za kijahili, kuzikataa sheria.

Kila mzuuia wazo



Hawa watu wa uozo, mawazo kwao adui,
Waitafuta mizozo, na tija isiyo hai,
Madhulumu wa matozo, na ziada wanadai,
Kila mzuia wazo, uongozi haumfai!

Uongozi si igizo, latakiwa watu hai,
Wasiofanza gumzo, ila vitendo kutdai,
Na walio na mafunzo, ya filimbi sio nai,
Kila mzuia wazo, uongozi haumfai!

Waliokuwa chelezo, wazo kwao sio rai,
Wanatilia mkazo, yanayotia nishai,
Wayapenda mapumbazo, watu kitu wasidai,
Kila mzuia wazo, uongozi haumfai!

Huo ni wao mchezo, nidhamu hawaijui,
Kila kitu telekezo, heri yao ndugu mwui,
Hufanza kondoo igizo, kumbe hao ndio chui,
Kila mzuia wazo, uongozi haumfai!

Kijibwa mwanavigezo, yaliyomo hayafai,
Na kila mpewa tunzo, amhifadhi adui,
Na kila mwenye mawazo, huonekana hafai,
Kila mzuia wazo, uongozi haumfai!

Mwenye uchumi mgeni


Kapewa nchi mgeni, mirija na pia nyuma,
Na kisu cha Kitangeni, kuku akajikatia,
Na wengine hayawani, hayo tukapuuzia,
Mwenye uchumi mgeni, mwananchi afilisiwa.

Mzawa hana thamani, lazima kubaki nyuma,
Kumtanguliza mgeni, wananchi hili lazima,
Mnajua kitu gani, Waafrika mna noma,
Mwenye uchumi mgeni, mwananchi afilisiwa.

Tumuachieni madini, mkuu alishasema,
Tofali kalibaini, pepo yake kaipema,
Jamaa na wake amini, tuhuma zimeshakwama,
Mwenye uchumi mgeni, mwananchi afilisiwa.

Kamwandika Manani, na sisi tunatazama,
Walii hanalo deni, mtaiona sinema,
Kuchuma wasiochuma, wakafulia kazini,
Mwenye uchumi mgeni, mwananchi afilisiwa.

Madaktari yakini, hivi sasa wanahema,
Kuhemea kwarubuni, wamezibwa kwa kalima,
Na pasi hawabaini, kaioneni dhuluma,
Mwenye uchumi mgeni, mwananchi afilisiwa.

Hiki ni kikundi gani, chenye sifa ya unyama,
Na hii ni nchi gani, isiyokwisha lawama,
Na wasema wenye dini, kwetu dalili ya kiyama,
Mwenye uchumi mgeni, mwananchi afilisiwa.

Wakubwa wakijiuza


Juu wakinunuliwa, watumwa wa chini huwa,
Ndivyo ilivyo dunia, hainao msamahaha,
Wajiuza kwa kujua, au kwa kutokujua,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Wajiuza kwa kujua, au kwa kutokujua,
Yote sawa inakuwa, na utumwa kuingia,
Fedha cheo akapewa, bwana mkubwa akawa,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Fedha inaabudiwa, tena sana kutamaniwa,
Watu wakakimbiia, ingawa kupata mkia,
Njiani wakiumia, pasina kujitambua,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Shetani ndani kwingia, hata watu kuwagawa,
Ikawa ndugu na jamaa, hakuna wa kuridhia,
KIla aliyejaliwa, hudhani amelaniwa,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Hao wakinunuliwa, fedha bwana inakuwa,
Na kila mwenye njaa, rahisi kununuliwa,
Nchi nayo ikizubaa, mnada pia hutiwa,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Masikini hubakia, kaziye ni kuiokoa,
Aliyeshiba nazaa, vya kwake kuviachia,
Waachiwa wenye njaa, hujuma kuifumua,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Nchi wataiumbua, ikisha kuzainiwa,
Kilio watu kulia, mashaka yakiingia,
Wakuu waliokuwa, kwingine kukimbilia,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Marikani wamwachia, hadi ndani kaingia,
Kila nikiangalia, salama sijaijua,
Ndege wanazitumia, kisasi kutugawia,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Uranium wachimbua, salama imeshapaa,
Uongo waongopewa, wajinga wahadaiwa,
Kimya kinachotokea, nyuma ya hilo pazia,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Waandishi wanunuliwa, uongo kujitungia,
Hidaya wakazipewa, ukweli kuukataa,
Hii ndiyo Tanzania, haya yake majaliwa,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Ukombozi watakiwa, safu wasafi wakawa,
Hili ni la kulilia, kuamka na kusinzia,
Mola kutusaidia, mabaya kutwepushia,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Vichaka kuviondoa, vilivyojaa balaa,
Wenyewe kujiumbua, mabomu kuwalipua,
Salama tukabakia, kwa Mola tukirejea,
Wakubwa wakijiuza, wadogo huwa watumwa.

Shikilieni huko juu





Ndipo walipoamua, chini kwao kubomoa,
Na juu wakaambiwa, waanze kushikilia,
Watabaki waelea, au waning'inia,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Dhairi iliyokuwa, hawawezi kununua,
Nyumba nzima kuitwaa, hali bei imepaa,
Kama wakiwachia, na nyumba hawatakuwa,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Na nchi tarajiwa, juu wakinging'inia,
Chini waweza amua, vyao chini kuvitwaa,
Au kujinyamazia, wabaki kuangalia,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Jazba ikitumia, wote huwa wafulia,
Nchi ikahujumiwa, na mizizi kung'olewa,
Ya amani ilokuwa, amani, umoja pia,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Ghorofani wamekaa, chini wawaangalia,
Msiba umetokea, pembeni wanajitia,
Na watu wanapolia, vijisenti wanatoa,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Msingi wajichimbua, na haki yahakikiwa,
Hesabu ikitolewa, mtazilipa rupia,
Ushahidi wafichua, chini sana kunaliwa,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Kaeni mlivyokaa, hatima itawajia,
Badili mkibetua, ajali itatokea,
Na mzuka huzuzua, ukweli mnatambua,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!

Ya Adilu wasikia, Ya miskin tunalia,
SMS twakutumia, haki ukatutendea,
Subira yatuishia, twataka kusaidiwa,
Shikilieni huko juu, wao chini wabomoa!


Asiyetetea haki


Haki asiyetetea, naye ana wake ubaya,
Dhuluma aiachia, wananchi wanaumia,
Hicho anachokipewa, motoni kumchukua,
Haki asiyetetea, dhuluma naye alea!

Huyo naye ni adawa, fukara awaumbua,
Msaada kukataa, awafanzia ubaya,
Thawabu azikimbia, motoni kuungulia,
Haki asiyetetea, dhuluma naye alea!

Kama nasara akiwa, mwana kamkubalia,
Hana kinachopotea, tayari keshautwaa,
Yake anayangojea, zawadi waahidiwa,
Haki asiyetetea, dhuluma naye alea!

Yake anayangojea, zawadi waahidiwa,
Qurani yasimulia, kwa wanayomzulia,
Hili hakufurahia, nao si wa kujitambua,
Haki asiyetetea, dhuluma naye alea!

Hakimu unayepewa, au jaji kuchaguliwa,
Ukiamua sheria, uende kukengeua,
Jua unajiumbua, kwa akhera na dunia,
Haki asiyetetea, dhuluma naye alea!

Madhambi mwajichumia, umma kuutania,
Sisi leo tukilia, milele mwaja kulia,
Huruma nawaonea, viumbe msiojijua,
Haki asiyetetea, dhuluma naye alea!

Walimu na daktari

Mizani nimetumia, dhuluma naikisia,
Haki wanaolilia, kuzidi kushindiliwa,
Sheria ikalemaa, na dhuluma kuachia,
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Mzigo twawaachia, mlo tunauchukua,
Wao wanapoumia, sisi twazidi tanua,
Na pssho twaongezewa, kujinoma si udhia?
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Vifaa twapuuzia, walimu kufundishia,
Mzigo kuwazidia, hadi jasho kuwatoa,
Jiwe tunang'ang'ania, damu lazima kutoa,
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Keki tukiipakua, nusu nyie mwajilia,
Kidogo kikibakia, bado mnakidokoa,
Kwanini waache kulia, kama si kuwaonea,
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Hali zao zinavia, hadi kuuza vitumbua,
Na michicha na bamia, kazi wasizosomea,
Sisi twawaangalia, twasema ni majaliwa?
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Ulafi umetujaa, juujuu kwenda kaa,
Na tunachowafanyia, madudu tupu yajaa,
Uongozi walemaa, nchi vipi itakuwa?
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Wazungu twawaachia, dhahabu waichukua,
Mengi tusiyoyajua, nayo pia wachimbua,
Yakienda huko Ulaya, mwapewa asilimia?
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Twaona zeu jamaa, ndio bura kuwafaa,
Ngawira kuwagawia, kwingine wakazigawa,
Na safari zazidia, zisizo na manufaa,
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Sasa tunawazuia, na kuwanyima rupia,
Sensa tumewaondoa, ujira hatujatoa,
Vijijini wakimbia, mjini kupumulia,
Walimu na daktari, naoana twawaonea !

Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!


AJABU ya Tanzania, kwa mwenge kuukimbiza,
Tope wakaliogea, hakuna wanariadha,
Vipaumbele vavia, masazo kazi kusaza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Tanzania yafulia, yabakia kusuza,
Sera zachakachuliwa, hakuna la kuongeza,
Yanazidi kupungua, sifuri tutaikuza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Amana wanaopewa, matumbo wanayatunza,
Wenyewe kutangulia, wakafata wanawenza,
Ndivyo inavyotokea, vingine huwezi waza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Vijana kuwanyanyua, budi wao kuwatunza,
Mbio watazikimbia, na metali kutunzwa,
Wenyewe tukijilia, tutabakia kuoza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Viongozi waogea, wazuri tuliowaza,
Na kinachoambuliwa, chabakia kuongeza,
Njaa yawashambulia, ni nani wa kuwatunza ?
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Mashule yahujumiwa, kwa michezo kuikwaza,
Wawekezaji wavia, vipaji kutovikuza,
Mapambo tumeazimia, nchi yetu kuitunza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Kidogo kikibakia, kazi yetu kupoteza,
Twafanza tusokijua, na dira kutoangaza,
Hatujui pa kwendea, vipi tutajiagiza?
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Mashauzi yazidia, na vipozi kutuponza,
Shere tunazochewea, zote twazifurahia,
Hakika mwenye kulemaa, hajui kinachomponza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Heshima imepotea, kumbukumbu tunatunza,
Udikteta kuvimbiwa, yote kutaka kufanza,
Mwisho wake waogea, sabuni zilizopooza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Twazoea kutumia, sio watu wa kutunza,
Wala kufikiria, yale yanayoingiza,
Kicheko kimebakia, nchi ikaokoteza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!

Mwenge ninadhania, riadha waweza kuza,
Siasa ikitolewa, na manujfaa kuingiza,
Mwenge michezo kwashiwa, kazi ikawa kwendeleza,
Mwenge tunaukimbiza, wanariadha hatuna!


Hivi sasa ndugu pacha


Waka'ngwa Watanznia, kwa yao wenyewe mafuta,
Hupikwa wakapakuliwa, pasipo hata utata,
Wenye nchi wajilia, wakazidi meremeta,
Hivi sasa ndugu pacha, simu na umaskini!

Wawekezaji wavua, pasipo ya kuchakata,
Sio papa na dagaa, kwenye nyavu utakuta,
Kila siku wavulia, kufulia si wakata,
Hivi sasa ndugu pacha, simu na umaskini!

Dracula wamekuwa, kwa meno wanatung'ata,
Damu wakajinyonyea, na uhai kuupata,
Nyuma tunaobakia, hugeuka mazezeta,
Hivi sasa ndugu pacha, simu na umaskini!

Mashirika twasikia, chama yameshakipata,
Kwetu kinapodonoa, wenye chama wanavuta,
Umelaaniwa ubia, na wanaoupakata,
Hivi sasa ndugu pacha, simu na umaskini!

Siasa wazichagua, na kisha wakazipeta,
Ungo wakatulia, wanasiasa kutota,
Mfukoni wakitiwa, hawawezi kuwasuta,
Hivi sasa ndugu pacha, simu na umaskini!

Nani wa kulibetua, hilo tumeshalipata,
Ni letu la kutundikiwa, budi kuzidi kusota,
Hadi Afu kuamua, nusurra tukaipata,
Hivi sasa ndugu pacha, simu na umaskini!

Viongozi wa mkoa


Hao watu wa kupewa, zawadi wanachukua,
Haki kukutendea, naona haitakuwa,
Humwabudu mteua, kama Mungu kumwofia,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Udugu wanatumia, na uchama kuitia,
Bendera ikipepea, wao inawapepea,
Si huru tulokuwa, katika yetu mikoa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Kampenzi zanunua, kapuni zikawatia,
Sababu nchi kuvia, ni wakuu wa mikoa,
Ya watu kutoyajua, chama kukifikiria,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Wengine wanatumiwa, watu yao kuibiwa,
Madini yaliyojaa, na haki za kidunia,
Kisha wawashindilia, na risasi kutumia,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Viwanja huvichukua, wenyewe kujigawia,
Na mashamba nayo pia, kupona haitakuwa,
Yote wanayamavia, ubepari kuchipua,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Ndani wanawatumia, na nje kuwauzia,
Haki kwao sio nia, ila nia kujilia,
Hawatetei raia, mkubwa wamtetea,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Watu wawashambulia, upinzani kama wawa,
Kwao demokrasia, ni ufalme kuridhia,
Wameila hadaa, kutapika wakataa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Si wema walokuwa, Mtwara ukiangalia,
Dini zinawatumia, wakijidai watawa,
Mambo wawafanyia, ndugu zaburi yajua,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Imani wakihofia, watu watawaonea,
Yao wakayakataa, na uzushi kuwazushia,
Mola haachi chukia, akawaona udhia,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Bure tu hujifutua, kwa dola kuitumia,
Dua tukiwaombea, ulemavu wauvaa,
Waumini mwatakiwa, mamb haaya kuyajua,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Dini ikijitambua, mbali nao itakaa,
Serikali hufatia, Mungu anatangulia,
Jihadi tunajua, ni amri tumepewa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Kiumbe ukijifia, dini yao kutetea,
Peponi utaingia, mambo mema kuridhiwa,
Mola kumsabilia, ni chaguo lake huwa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Ubwana wanajitia, na utwana kututia,
Tunu inayowafaa, madarakani kung'oa,
Wengine tukachagua, viongozi wetu kuwa,
Watu hawawakilishi, viongozi wa mkoa.

Siwezi kujizuia



VYOTE ninavyotamani, umejaliwa mwandani,
Tabia ninayothamini, na uzuri wa usoni,
Mwili ulio sakini, na ngozi ilo laini,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Ni ndoto yangu amini, nikiiota zamani,
Ruia zenye hisani, nikiwaza urulaini,
Kiasi mwangu moyoni, nikajiona jangwani,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Msafiri duniani, vijijini na mjini,
Wengi natia machoni, ila hawawi moyoni,
Hadi nilipobaini, utokako mafichoni,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Sijalisema kinywani, na kuachia saini,
Cheche zikiwa rohoni, utauliza amini,
Kisha ukaja nyumbani, na wala si mitaani,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Nilishachoka moyoni, viumbe sikutamani,
Moto waisha njiani, japo pepo zi makini,
Kisichopo moyoni, sio ashiki mwilini,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Nimelipenda jasmini, ua lisilo nuksani,
Harufuye ni makini, inatembeza puani,
Ukitupa kitandani, miski utazaini,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Nalitauta yakini, lilipo kwenye bustani,
Mche wake niauni, kuja kupanda nyumbani,
Harufu yake niwini, niwapo mwengu chumbani,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Jasmini, asmini, jinalo nalitamani,
Nasibu siiamini, kukupata kilaini,
Ndio niko matesoni, akilini na moyoni,
Siwezi kujizuia, nikaacha kukupenda!

Matajiri Tanzania


Fedha wameitamia, vifarana kuangua,
Wanasiasa wapewa, kesho kutoangalia,
Na vingine wagaiwa, upofu wakawatia,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Benki waliokwapua, na fisadi kuzipewa,
Madeni walioyatwaa, kwa ujanja na hadaa,
Na miradi kuizua, fedha zinakochanua,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Upofu wanawatia, wanaowashtakia,
Na wengine wanaua, kwa yao kukataliwa,
Shetani ajivunia, nchi kuja kuiua,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Matumbo wajishonea, mawili mawili wavaa,
Nafasi ikitokea, lingine huongezewa,
Jetha kawatunukia, hulka yake kutwaa,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Viongozi wanunua, mfukoni wakati,
Na kushoto na kulia, paredi wanatembea,
Ubepari waingia, hata nguo tutavua,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Na wakubwa wenye njaa, uziwi wameingia,
Zama walizozijua, leo wanafiikiria,
Mradi wajipatia, posho wanayopewa,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Hakuna wa kulilia, nchi yake Tanzania,
Kila mmoja kawania, ya kwake kupigania,
Mwalimu kutondokea, balaa zinazaliwa,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Hakuna alobakia, nchi kuigombania,
Kila mmoja awazia, ya kwake yakamfaa,
Na nchi kutochanua, mradi ajipatia,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Na Mola kawaachia, madhambi kujichumia,
Hadi milima ikawa, na toba kutoijua,
Hatimaye kuwavaa, kuwapa yao hidaya,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Ya ovyo wafatilia, ya utu kutoyajua,
Masikini wanalia, michezo washangilia,
Ushindi usiokuwa, wala neema kupewa,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Nchi wanajigawia, na keki ya Tanzania,
Wazawa pipi kupewa, shukrani wakatoa,
Yao yazidi lemea, washindwa kuyachukua,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.

Siku ninaingojea, machozi kuyaachia,
Taulo ninaandaa, machozi kujifutia,
Tena la kuogeea, kubwa sana lililokuwa,
Matajiri Tanzania, wangojea kutawala.


Shilingi Olympiki



Shilingi Olympiki, medali imeileta,
Dhahabu wameafiki, tutunzwe kumeremeta,
Ni kweli siwadhihaki, ikulu wanayateta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Baibai mamluki, watu wanashangilia,
Mapenzi sio riziki, na upendo twafulia,
Tumebakia mashabiki, Uswizi kuzimiliki,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Mtanzania mnafiki, aishi kwenye kiota,
Nchini hayaaniki, ila nje yanaota,
Ufalme twaashiki, na ujamaa twasuta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Kulimbikiza mikiki, kila mtu anatweta,
Inawapanda ashiki, nchi wapate pepeta,
Waenziwe kwa milki, ya wenye kiu na njaa,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Waisifia kaniki, eti kwayo twatakata,
Wao wanazimiliki, suti zenye kutokota,
Friji zinazodiriki, ndani huwa zakokota,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Shilingi amediriki, medali ameileta,
Maisha kuwa hilaki, na utumwa kuuleta,
Wakubwa wayabairiki, na kuyapaka mafuta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Na wala sinayo chuki, mimi siye wa kupata,
Haitakati kaniki, dobi siwezi msuta,
Walo wangu marafiki, wataenzi golgota,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Wasema wastahiki, chaguo mola kaleta,
Kweli tunastahiki, taabu kuzikamata,
Tukabakia mabaki, historia kufuta,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Waema kaleni keki, kama mkate hamjapata,
Na wala hawadhihaki, hakika si wanaoota,
Hawanao uhakiki, yetu yanavyotokota,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!

Shilingi yangu rafiki, medali unaileta,
Ila kwetu sisi dhiki, maisha yanatokota,
Kwenda usingestahiki, salama tungeipata,
Shilingi ina medali, imeshinda riadha!


Kumbe wanaenda choo...


Saa zinaishilia, na maisha yaishia,
Hakuna la kuongeojea, ukichelea wavia,
Kula wanaojilia, hata wakazidishia,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Kizuri kinacholiwa, kumbe mate kimetiwa,
Makohozi nayo pia, utamu kuongezea,
Pembeni hujichekea, kwa kila aloandaa,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Ukubwa kujititimua, njiani wanapokuwa,
Na saluti kupuziwa, shenzi wakaziachia,
Hakuna anayejua, nani moyoni kwingia ?
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Mmoja nimesikia, mlinzi ndani katia,
Eti kisa kutumia, choo cha mheshimiwa,
Afrika ina jaa, mengine kama usaha,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Watu wanajisheua, vyeo wakivikalia,
Kisha wakaparamia, hata wasiyotakiwa,
Na katiba kupindua, wao juu wakakaa,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Vidogo wanaugua, makubwa watayajua?
Vyoo vya mheshimiwa, masalo vinanukia,
Ila vya wake raia, utataka kukimbia,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Islamu tungekuwa, usafi tungeujua,
Udhu kutokuujua, janaba nayo twatembea,
Mola wamsujudia, huku kashfa wamejaa,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Udi waliojitia, shetani kawapatia,
Na mavumba yamejaa, ni ubani wa chokaa,
Hakuna cha kunukia, kunuka ni maridhia,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Pepo ya kila msifiwa, kwenye dampu huishia,
Takataka na vinyaa, haachi kuvichukua,
Ingelikuwa mbolea, pengine ingewafaa,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Tanzu ninamalizia, kuntu nilowaambia,
Hitilafu nimejua, chooni inaanzia,
Mafunzo tukishapewa, ukubwani kuingia,
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Uchafu waujua, kwa kuwa choo waingia,
Mbona wanatuachia, jamii kukanyagia,
Kinyaa chawapotea, au wamekusudia ?
Kumbe wanaenda choo, muda mrefu kukaa!

Ufunguo wa bustani



Bustani imefungwa, watu taka wakalia,
Hakuna kilichopangwa, kila mtu atupia,
Mhonga naye mhongwa, pacha sasa wamekuwa,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Makamasi yanapngwa, na uoza waingia,
Harufu inacharangwa, haramu iliyokuwa,
Wamati[wa ma vichanga, wabakwaji wakizaa,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Hawalioni ni nongwa, viumbe wametulia,
Ndarahima zawazonga, utuf wakaufulia,
Kuogea wanapangwa, ibilisi kumwogea,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Masanamu wanachongwa, karne iliyoingia,
Viumbe kutabananga, na sujuda kuzitia,
Wamcha mwenye kuhonga, riziki kumuachia,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Uongo wanautunga, na vyombo kuviutmia,
Nusura visivyokingwa, ila maovu kulea,
Nafasi zao zazugwa, waja waliopotea,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Wangojea kujagangwa, ukuu wakapatiwa,
Mikoa wasipopangwa, wilaya huwatumia,
Demokrasia mkunga, haramu yaiandaa,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Zamani nilishatengwa, na wekundu kuwekewa,
Sikukubali kuzugwa, wakubwa kunitumia,
Waniaga nawaaga, mbalimbali twatembea,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Mnyonge kama mfungwa, ridhaa hawezi toa,
Kaziye yeye kuchungwa, na bakora kugaIwa,
Na nchi isiyozinga, watu wake huchakaa,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Huchakaa wakakongwa, na migongo kuugua,
Huku wanakaarangwa, kwa mafuta ya kutoa,
Nafsini wakaengwa, ubaya na umaluni,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Nafsini wakaengwa, ubaya na umaluni,
Wakakuta wanatengewa, na haki na masikini,
Hapa wameshafinyangwa, kubadili sio nia,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.

Mlango haukufungwa, wa saba naupitia,
Yaishia yamnyengwa, kauli sio hatia,
Kwa udugu wanazongwa, mambo yao wafulia,
Ufunguo wa bustani, nimeuweka mfukoni.



Hadhi ya maji kujua




Ukitaka kuijua, isumbuayo kadhia,
Kijijini kuingia, kisha maji kullia,
Nawe ukajaimbiwa, wimbo wa kiu na njaa,
Hadhi ya maji kujua, ukose hata ya kunywa!

Halafu ikatokea, kanzu umeichafua,
Wataka doa kutoa, maji adimu yakawa,
Tayamamu kunuia, hali bado wazubaa,
Hadhi ya maji kujua, uchafu ukishajitia!

Kinamama wanalia, kilomita watembea,
Si moja ninakwambia, hizo zaweza kuwa kadhaa,
Alfajiri kujitoa, kudamka wakimbia,
Hadhi ya maji kujua, umbali ukitembea!

Hubakwa kwenye majia, na wengine kuuawa,
Na nyumbani kuibiwa, usalama kusinyaa,
Maisha kuwa balaa, na zikachanika ndoa,
Hadhi ya maji kujua, umbali ukitembea!

Nguo chafu utavaa, harufu zinazotoa,
Jasho lililogandia, tena gumu kulifua,
Kitambaa kufubaa, cheupe cheusi kuwa,
Hadhi ya maji kujua, ukose ya kufulia!

Kwenye miji wafulia, vyoo vibovu kujaa,
Vinyesi vinatembea, watalii vimekuwa,
Vyatisha kwenye njia, muumini waduwaa,
Hadhi ya maji kujua, ingia choo bila maji!

Misikiti hukimbiwa, maji adimu yakiwa,
Ibada haitakuwa, bila maji kujitia,
Usafi waamriwa, vingine haitakuwa,
Hadhi ya maji kujua, msikiti hukimbiwa!

Kodi wanajilipia, maji yazidi potea,
Na ahadi zatolewa, pembeni kwenda tokea,
Maonyesho kwenye njia, sinema bure twapewa,
Hadhi ya maji kujua, usiwe na ya kuogea!

Twakukabidhi Radhia, kuiondoa kadhia,
Mwelekeo wadumaa, suka njia kapotea,
Imebaki majaliwa, salam kujipatia,
Hadhi ya maji kujua, umbali ukitembea!