Monday, October 31, 2011

Ukoloni wa mweusi

Wa weupe ukoloni, haukuwa wa kisasi,
Kumezuka majinuni, wa bakora na bisibisi,
Kuwapinga uhaini,watakujakutoa kamasi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Hujikweza kiutani, akaipita kamusi,
Maneno kwa dizaini, ni lukuki na fususi,
Na kumbe ni majinuni, nchi yapata nakisi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Mipango haubaini, ukoloni wa mweusi,
Mambo yenda kwa anwani, za ahali na watesi,
Hana anayemwamini, na mapya hawaasisi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Ungejua walakini, wakati unavyoasi,
Umdhaniye makini, kabeba zake nuksi,
Ya uani barazani, hawana siri wasusi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Mweupe alithamini, tasihili na wepesi,
Goigoi kuwahini, wasiwalete waasi,
Njia akazibaini, si kwa thuluthi na sudusi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Alihofu uyakini, hilo hakuwa mwepesi,
Aliyatia shakani, ambayo hakuakisi,
Hakuna aliyemwamini, hata mke na damisi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Kusoma aliamini, hakuacha kudurusi,
Kubahatisha mgeni, hilo hakutanafusi,
Kakataa usanii, kama hauna asasi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Na katika mitihani, hakutunyima maksi,
Kila aliye makini, haki kapewa kiasi,
Na pia wakashaini, washairi na watesi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Weusi kama utani, wazidi kwa ubinafsi,
Vya kwao huvithamini, na sio vya kadamnasi,
Kishenzi hujiamini, vigumu dhiki kuhisi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Wananchi wanshabaini, ukoloni wa mweusi,
Tofauti dizaini, atharize mahsusi,.
Kadhalika walakini, balaa pia mikosi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Niepushe aliamini, kwa hasira na kisasi,
Nipe adili auni, fukara au mkwasi,
Nikidhie tathmini, sheriazo nisiasi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Nikwepe uhayawani, nitese nisianisi,
Nijaze kheri kichwani, daima nisikuasi,
Nifanye mtu makini, kwa ushauri wa asasi,
Ukoloni wa weusi, heri ya ule wa weupe!

Niuzieni kijiji

Nanena kama kuuza, kweli ndiyo yenu kazi,
Kijiji nawajuuza, nitafanya manunuzi,
Watu mkishawapuuza, ninapenda hiyo kazi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Madalali napuuza, nawaombeni wajuzi,
Msije kuja niiza, wala kufanya ajizi,
KIfedha ninajiweza, ardhi nataka hodhi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Ni mtu wa kuwekeza, kama hamjamaizi,
Na simwamini Pweza, hata atoke Uholanzi,
Nai nitaipuliza, naye awe hajiwezi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Mchezo wangu hucheza, waroho na walanguzi,
Na hata wasiojiweza, siwapi na siwatunzi,
Thawabu kulimbikiza, mengineyo upuuzi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Jua chungwa sio chenza, ingawa mmoja mzazi,
Wasemao nimeoza, sina ila maombezi,
Laniogopa jeneza, na nyie hamniwezi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Ukubwa ninauweza, kwani wengine washenzi,
Sio kazi kuongoza, mbona nina mwingi ujuzi,
Trilioni ukichuuza, utashindwa na vibuzi?
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Waandishi nawakweza, ninaifanya palizi,
Watu wasiojiweza, kuukata siwakwazi,
Kwangu mchuzi wa pweza, vitafunwa na mandazi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Huanza kwa kuyauza, mashamba ya wanagenzi,
Kisha watafululiza, kuuza hata makazi,
Na mwishowe huweza, kuwauza vijakazi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Wanajifunza kuuza, hiyo ndiyo yao kazi,
Tena vya wengine huuza, vyakwao hawaviuzi,
Si shaibu si ajuza, hubaki kwenye simanzi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Mie ninaitanguliza, nia yenye uwokozi,
Kijiji mkikiuza, iwe kwangu mnunuzi,
Kisha wote nitafunza, wajue shika mianzi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Mianzi wataicheza, kwa muziki wa mahadhi,
Ya moyoni hawataviza, wataacha waziwazi,
Ngoma hamtaibeza, na kucheza hamuwezi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Nyumba tutatengeneza, kwa makuti na mabanzi,
Kodi nitakayotoza,ni huruma na mapenzi,
Gharama ni mangimeza,na waongo waenezi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Nitalindoa giza, kwenye nuru wabarizi,
Juu nitawaongoza, wazipande hizo ngazi,
Wataweza wasichoweza, kwa rehema na majazi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Watajua nani funza, na nani ni kiongozi,
Ufukara watasaza, wakiona mbalamwezi,
Atue kifimbo cheza, na bakora kuienzi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Ushuru sitautoza, kwa kaniki na viazi,
Vipi utawaunguza, motoni wenye makazi,
Laana nitaichagiza, hata kwenye usingizi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Milki nitatangaza, ni marufuku kwa wezi,
Fisadi nitawangaza, watunukiwe vitanzi,
Wanasiasa sikiza, ngoma hii hamuwezi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Viongozi kwenye giza, mtayavuna masinzi,
Mshindwao kuongoza, chini mpate makazi,
Njia wanaotengeneza, tutawapatia kazi,
Niuzieni kijiji, ili chote kiwe changu!

Sawaka

Eti katumwa na mzuka, sawaka anazunguka,
Sumu yake kaitwika, kwenye jino kaiweka,
Kila anapopachika,mauti hupumzika,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Sumu wameneemeka, sawaka wa Afrika,
Hasira zikiwashika, ovyo wanaitapika,
Kokote huipachika, hata kwa waliowaweka,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Na wanakoathirika, ni kule wanakoleleka,
Aidha huaminika, sumu imeshawatoka,
Nyumbani ukiwaweka, salama haitatoweka,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Neno husambaratika, pale wanapo kurupuka,
Wengine juu huruka, mijino kuichomeka,
Watu wakahamanika, wasiweze kutimka,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Kaskazini hutoka, hadi kusini kufika,
Sio wa kuaminika, hawawezi kufugika,
Bora porini kuweka, na chatu kukutanika,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Mishipa imenitoka, nyoka anavyoogopeka,
Na akifa hufufuka, akazidi kukusaka,
Vigumu kuelezeka, ni kioja cha hakika,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Rahisi kuterereka, utelezi ukiweka,
Kutamba huja kuchoka, na misuli kumvuka,
Chini akajibweteka, na kichwa kikamtoka,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Mauti yakimfika, pumzi hupumzika,
Kichwa akishakatika, hawezi kuja fufuka,
Na mkia ukiondoka, nduguze hawatamzika,
Sawaka wa Afrika, sumu wameneemeka!

Mapori bakini nayo

Wanyama 'wetu' twauza, mbaki nayo mapori,
Fedha twataka tengeza, hatuichezi kamari,
Hakuna wa kutuiza, hii ya hija safari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Njaa inatuongoza, na wala si ujuzi,
Teua kilichooza, samadi ni matumizi,
Na mbwa naye ukicheza, masjidi fumanizi,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Kijani tumeagiza, ni rangi yetu ya kheri,
Dunia tunaijuza, kwetu heri huwa shari,
Uroho unatumaliza, na wala sio kiburi,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Hatukuja kutengeza, tumekuja kuathiri,
Nchi tutaigeuza, iwe kama harakiri,
Wenyewe mnajimaliza, kutimiza wetu urari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Ahera tunawatanguliza, kuziepuka hatari,
Kadhalika kumaliza, gharika na ufakiri,
Kesho yenu twatengeza, hampaswi kufikiri,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Mwadhani mmetuweza, na sisi ni wajeuri,
Na sasa twawachuuza, kuupata utajiri,
Wazee tukishawatunza, huziondoa hatari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Wazawa mate kumeza, hiyo ndiyo yao kheri,
Vyenu vyote twaviuza, na mkose ujasiri,
Mkishindwa kuyameza, kuna za bure safari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Msisubiri mwangaza, kutakucha mghairi,
Na utu kutanguliza, mtajikuta washairi,
Twala na tunamaliza, ni nani mwenye jeuri?
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Magari maendeleo

Vigelegele watoto, magari maendeleo,
Hii kubwa yenu ndoto, kwa yale myatakayo,
Twawapa huu uoto, myajenge matamanio,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Hata bila ya kipato, yaweke matarajio,
Mbona haya ni mchoto, usihofu mwanakwao,
Ukishindia ruketo, bado unalo gawio,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Ni haki yako mtoto, gari ni la kwako gao,
Baba hakupigi ngoto, yeye na mama la kwao,
Babu na bibi si ndoto, pia kuwa na kipandio,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Hata pasipo vipito, tunataka matokeo,
Kwenye tope si kokoto, haya ni maendeleo,
Na pasipo zimamoto, kuna bima yako ngao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

KIna Kurwa kina Doto, hii ni dunia yao,
Acheni malipyoto, ya kitoto madai yao,
Ni kipi chenye mvuto, kwenye maendeleo?
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Ni kipi chenye mvuto, kwenye maendeleo,
Kulikoni kaamoto, Japani tununuayo,
Motokaa za Kyoto, Uchina pia Tokyo,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Tumezitimiza ndoto, ndani wapo walalao,
Ni viota vyenye joto, kwa wote wapendanao,
Si makaburi mazito, vibaya watumiao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Nyumba hazina mapato, hujanjaruka waishio,
Budi kuwapa mseto, na ajira bila mafao,
Zifutike zao ndoto, magari yawe ni yao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Kwa mkopo mikong'oto, huisha jeuri yao,
Wawe kama ni watoto, rambaramba iwe yao,
Na wakishindwa makato, ukata uwe ni wao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Chakula kimchakato, hutunza afya yao,
Wataliongeza joto, zirudi akili zao,
Hvi yafanye mpito, haya yasiwe ni yao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Ajali zipate uzito, kukata maisha yao,
Nyota ya kijani keto, kucheza mchezo wao,
Hati hii hati ya mkato, huibua yaeleayo,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Yende hadi Kibongoto, Siha hadi Rahaleo,
Yawazuzue Mporoto,wao na vizazi vyao,
Nguo zisiwe misuto, mitumba ni hadhi yao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Magari ni manukato, maua yachanuayo,
Hulea hawa vizito, maboya ya sera zao,
Kwa karatasi uzito, huwa ndiyo deni lao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Tanzania mtokoto, ni wengi yawasumbuao,
Hivyo vyombo vyenye moto, na njiani vituko vyao,
Pikipiki na mkokoto, ni wengi waumiao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Ipepeteze pepeto, pumba na chuya ziwayo,
Wahitaji na kung'uto, kwa haya uyachujayo,
Ukubwa kana utoto, malezi hayana mwao,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Naufanya mchakato, historia jana, leo,
Unapoangaza moto, kwa jotole na baridiyo,
Samaki wangu ni sato, sangara si kitoweo,
Magari maendeleo, dhana mpya Tanzania.

Mapori bakini nayo

Wanyama 'wetu' twauza, mbaki nayo mapori,
Fedha twataka tengeza, hatuichezi kamari,
Hakuna wa kutuiza, hii ya hija safari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Njaa inatuongoza, na wala si ujuzi,
Teua kilichooza, samadi ni matumizi,
Na mbwa naye ukicheza, masjidi fumanizi,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Kijani tumeagiza, ni rangi yetu ya kheri,
Dunia tunaijuza, kwetu heri huwa shari,
Uroho unatumaliza, na wala sio kiburi,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Hatukuja kutengeza, tumekuja kuathiri,
Nchi tutaigeuza, iwe kama harakiri,
Wenyewe mnajimaliza, kutimiza wetu urari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Ahera tunawatanguliza, kuziepuka hatari,
Kadhalika kumaliza, gharika na ufakiri,
Kesho yenu twatengeza, hampaswi kufikiri,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Mwadhani mmetuweza, na sisi ni wajeuri,
Na sasa twawachuuza, kuupata utajiri,
Wazee tukishawatunza, huziondoa hatari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Wazawa mate kumeza, hiyo ndiyo yao kheri,
Vyenu vyote twaviuza, na mkose ujasiri,
Mkishindwa kuyameza, kuna za bure safari,
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Msisubiri mwangaza, kutakucha mghairi,
Na utu kutanguliza, mtajikuta washairi,
Twala na tunamaliza, ni nani mwenye jeuri?
Mapori bakini nayo, wanayama 'wetu; twauza!

Hudhalilika mjanja

Ukubwa wanaoonja, kuuacha hujikinga,
Huutafuta ujanja, vyeo vyao kuvizinga,
Hudiriki kuwapunja, wanaodhani wajinga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Wanazuka chinjachinja, mumiani wanawanga,
Utamu wanaoonja, kuukosa wanaganga,
Naona alama za denja, Kaole na Sumbawanga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Nchi ni chake kiwanja, cha nchi anayejenga,
Mwananchi havuti ganja, na huwezi kumfunga,
Akishakwa mjanja, hukukimbia waganga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Wazuka wapya viranja, wasaga kisha kutwanga,
Kina Mhina pia Minja, uchifu hamtawavunga,
Makabila yataanja, heshima yao kudunga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Msijifanye wajanja, wananchi wawe wajinga,
Miiko mshaivunja, sasa mwataka matanga,
Na nchi mwenye kuvunja, ni kiongozi mjinga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Hudhalilika mjanja, akiigiza ujinga,
Utajipakaje wanja, kama nisai kuringa,
Unauweza msanja, au wataka tuvunga?
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Nchi yaweza jikunja, na nyie ikawasonga,
Uongozi si ujanja, ila ni nchi kuiganga,
Enzi za wale wajanja, ukomo zimeshagonga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Wajua mimi si mjanja, mmiliki ardhi na anga,
Nachunga changu kiwanja, peponi unachojenga,
Huu mwiko sintavunja, na sihitaji ubingwa,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Mimi mtu wa kubanja, nitawezaje kuringa,
Hali yangu ya ugonjwa, lipi kubwa nitajenga,
Mtu wa kuni kuchanja, ghorofa siwezi jenga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Watatafutwa na ninja, kuvurunda wakiganga,
Watageuzwa makanja, mafundi wa kuboronga,
Na mifumo watavunja, ahali wanaowakinga,
Hudhalilika mjanja, akijifanya mjinga!

Saturday, October 29, 2011

Wazungu hawana kazi

Uzunguni kiangazi, hakuna wa kuajiri,
Maprofesa wazuzi, wanakuwa mafakiri,
Kisa si kukosa kazi, ila hapana mwajiri,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!


Marekani kaskazi, wamekwisha waajiri,
Wanazuka mabitozi, kuugani ushairi,
Ngonjera za nguvu kazi, na ajira kutabiri,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Mkowapi viongozi, wazungu kuwaajiri,
Nchi hamuiendelezi, na fursa kuabiri?
Hii neema ya Mwenyezi, nyie mwaiona shari?
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Tunataka wafanyakazi, tena walio hodari,
Kuendeleza ujenzi, barabara na bandari,
Kadhalika uvumbuzi, wa meli na manowari,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Umeme kwetu ajizi, mitambo sio akheri,
Tuwaiteni wajuzi, kuja kufanya urari,
Sayansi kuipa kazi, kuepukana na shari,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Wahandisi waso kazi, na waliokwishajiajiri,
Hili hamjalimaizi, kuwepo kwa askari,
Waliosoma na hadhi, na ufundi kukariri?
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Ubia mkimaizi, nchi itapata heri,
Ni mengi sana majenzi, sasa hatutaghairi,
Hata vijiji kuenzi, karne hii viabiri,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Inanitia simanzi, kuona kuna jeuri,
Na pengine ni ushenzi, majivuno na kiburi,
Nchi yataka wajenzi, sisi twafanya hadhari,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Amkeni viongozi, twataka unda magari,
Kununua kubwa kazi, tunazidi ufakiri,
Ama baadhi na baadhi, inkishafi sighairi,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Kosa akili ya ujuzi, lakini sio minghairi,
Usikose utambuzi, pale palipo na heri,
Majuu kwenye wajuzi, kunataka itihari,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Wahandisi wanafunzi, wazungu watahadhiri,
Wajifunze kwenye kazi, reli zote kuabiri,
Safari na uchuzi, uje kuwa wa kheri,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Utafanyika ujenzi, Unguja binghairi,
Meli mpya zienzi, tuziondoe hatari,
Sisi tuwe ni wajenzi, na wauza kwa fahari,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Yatafanyika majenzi, makubwa yaliyo kheri,
Nchi irindime kazi, bila kitu kusubiri,
Waongezeke wajuzi, na makubwa kubashiri,
Wazungu hawana kazi, wangoja tuwaajiri!

Hamsini yanihini

Afkani siamini, hamsini majinuni,
Sijailola nishani, na medali sizioni,
Tasnia hii gani, hamsini yanihini,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Tata nilishabaini, ugumu sikamini,
Ni likubwa letu deni, kuliko pato yakini,
Na pengine hazinani, thamani yake majani,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Ni Kaleb na Kaini, wananchi na wahisani,
Na viongozi nchini, wengine mabaniani,
Na kiatu yumkini, ni dawa ila siioni,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Nilichokifanya ni nini, sijajua kwa yakini,
Nilishindwa kitu gani,hadi bado maskini,
Ujinga na uzaini, wachangia ktiu gani ?
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Nimefanyiwa na nani, nami nimefanyiwani,
Kwa shilingi na pauni, nimepata kitu gani,
Ni asilimia gani, yangu na hao wageni,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Wamekwiba kitu gani, tangia ya ukoloni,
Na leo niko taabani, waendelea kufanyani,
Isiwe hesabu za nyani, daima nusu shakani,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Au biashara guni, gumba isiyo auni,
Wanunua hamsini, wauza kwa ishirini,
Au mtaji wa deni, kwa riba uhasarani,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Hainingii akilini, mimi kuwa shereheni,
Ni ndoa ya majinuni, hajui ya kesho ni nini?
Atumia milioni, kesho aomba thumuni,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Walopata wamewini, muwachache furahini,
Na ndivyo ya duniani, yanavyokuwa vichwani,
Kwani miye kitu gani, apataye mwanandani,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Kitendawili yakini, kwa walio mashakani,
Na mgumu mtihani, kwa wasio majinuni,
Kombakomba wako mjini, kukavu kwetu shambani,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Maji hatunywi bombani, tunakunywa topeni,
Matofali niamini, ndio viti mashuleni,
Kompyuta hatuioni, twaisikia redioani,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Vijiji ni nchi gani, nina mashaka kichwani,
Si Tanzania nadhani, lazima sayari ngeni,
Kama hamuamini, wakubwa tembeleeni,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Hizo taa za mjini, zisiondoe uoni,
Nchi bado maskini, na watu wako taabani,
Sherehe tuziageni, tufanye ya afueni,
Yanihini hamsini,naishindwa tathmini.

Tuesday, October 25, 2011

Masika Uarabuni

Pengine hatufanani, lakini yanatufika,
Si wa nje si wa ndani, dunia yabadilika,
Upole unahaini, vijana wanacharuka,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.


Wanapoteza imani, wale wasionufaika,
Hawaishi kwa karni, bahati nusu kufika,
Wasipopata auni, miaka haitafika,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Wataka matumaini, na maisha ya hakika,
Wajue ni jinsi gani, waweza kusalimika,
Na kizazi chao njiani, huduma zahitajika,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Maneno wamebaini, mfupa hutovunjika,
Na sasa wanasaini, tamko la kutikisika,
Asiyeleta pauni, mwenyewe ataondoka,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Kazini na mahuleni, wote wameshastuka,
Hawataki ya uani, wanataka ya hakika,
Fisadi kaeni chini, vipi watapoozeka?
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Na wazazi majinuni, lao halitakubalika,
Wachekwa wa zamani, uoga umewazunguka,
Haya ni maisha gani, wakataa kukubalika,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Vipi wajipa thamani,hakuna linalofanyika,
Mijini na vijijini, kizazi kinataabika,
Huu uongozi gani, watu wasiponeemeka,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Wakubwa wajidhamini, hata wasipohusika
Wake wawathamini, na ahali waliozalika,
Laki si baki yakini, na hao sio shirika,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Apartheid wadhani, sasa hapa yafanyika,
Wapo wanaojidhani, wao wa kuthaminika,
Na wengine maaluni, na hawatohesabika,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.


Mtunzi nabaini, hofu nimeiandika,
Lakini haya yakini, ndiyo yanayofanyika,
Kama kukosa amani, chimbuko linachimbuka,
Masika Uarabuni, rasharasha Afrika.

Hadhi yetu ni kaniki

Hakika hili sipati, wadhifa nikihakiki,
Mshairi siwasuti, na wala siwashtaki,
Naitafuta risiti, na kile mnachomiliki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Hali yenu hatihati, mnavaa ya malaki,
Kuunganisha sikuti, mikono inshataliki,
Na majibu siyapati, ya haramu au haki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Najua kuna tovuti, na redio mnamiliki,
Televisheni zi kati, na simu zinatamalaki,
Wastani hauleti, hesabu haihesabiki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Ajabu kuvaa suti, na hadhi yetu kaniki,
Za kiume na sketi, wakwasi wataharuki,
Sijui ni utanashati, au unyani twadhihaki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Ingekuwa shuruti, China isingeafiki,
Mandela angetroti, awe naye mnafiki,
Baridi ya afriti, Afrika haifiki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Hainikwami sauti, tai sijaiafiki,
Nisingemimina beti, ila kwa sauti haivaliki,
Nikiwaza malimati, fakiri wasivyonaki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Unafiki hauvuti, wengi kwenye halaiki,
Waona kama nishati, kuwepo haiaminiki,
Kwa wengi sanda ni suti, huvaa bila kumiliki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Mtenzi nimetafiti, na hili sijabariki,
Tutafute ya bahati, mavazi yenye ashiki,
Waafrka tuketi,mila zetu tuhakiki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Tubuni yetu mashati, na sarawili za kindaki,
Kinamama ni sketi, na magauni ya saki,
Hakimilki idhibiti, watuige Waturuki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Ya Mswati ya Mswati, ya kwetu yanashtaki,
Taifa kujizatiti, desturi zitamalaki,
Zesha za kina waiti, zaja za chaki na cheki,
Mbona mnavaa suti, na hadhi yetu kaniki?

Sukari ashike nani

Hekima bila anwani, huishia ufukweni,
Na wapangaji makini, kubadili uhaini,
Mbele nyuma si auni, ni tabia ya kihuni
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Soko huru kubaini, vipi twavunja kanuni,
Twatafuta kitu gani,ili kumpendeza nani,
Rahisi si afueni, wakait mwingine duni,
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Mikoa twajizaini, kutawala kwa hisani,
Uhuru kuusaini, litapandisha mizani,
Ukiritimba kuwini, tutajikuta shakani,
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Utandawazi amini, mikoa huru yaghani,
Mipaka iwe laini, ya nje pia na ndani,
Na siasa kuzibuni, zisizo na walakini,
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Cha ndani hakipatikani, cha nje kiagizeni,
Soko lililo makini, linazijua kanuni,
Ukifuata mizani, hutokosa abadani,
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Mwataka ashike nani, sukari humu nchini,
Hivi kati yetu nani, utamu hauthamini,
Na hasa wa mamilioni, usoshika mikononi?
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Mbuzi ashike majani, ushahidi mashakani,
Viongozi hawaoni, au akili kichwani?
Nini wanchotumaini, kukipata ofisini?
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Ni shere yumkini, au mwatufanyia nini?
Mwahadaa watu gani, au walo afkani?
Ninacheka majinuni, hata mimi siamini
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Atashuka huku nani, aje aone ya chini,
Mwabakia ghorofani, hamjui ya ardhini,
Na uongo mwasaini, ukweli huku mwadhani,
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Kipanya haiwezekani, nyuma alishabaini,
Mwaumwa masikioni, dawa basi tafuteni?
Twajikuta hadharani, vigumu kuwatajeni,
Sukari ashike nani, utamu aache nani?

Monday, October 24, 2011

Tujengeni kwanza kwetu

MOLA twamtanguliza,kwenye familia yetu,
Jina lake ni la kwanza,kabla maombi yetu,
Naye atatuongoza,sisi na kizazi chetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!


Twamshukuru Muweza, kujali kizazi chetu,
Kwake tuzidi pendeza,kumcha tusiache katu,
Kila kitu tutaweza,hata yasiyo saizi yetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Usafi kitu cha kwanza, iwe ni ibada yetu,
Uchafu kutokomeza, usikae ndani mwetu,
Udhu kuutanguliza, hii ndiyo kazi yetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Sauti kuipaaza, nje mlangoni mwetu,
Nje tukiwa twawaza, kwenda kweye mambo yetu,
Nuru kuitanguliza, na ije nyuma yetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Nuru iwe yaangaza, juu pia chini yetu,
Machoni kuipenyeza, na masikioni mwetu,
Mdomoni kuingiza, na ikae moyoni mwetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Izinge bila kukwazwa, kuzunguka miili yetu,
Itulinde bila kusaza, hisia na viungo vyetu,
Na tusiwe tunachowaza, ila ni sifa zake tu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Elimu twaokoteza, na hii ni kinga yetu,
Muda hatujapoteza, kutumia watu wetu,
Ujinga kuumaliza, iwe bora afya yetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Mashamba hatukukuza, hayakuwa mali kwetu,
Tufanze tunachoweza, tusiige ya wenzetu,
Biashara tukiwaza, iwe na manufaa kwetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Sheria tukijifunza, tuwasaidie wenzetu,
Udaktari tukiweza, tuwatibu watu wetu,
Na yote tukiyafanza, tufanze kwa Mungu wetu,
Tujengeni kwetu kwanza, kisha tusaidie watu!

Nyumbani kwako mwenyewe

PAKA kama sio mwewe, nilivyokujadhania,
Kumbe mwenye nyumba wewe, ufanyayo nashangaa,
Ugonjwa au kiwewe, kichwani umeingia?
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?


Ni vipi ufikiriwe, na wanaokuangalia,
Mtu gani kama wewe, haijawahi tokea,
Ni yepi maruweruwe, akilini yameingia?
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?

Ni lazima uvizie, ndipo unapoingia,
Shurti uogopewe, na wote wanaokujua,
Watakudhania wewe, mwanga umekwishakua,
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?

Huna ufanyalo wewe, nanio anayeumia,
Ujinga ufanye wewe, lawama unaziktaa,
Ni nani akujali wewe,jambo usiosaidia,
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?

Tafuta radhi ya mamawe, usijifanye wajua,
Leo hii kamwangukie, na Mola atakusikia,
Sali na ukuchwe wee, bure havitakusaidia,
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?

Wamdharau mumewe, furaha utaijua?
Hajui wajua wewe, wazidi mharibia?
Nafasi upewe wewe, huna unalozingatia?
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?

Bora wenyewe wachukuwe, kidunchu kikabakia,
Nongwa kukukabidhi wewe, nje unayeangalia,
Nyumbani kwako mwenyewe, huwezi paangalia!~
Nyumbani kwako mwenyewe, wawa kama paka mwizi?

Watu hawana thamani

Watu hawana thamani

KAMA ilivyo Ulaya, sasa yazuka nyumbani,
Vitu vinaabudiwa, mtu hanayo thamani,
Mavazi usipong'aa, waonekana ni duni,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Ni ibada pia dua, vitu vilo madukani,
Na hija yakubaliwa, kwenda vileta makani,
Navyo ukipungukiwa, waonekana afkani,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Mapambo nje twajua, sio usafi wa ndani,
Hili nikiimanishia, ya rohoni na moyoni,
Nyikani tunapotea, twadhani njia twajua,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Tumetekwa Tanzania, na bepari duniani,
Wanataka sisi kua, kama walivyo Marekani,
Na uchi tutatembea, hili ninayo yakini,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Si watu wanaojijua, viongozi wetu nchini,
Waamka na kutembea, siraji hawaioni,
Tunazidi kupotea, maendeleo wadhani,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Ningelitoa usia, niseme baniyamini,
Furaha ndani yakaa, huipati mitaani,
Na havitakupatia, vitu ukijaza ndani,

Raha Allah Kumjua, si mali wala madini,
Juu, chini huja huwa, sheria ya duniani,
Kubwa, dogo huja hua, na hili nalo yakini,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Kizuri huwa kibaya,chema kukosa thamani,
Akili huja sinyaa, akiridhia Manani,
Fahari hukutumbukia, ukiipuuza dini,
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Mola nakuangukia, dunia nisithamini,
Viumbe kushikilia, hata kama maskini,
Kisha nikawasaidia, 'shara yara dharatini',
Vitu vinathaminiwa, watu hawana thamani!

Sunday, October 23, 2011

Nchi isiyoshinda

Ninawaonea gele, nchi zenye washindani,
Wasio na makelele, bali zina ushindani,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Si wazima bali mwele, twaugua akilini,
Imezimika miala, ya wa kweli ushindani,
Yamebaki makelele, tv na redioni,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Zinshanicheza chale, Yanga, Simba siamini,
Hawa ndio walewale,nje giza nuru ndani,
Kimataifa bwelele, chakula chao wageni,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Ushabiki niagule, umekufa ja moyoni,
Nafsi nikomalile, wakaya sina utani,
Ngoma sijui shinale, nikacheze kitu gani?
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Hawa si watu wanole, kupanga si yumkini,
Mambo yaenda kikole, utadhani wa zamani,
Na siasa zipalile, sangari nishabaini,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Ni nchi ya wanawale, wazaliwao njiani,
Kaulizile babale,utaambiwa yumkini,
Mwanaharamu kalole, na herufi habaini,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Ni nchi ya mashogale, wanaume siwaoni,
Mhehe ningefyale, huu ni mchezo gani,
Si filimbi si kengele, hamnao ushindani,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Neno langu lile lile, sibadiliki abadani,
Vyombo vya habari ngole, wawashinda uwanjani,
Wastahiki kilele, au kadi za kijani?
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Lelemama wafanyale, hawa si watu makini,
Hata ngoma wateule, huingia shindanoni,
Mazoezi toka kale, ndio njia ya yakini,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Na wazawa washikile, bendera kwa kila fani,
Ni makocha wateule, na walimu wa kanuni,
Hali hii wailole, na tupige abautani,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Viwanja tuezekele, mijini na vijijini,
Tuvitunze si ndulele, viwe rangi ya kijani,
Na maji tuyafosile, ghali hayapatikani,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Mipango tuipangile, sio kungoja mwakani,
KIla mchezo uvale, tarehe za ushindani,
Tusiwe ni misukule, twasukumwa viwanjani,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

Wanasiasa walole, uchumi ukiwa duni,
Na michezo hudumale, maktaimu kuauni,
Michezo haiendi mbele, nyuma hubaki yakini,
Ni nchi isiyoshinda, kila fani inashindwa!

'Taka niwe kama baba

Dekeza, dekeza baa, na rahisi kupotea,
Njiani mwana alilia, pipi wamnunulia,
Alilia motokaa, ya watu utanunua?
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Halahala msojua, kigeugeu dunia,
Chako bora ukijua, cha wengine kufubaa,
Visa watakufanyia, harabu lazima kua,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Bahati wanaopewa, akili ya kuzaliwa,
Maisha hupigania, nafasi kujipatia,
Hawana wa kutegemea, na Mungu huwasaidia,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Wamezuka Tanzania, wadekezaji twajua,
Nchi watuharibia, kwa mizoga kuchukua,
Huku wanajivunia,na wao eti wamezaa,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Kazi zao kujisifia, na ushindani kujitia,
Nyimbo watakuimbia, kama wa kwetu mkiwa,
Kaingia Romania, katokea Italia,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Na London kapitia, ili mpate kujua,
Hayo vipi yatusaidia, vijijini twajifia,
Na mahekalu wazua, shida zinakoelea,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Watu wanawahadaa, ukata kushikilia,
Eti wamechaguliwa, wao hawakuteuliwa,
Utajiri ni balaa, masikini waambiwa,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Maskini waelea, bahari ya ushujaa,
Matajiri na visiwa, vyenye ulinzi na taa,
Fukara hana mshumaa, kwa vijinga huungua,
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Kuendelea balaa, nisije kujiumbua,
Uongo sikuzoea, na ukweli mwakataa,
Uchi mnasema kavaa, sasa nini nitawaambia?
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Hawafunzwi utadhania, kazi nyingine kujua,
Kama nyani wanakaa,ya baba kuingojea,
Nani asiyechukia,kwenye nchi yenye njaa?
'Taka niwe kama baba, ndiko wanakoanzia!

Mafisadi waoanapo

Waoanapo mafisadi, mwananchi sema hapana,
Wa siasa mafisadi na wa dini kuoana,
Ni ndoa ya kuritadi, yafaa kuepukana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Taifa watalinadi, bei wakishapatana,
Mwananchi kuwa zawadi, ya wao wa nje mabwana,
Si uvumba wala uodi,uoza utaepukana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Watahurumiana kodi, maendeleo kubana,
Waje ndani bila hodi, watugeuze watwana,
Imani kuwa kuwadi, na kufa iwe kufaana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Watafanza kujinadi, michango kuchangiana,
Na sisi hatuna budi, na wao kuja achana,
Haijawa yetu jadi, madhambi kuchangiana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Tuiogopeni radi, ya Ahadi Maulana,
Hawapendi wakaidi, wajifanyao mabwana,
Hatuna budi turudi, kwake tukawa watwana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Ujibari na hasadi, kazilani Rahmana,
Ajua hao kuwarudi, kwa moto wenye laana,
Ikiwa hapana budi, duniani huwakana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Haoni haya fisadi, kaziye kusema sana,
Aghali akijinadi, aonekane muungwana,
Kumbe uoza ni jadi, na kwa mzazi ana laana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Tuepushe na kuwadi, Yaa annafi yaa rabana,
Dini zikawa abadi, huru na kwako za maana,
Kukuabudu tuhidi, na sio wengine bwana,
Mafisadi wa siasa, waoapo wa kidini!

Napenda ishi kijijini

Maisha hapa mjini, hayana lililo jema,
Naishi kwa kubaini, vijiji vingali nyuma,
Mengi hayapatikani, mahitaji wanakwama,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Ningehamia mwandani, na mi niende kulima,
Nikaishi vijijini, hewa isiyo tuhuma,
Ufugaji kubaini, kuku,bata wa hakika,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Tena yaishe kinywani, mayai yenye mashaka,
Kienyeji kusaini, mkataba wa hakika,
Maradhi ningehaini, niishi pasi dhihaka,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Matunda ningeyawini, shambani yakapandika,
NIkavuna kwa hisani, juisi kutengezeka,
Upepo wa bustani, unipe kupumzika,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Ningeepuka uhuni, pikipiki kuepuka,
Bajaji kuacha tauni, kelele kutosikika,
Daladala za kihuni, nazo hazitosikika,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Kawaambie madiwani, huduma wakiipeleka,
Maji yawe kijijini, mjini ninaondoka,
Sioni sababu gani, mjini kujateseka,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Mbunge naye abaini, hapa ninalazimika,
Ninabakia mjini, umeme nami shirika,
Kazi zangu si auni, bilao hazitafanyika,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Umeme wa kijijini, siku utakapowaka,
Nitaondoka mjini, niende kushereheka,
Pasiwe abautani, tena kwa mingi miaka,
Ningeishi kijijini, zingekuwepo huduma.

Mwanademokrasia

Haogopi kuchukiwa, mwanademokrasia,
Kazi yake aijua,dhuluma huzikataa,
Dhulumati humuhadaa,Kama wao kujakua,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Na asipowakubalia, huanza kumchukia,
Watamfanyia nazaa, kumzushia balaa,
Hata sumu huwekewa, uendelee ubaya,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Siasa za kuhofia, wengi wau wana njaa,
Wengine wamebobea, matumbo yanavujia,
Hayawezekani kujaa, kila siku hupungua,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Uchama naukataa, naijenga Tanzania,
Upande kutoegemea,ila demokrasia,
Nchi ipate kufaa,sio takataka kua,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Nani kunisogelea, uongo naukataa,
Usanii nachukia, na dhuluma naijua,
Haki ninaililia, kila mtu Tanzania,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Mapambano yaendelea, sasa uchumi hatua,
Umaskini kuuvua, huru kiuchumi kua,
Ikashindana mikoa, uchumi kuunyanyua,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Siasa za kimatonya, mwisho sasa zafikia,
Chaja kizazi kipya, nchi kujaisimamia,
Nyuma wanaongalia, hapo hapo kubakia,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Kazi nimeshairidhia, siwezi kuikataa,
Kuenzi demokrasia, hadi mizizi kukomaa,
Daima nitatetea, hadi kaburini kwingia,
Mwanademokrasia, haogopi kuchukiwa.

Sauti itasikika

Hadi ng'ambo kaburini, sauti itajafika,
Sauti hawatahini, leo wanaosifika,
Utazimika ubani, na marashi kutoweka,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Haki wanaoamini, ni watu wa kuteseka,
Ila kilicho moyoni, daima huwapeleka,
Binadamu si Manani, hilo wana uhakika,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Huwajua wazaini, na yanayokujakuwafika,
Ukweli walishabaini, si rahisi kutumika,
Mkataba huughani, hakuna vuka mipaka,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Wababe wanaodhani, waweza kunyamazika,
Hukuta ni mtihani, usiowezekanika,
Kufaulu hubaini, kwao huwa ni mashaka,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Waondoke duniani, bado sauti hufika,
Mizuka na maruhani, vuguvugu hulidaka,
Wakawa ni mashakani, hadi kifo kuwafika,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Hili ninaliamini, watazame wahusika,
Kusi hadi kaskazini hapa kwetu Afrika,
Viongozi mashetani, Mola anawamulika,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Si watu wa kuamini, vyeo kwao huabudika,
Ni vipofu duniani, moto wao wanapika,
Sio bora, watu duni,watakujabainika,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Isiwe yako idhini, wangu Rahimu Rabuka,
Kuniweka duniani, dhuluma ikafanyika,
Niepushe mitihani, nisije kudanganyika,
Sauti itasikika, hadi ng'ambo kaburini.

Fisadi mvunja nchi

Hafai kuvumiliwa, fisadi hana rafiki,
Ubinafsi kajaa, vyote hutaka milki,
Mtaji hujipatia, kwa njia zisizo haki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Kunyonga keshazoea, kuchinja hayumkiniki,
Za mkato kupitia, hizo njia amiliki,
Huwezi mtegemea, ni mkubwa mnafiki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Ajua kuwatumia, bila malipo ya haki,
Mawazo huyachukua, akidai hayataki,
Kisha huja kutumia, kwa kuiba hatimilki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Wakubwa huwahadaa, kama binti na Fataki,
Ajua kuwasifia, magharibi, mashariki,
Wakajiona wajua, kumbe bure mamluki,

Ni mabuzi atumia, kuwachuna pasi breki,
Na anavyozitumia, Mangi atamtaliki,
Hisia hufa kifua, ukubwa kutamalaki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Mbumbumbu wangelikuwa, utadhani mabruki,
Si watu wa kuaminiwa, kawalaani Maliki,
Pepo hujitangazia, dunia itawashtaki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Akili hawajatulia, utadhani mashabiki,
Huishi kwa kubabia,kwa dhuluma za riziki,
Muhali kuhesabiwa, kwani hawajumliki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Kama ningeliwatambua, nawafanza mshikaki,
Wazi ningewachambua, niwachome kwa hamaki,
Wananchi kuwagawia,wale na wanywe na wiski,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Wanaojichukulia, taifa isivyo haki,
Kujimilikisha dia, nchi kuwa yao milki,
Wakawa waitumbua, mwananchi wamdhihaki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Ardhi tunayokalia, hii ni ya kwetu haki,
Iweje kutuvamia, mkawa wastahiki,
Malipo kuyachukua, sisi tupu tukabaki?
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Macho tumefunguliwa, tutaipigania haki,
Wawekezaji kujua, ardhi haikaliki,
Chetu tusipokujapewa, na hisa nazo kumiliki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Tumechoka hadaiwa, hapa tena hatwondoki,
Dhahabu tutafukia, hadi malipo ya haki,
Ufukara twakataa, kijiji hakistahiki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Kila atakeyingia, utajiri tutalaki,
Serikali kutwibia, katu haikubaliki,
Ni sisi tuliokaa, kijijini twastahiki,
Fisadi hana rafiki, na hafai vumiliwa.

Mbumbumbu wa Teknohama

Mbumbumbu wa teknohama, wasipewe uongozi,
Hao sawa na vilema, kujihimu kwao kazi,
Wanaongeza gharama, za maisha pia kazi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Ya jana hawakusoma, wayashangaa ya juzi,
Wameghairi ulama, na hawajiendelezi,
Wazidi kubaki nyuma, dunia ya utandawazi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Ni wafanyabiashara, wameshika maongozi,
Mkongo umetuama, sababu ya shinikizi,
Wanasiasa daima, nyuma kama madoezi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Hawa wetu maamuma, hawaijui ngamizi,
Kompyuta walalama, imewashinda ujuzi,
Ustawi na salama, mashakani tumaizi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Kiongozi kumtema, kama aleta ajizi,
Kuidaka na kusoma, teknohama kwa mapenzi,
Na kisha kuisukuma, tufanze mapandikizi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Serikali imekwama, mikoani ni uchizi,
Wavuti zimesimama, kisa pesa na malezi,
NI mengi yamesamama, maendeleo na kazi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Ingepaa teknohama, sisi si Rwanda wazuzi,
Mashariki ingetetema, kwa vyuo na maandalizi,
Wanafunzi wangehama, mamia wakapata kazi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Bungeni kuna tuhuma, ni wapinzani wajuzi,
Kulala wanawasakama, hao kinamapinduzi,
Huropoka si kusema, na tafiti si wajuzi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Wengine ni kinamama, vyeo kwao fumanizi,
Kwa za uongo tuhuma, leo wamepewa kazi,
Hivi ndivyo tulivyo nyuma, kujivua hatuwezi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Sitini ikisimama, ni vigumu ugunduzi,
Ila walo na karama, awapendao Mwenyezi,
Arobaini ya heshima, kuwa wetu kiongozi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Kwa busara na hekima, arobaini yakidhi,
Asizidi kuegema, bado awe mvumbuzi,
Abuni yenye neema, yatokee mageuzi,
Mbumbumbu wa Teknohama, wasipewe uongozi!!

Vijana msigawanyike

Msigawinyike vijana, kitaifa msigawike,
Itakuwa ni laana, ya wazee wawatwike,
Yakwao wao ya jana, mbeleko sasa tweleke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Wakati wao ujana, kwa uhuru utumike,
Katu hawakubaguana, mkoloni aondoke,
Wazawa kuaminiana, ilibidi lifanyike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Uhuru ulipatikana, bendera ipeperuke,
Ilibidi kushikana, Mwingereza ang'atuke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Leo tunayoyanena, uchumi uimarike,
Lazima kupatikana, uchumi uhuru wake,
Nasi tusipoungana, ni vigumu lifanyike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Wazee wajanja sana, wataka tugawanyike,
Ili wahodhi ubwana, na sisi tudhalilike,
Wengine hawana wana, na ukubwa ndio mke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Muamana wa kupona, nchi dia waiweke,
Miaka tena hawana, kwanini wasononeke?
Mtakaopotezana, ni nyie mzainike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Baraza haraka sana, lazima sasa lizuke,
Kuunganisha vijana, na kila chama watoke,
Dira na yetu amana, nchi sasa ijengeke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Mafisadi kuwabana, na wazee waondoke,
Hakuna kubabaishana, budi uchumi uumuke,
Na sote kuhimizana, maarifa yatumike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Bidii kuchagizana, na juhudi ifanyike,
Na wengine kutafutana, vijana mshikemshike,
Amerika na Uchina, mambo bora yapangike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Seychelles na Guyana, Brazili tuwashike,
India na Botswana, mifano tukaiteke,
Russia mpaka Ghana, mbinu twige tuchangamke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Iwe ni mwiko vijana, na wazee mtumike,
Ili wao kugawana, nyara ovu wazisake,
Ni sharti kuwabana, sasa wasambaratike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Chama mjue ni jina, linaweza lifutike,
Kulikoni kuja uana, vingine budi tuzike,
Umoja wetu amana, amani sote tutake,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Watanzania kuibiana, lazima tupige teke,
Hiki chanzo cha hazina, kwa mabaya yafanyike,
Ikawa twapatilizana, taifa liserereke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Ili sote kuungana, maandamano tukoke,
Wazee kuja wabana, fungamano lifanyike,
Na kiapo kuapizana,vijana wasitumike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Na kiapo kuapizana, vijana wasitumike,
Kuja sisi kutugawanya, na vita vije vizuke,
Kwa nia njema kuagana, nchi wenyewe tushike,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Namshukuru Rabana, umoja ausimike,
Na usiku na mchana, mipaka yetu ilindike,
Na uchumi kufaana, wote juu tunyanyuke,
Vijana msigawike, kuweni kitu kimoja.

Thursday, October 20, 2011

Waachie njia nyeupe

KABLA hujamalizia, hujifanya wanajua,
Maamuzi kuamua, nusu yasiyofikia,
Matokeo yake huwa, kama tunavyoyajua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Fahamu si kusikia, yataka kuyaelewa,
Kuona na kuambiwa, haviwezi kuwa sawa,
Hujua unachojua, pia usichokijua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Afanzaye kwa kusikia, naye ni kama mbeya,
Husema asilojua, kama vile anajua,
Na hili wapaswa jua, binadamu kajaliwa,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Mijini wanavyoingia, au wanapoajiriwa,
Vyeo wakifumania, hujisikia wajua,
Lakini hapana mjua, ila yule anayejua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Lataka kunyenyekea, hujui upate jua,
Si budi kutangazia, wengine watahadithia,
Ukimya huongea, na wengi hili wajua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Wapole wanaojua, kelele huzikataa,
Polepole huongea, taahira utadhania,
Ila huyapangilia, ujue usichokijua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Wajifanyao wajua, maneno huyadakia,
Maana hawajaelewa, waanza kuelezea,
Na katikati ya njia, hujikuta hawajajua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Wepesi wa kutangulia, wengine kusimulia,
Mji hawajaingia, ramani hukuelezea,
Nchi wanaisikia, kufika watakwambia,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Mtu hawajamjua, watasema wamjua,
Na sifa kumsifia, au huja muumbua,
Uongo kumzulia, ukweli ukadhania,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Waepuke watu hawa, acha nao kutembea,
Ogopa kuwasikia, dhambi utajichumia,
Na mtu mwenye staha, marafiki huchagua,
Wajifanyao wajua, waachie nyeupe njia.

Hutusaidii kitu

Kitu hutusaidii, tukwitaje kiongozi,
Twaona ni usanii, mbunge hauna kazi,
Jimbo bado asubuhi, twataka mchapakazi,
Hutusaidii kitu, tukwitaje kiongozi?

Uzawa hausaidii, jimbo lataka malezi,
Ufukara twakinai, yafanyike maamuzi,
Fursa hatutumii, au hili huliwazi,
Hutusaidii kitu, tukwitaje kiongozi?

Maiti mtu hatufai, sawa nfu kiongozi,
Ambaye kura adai, na maendeleo hawazi,
Ningeshaitoa rai, leo kumfukuza kazi,
Hutusaidii kitu, tukwitaje kiongozi?

Miaka mitano nishai, kuwa naye kiongozi,
Leo kama hatufai, aachie papo ngazi,
Chakula ukikinai, kuacha isiwe kazi,
Hutusaidii kitu, tukwitaje kiongozi?

Ni miaka hamsini

Umeme uko ndotoni, maji wala siyaoni,
Wanambia hamsini, nifurahi kitu gani,
Mbavu za mbwa uwani, makazi yangu anwani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Sina thamni nchini, sithaminiwi duniani,
Heri nakaa mjini, wakoje wa vijijini?
Twafanyiana utani, haya wala hamuoni?
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Mboga yangu mgagani, utadhani klorokwini,
Bada yangu dizaini, nasaga mwangu nyumbani,
Lishe yangu majinuni, kaniruzuki Manani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Nikenda hospitalini, nichange kitu gani,
Najitibia nyikani, mwezi shilingi sioni,
Roho naweka rehani, wala hamjabaini,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Niwalishe kitu gani, waendao skulini,
Utapiamlo kichwani, watafaulu somo gani,
Mlio madarakani, hebu shukeni chini,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Wachina siamini, watupita kitu gani,
Ni kwenye mwaka sitini, wote tukiwa maskini,
Nasikia redioni, leo wanayo thamani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Malaysia nchi gani, na Korea kusini,
Tulipokuwa vitani, kulikuwa ni nyikani,
Wao nini wamebaini, watuacha maskini?
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Mtunzi nakuamini, kuyaweka shairini,
Ufikishe shaurini, sifurahii kwanini,
Waelewe yumkini, nchi ina mitihani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Ni miaka hamsini

Umeme uko ndotoni, maji wala siyaoni,
Wanambia hamsini, nifurahi kitu gani,
Mbavu za mbwa uwani, makazi yangu anwani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Sina thamni nchini, sithaminiwi duniani,
Heri nakaa mjini, wakoje wa vijijini?
Twafanyiana utani, haya wala hamuoni?
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Mboga yangu mgagani, utadhani klorokwini,
Bada yangu dizaini, nasaga mwangu nyumbani,
Lishe yangu majinuni, kaniruzuki Manani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Nikenda hospitalini, nichange kitu gani,
Najitibia nyikani, mwezi shilingi sioni,
Roho naweka rehani, wala hamjabaini,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Niwalishe kitu gani, waendao skulini,
Utapiamlo kichwani, watafaulu somo gani,
Mlio madarakani, hebu shukeni chini,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Wachina siamini, watupita kitu gani,
Ni kwenye mwaka sitini, wote tukiwa maskini,
Nasikia redioni, leo wanayo thamani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Malaysia nchi gani, na Korea kusini,
Tulipokuwa vitani, kulikuwa ni nyikani,
Wao nini wamebaini, watuacha maskini?
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Mtunzi nakuamini, kuyaweka shairini,
Ufikishe shaurini, sifurahii kwanini,
Waelewe yumkini, nchi ina mitihani,
Ni miaka hamsini, ndiyo nifurahi nini?

Mambo yakishakushinda

Mlango kama si wazi, usifosi kuingia,
Kuna mingine iwazi, jaribisha kupitia,
Kuelewa hili kazi, subira sio tabia,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Usije ichuna ngozi, na mkono kuumia,
Usishikwe kikohozi, kwa hodi kung'ang'ania,
Umefungwa hauwezi, kwingine sasa pitia,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Kibaya king'ang'anizi, riziki huja potea,
Unakuwa ni dumizi, pale pale kulilia,
Hayasaidii machozi, mlango hayotofungua,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Vipindi ni angalizi, na nadra kutimia,
Ikiwa hauyawezi, yanini kujagombea,
Kiinimacho mbalamwezi, hajui asiyeyajua,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Usimngoje mtenzi, jambo kuja kukutendea,
Na usiipande ngazi, kushuka unapotakiwa,
Kitumbua si andazi, ashakum ni staha,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Mvua za kiangazi, sio za matumaini,
Wapo wa nyumba wajenzi, vigumu kuishi ndani,
Moyo nauacha wazi, anabaini Matini,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Shairi nimedarizi, hekima kuibaini,
Natumai uongozi, watoka kwako Bathini,
Nipandishe hii ngazi, nikakae ghorofani,
Mambo yakishakushinda, acha, kubali yaishe!

Milioni hamsini

Ninahoji maamuzi, siasa sizibaini,
Twakosaje viongozi, na sisi mamilioni,
Wananiambia wajuzi, milioni hamsini,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Naona kuna ajizi, sababu mimi sioni,
Kuchagua sio kazi, penye siasa makini,
Pasipo na kura wizi, na haki tukithamini,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Njaa ni yetu maradhi, yazidisha umaskini,
Tunachagua viazi, watu hatuwathamini,
Tunaokota nazi, akili zisizobaini,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Au pengine Azizi, katuona maaluni,
Katuachia kizazi, kupata waso makini,
Ife miji na kamazi, hadi warithi wageni,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Sijapata ufumbuzi, najiona majinuni,
Wakulima na wakwezi, kuongozwa na wahuni,
Mliwapatiaje kazi, watu wasiowathamini?
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Zimezagaa mbaazi, shambani pia njiani,
Huokota mabazazi, mashuzi nani atamani,
Kweli hapana wajenzi,miti iliposakini,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Tumkurubie Hafizi, ambaye wetu Manani,
Atufanyie majazi, wepesi wa mitihani,
Nchi yataka ujenzi, kuondoa umaskini,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Nchi yataka ujenzi, kuondoa umaskini,
Atupe wake ujuzi, tuweze kuwa makini,
Tupatilize washenzi, na wafanyao utani,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Ah, Yaghaniyu, Ya Mani, sitatul tuiimaizi,
Tusijikwae njiani, twataka bora makazi,
Firdausi kwetu shani, ustadhi na wanafunzi,
Twakosaje viongozi, milioni hamsini?

Nabii wajisimika

Nabii leo wazuka, wenyewe wajisimika,
Muumba wamemkwepa,wamejipa madaraka,
Sijui akikasirika, ni wapi watamwepuka,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Magazeti yaandika, redio zinasikika,
Televisheni kuzuka, ndio zinathaminika,
Ndio waliookoka, nao kwao utaokoka,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Nasikia kwa hakika, waliotokota hufika,
Na hawa wanaosifika, wapo wanaokujashuka,
Hupati unalotaka, hupewa utakaloshika,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Miujiza watajika, mengine hutia shaka,
Sarakasi ukifika, utadhani yafanyika,
Dunia hii kufufuka, sijui wanakotoka,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Maisha yakichemka, manabii hujazuka,
Wa namna hii hakika, wakati wao wafika,
Na ukiwa mshirika,huenda yakakufika,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Nchi hii Tanganyika, sio kwanza wanazuka,
Waja, kisha kutoweka, vizazi husahaulika,
Maisha kuteremka,rahisi si kupandika,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Umetaka hukutaka, wakija wanaozuka,
Ukipenda utaanguka, usipopenda utashuka,
Akili za Kiafrika, kaeni mzipe mwafaka,
Nabii wajisimika, Mungu-mtu sasa aja!

Mnafiki

ZABIBU kumbwaga chini, sungura kasema mbichi,
Waona ajabu gani, kusema kichwa kibichi,
Kwani wao watu gani, bali za shamba kabichi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Yanga, simba uwanjani, atasema mshindwa mechi,
Kwa aliye taabani, tuhuma hawaifichi,
Binadamu mbaini, tabia humweka uchi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Na msemwa haamini, na kauli hachekechi,
Mbovu na puya zi ndani, mtalishwa wali mbichi,
Kisingizio kitu gani, nani kawafundisha nachi?
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Jumbe niache makani, na polisi wasinisachi,
Kaniudhi majinuni, kaiba zangu chikichi,
Kanifanyia uhuni, si wake mchikichi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Watazame limbukeni, akikaa kwenye kochi,
Raha akiibaini, usingizi haumwachi,
Kazi kumtoa ndani, TV ikiwa na mechi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Miaka nimesaini, si ya kwangu hii nchi,
Wenyewe ni lalwamani, apendwa bora Mdachi,
Mweusi alwatani, mkoloni nusu-uchi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Na walio mashakani, chuki zao hawafichi,
Utapandaje paani, ngazi uipige tanchi,
Juha nakaa tawini, kwanguka chini siwachi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Katwaa kinu uwani, kauacha ndani mchi,
Utatwanga na nini, au ni mzee wa panchi?
Ufanyalo siamini, utaacha kuwa kuchi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Kama u mtu makini, tulia utunze ranchi,
Na wakija kijijini, wajukuu wape pochi,
Mjini sasa nyikani, na kwako kucha haukuchi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Mshairi masikini, mbivu siiti mbichi,
Ukweli nilishabaini,haukuwa nusu uchi,
Bayana niliamini, kufika kipindi hichi,
Mnafiki twamjua, sungura kasema mbichi!

Mkosaji

Mbona kwake kawaida, mkosaji kupayuka,
Hii ni mila na ada, labda haijaeleweka,
Na ingelikuwa bida, tamaa isingejengeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Ni jambo la kawaida, mkosaji kupayuka,
Vitisho kwake kaida, mipaka hajaivuka,
Na kiada na ziada,
huagiza akitaka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kupayuka ni ibada, jua hilo kwa hakika,
Hata akienda eda, mengine hulalamika,
Utadhani kama buda, lakini aeleweka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kwake lisilo faida, manufaa hugeuka,
Na kileo akigida, maafa yakamfika,
Bado huwa kama nunda, kulalama kalogeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Watu wengine ni shida, hupati pa kuwaweka,
Hujichanganya mada, wakashindwa eleweka,
Ponda kugeuzwa poda,ni kipi utakachoshika?
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Mkosaji

Mbona kwake kawaida, mkosaji kupayuka,
Hii ni mila na ada, labda haijaeleweka,
Na ingelikuwa bida, tamaa isingejengeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Ni jambo la kawaida, mkosaji kupayuka,
Vitisho kwake kaida, mipaka hajaivuka,
Na kiada na ziada,
huagiza akitaka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kupayuka ni ibada, jua hilo kwa hakika,
Hata akienda eda, mengine hulalamika,
Utadhani kama buda, lakini aeleweka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kwake lisilo faida, manufaa hugeuka,
Na kileo akigida, maafa yakamfika,
Bado huwa kama nunda, kulalama kalogeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Watu wengine ni shida, hupati pa kuwaweka,
Hujichanganya mada, wakashindwa eleweka,
Ponda kugeuzwa poda,ni kipi utakachoshika?
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Mkosaji

Mbona kwake kawaida, mkosaji kupayuka,
Hii ni mila na ada, labda haijaeleweka,
Na ingelikuwa bida, tamaa isingejengeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Ni jambo la kawaida, mkosaji kupayuka,
Vitisho kwake kaida, mipaka hajaivuka,
Na kiada na ziada,
huagiza akitaka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kupayuka ni ibada, jua hilo kwa hakika,
Hata akienda eda, mengine hulalamika,
Utadhani kama buda, lakini aeleweka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kwake lisilo faida, manufaa hugeuka,
Na kileo akigida, maafa yakamfika,
Bado huwa kama nunda, kulalama kalogeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Watu wengine ni shida, hupati pa kuwaweka,
Hujichanganya mada, wakashindwa eleweka,
Ponda kugeuzwa poda,ni kipi utakachoshika?
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Mkosaji

Mbona kwake kawaida, mkosaji kupayuka,
Hii ni mila na ada, labda haijaeleweka,
Na ingelikuwa bida, tamaa isingejengeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Ni jambo la kawaida, mkosaji kupayuka,
Vitisho kwake kaida, mipaka hajaivuka,
Na kiada na ziada,
huagiza akitaka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kupayuka ni ibada, jua hilo kwa hakika,
Hata akienda eda, mengine hulalamika,
Utadhani kama buda, lakini aeleweka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kwake lisilo faida, manufaa hugeuka,
Na kileo akigida, maafa yakamfika,
Bado huwa kama nunda, kulalama kalogeka,
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Watu wengine ni shida, hupati pa kuwaweka,
Hujichanganya mada, wakashindwa eleweka,
Ponda kugeuzwa poda,ni kipi utakachoshika?
Mkosaji kupayuka, ni jambo la kawaida.

Kuropoka majaliwa

Kuropoka majaliwa, umakini wasojua,
Na hapo ndipo hutua, lisilofutika doa,
Mtu hujashangaa, tatizo kutolijua,
Kuropoka majaliwa, majuto ni mjukuu!

Dhahabu huitwa ukimya, kwa wale wanaojua,
Kinywa usipokifungua, ni mengi utayaambaa,
Ukijifanya wajua, na wengine huwa hua!
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Waache wanaoongea, waongee wasojua,
Wewe uliyekomaa, hekima kuzingatia,
Eti hebu fikiria, neno shilingi lingekuwa?
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Busara ni kunyamaa, vito kujikusanyia,
Onekana hujajua, lakini yote wajua,
Hili ukilizingatia, dunia utaijua,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Utakiwapo kutia, neno ndipo unapotia,
Hakuna kitakachopungua, kimya ukijikalia,
Ucheshi si kuongea, bali pia kutoongea,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Maneno huwa balaa, wambeya wanapojaa,
Dogo kubwa hujakua, hata kimo kuzidia,
Mengine kuvumilia, kazi kubwa kujakuwa,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Mshairi naongea, tokana na mazoea,
Viumbe ninawajua, wewe bado kuwajua,
Nafsi kutumikia, ndicho wanachokijua,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Kuropoka majaliwa

Kuropoka majaliwa, umakini wasojua,
Na hapo ndipo hutua, lisilofutika doa,
Mtu hujashangaa, tatizo kutolijua,
Kuropoka majaliwa, majuto ni mjukuu!

Dhahabu huitwa ukimya, kwa wale wanaojua,
Kinywa usipokifungua, ni mengi utayaambaa,
Ukijifanya wajua, na wengine huwa hua!
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Waache wanaoongea, waongee wasojua,
Wewe uliyekomaa, hekima kuzingatia,
Eti hebu fikiria, neno shilingi lingekuwa?
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Busara ni kunyamaa, vito kujikusanyia,
Onekana hujajua, lakini yote wajua,
Hili ukilizingatia, dunia utaijua,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Utakiwapo kutia, neno ndipo unapotia,
Hakuna kitakachopungua, kimya ukijikalia,
Ucheshi si kuongea, bali pia kutoongea,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Maneno huwa balaa, wambeya wanapojaa,
Dogo kubwa hujakua, hata kimo kuzidia,
Mengine kuvumilia, kazi kubwa kujakuwa,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Mshairi naongea, tokana na mazoea,
Viumbe ninawajua, wewe bado kuwajua,
Nafsi kutumikia, ndicho wanachokijua,
Kuropoka majaliwa,majuto ni mjukuu!

Uzuri na Ubaya

HALI ya hewa yacheza, binadamu aicheza,
Shere anaifanyiza, ya mbele bado kuwaza,
Mwenyewe ajidumaza, adhani yeye akwazwa,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Dunia twaigeuza, wazuri wajitembeza,
Hali wabaya wajiuza, ninabaki kuuliza,
Haya tukishamaliza, ni mangapi twabakiza?
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Thamani umechuuza, uzuri wajitembeza,
Kila mtu wamtatiza, japo mate ayameza,
Gharama hatoiweza, na mchuuzi huchuuzwa,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Kibaya kinajiuza, dunia ya miujiza,
Na bei hujiongeza, kila kinakopitiza,
Wanunuzi wakimbiza, kupata hawajaweza,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Uzuri wabembeleza, na watu wanauiza,
Baba anatukataza, na mama anaapiza,
Shangazi naye abeza, mjomba anagombeza,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Uzuri umejichakaza, thamani umeipoeza,
Nuru imekuwa giza, imebaki kuomboleza,
Maradhi ukiingiza, huna utakachobakiza,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Dunia yatuduwaza, kizuri kujitembeza,
Ni nani wameukwaza, chini sasa wajiburuza,
Na swali, je, unaweza, kuja tena kujiuza?
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Sala inayopendeza, Mushawari kuhimiza,
Ajua kutengeneza, aali visivyojitembeza,
Naye ukimbembeleza,atakujazia chaza,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Kazi nimeimaliza, malenga nawaagiza,
Fanyeni kupeleleza, siri hii kuchunguza,
Huu mkubwa muujiza, haufai kupuuza,
Uzuri wajitembeza, ubaya unajiuza.

Mjivuni

Njia yake haikwepi, hayo yake majaliwa,
Kama refu au fupi, lazima kufuatilia,
Aendako kama kupi, yeye mwenyewe ajua,
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Mbegu hugeuka kapi, kwa anachojivunia,
Maisha yake mafupi, binadamu hajajua,
Hata kama haogopi, hushtuka kulijua,
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Kikusikitishacho kipi, laiti ungenambia,
Ningekupatia pipi, mpenzi uache kulia,
Haijapo hunenepi, sharti utafurahia,
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Huruma yangu upapi, mengi nimevumilia,
Bado wajifanya chupi, lazima kujavuliwa,
Uendako huko kupi, umeshindwa kuyajua,
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Walishashindwa wangapi, wewe unang'ang'ania,
Kikukondeshacho kipi, kama si ya kujitakia,
Furaha yako iwapi, nje ukiifuatilia?
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Nimekuonea lipi, kama si kujitakia,
Mimi na wewe wapi, tulipokujakosania?
Nimekutenda mangapi, na haukunisaidia?
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Kiburi sawa na nepi, mtu mzima kuvaa,
Nikufungue kwa vipi, macho ujue dunia?
Unakokwenda ni kupi, kusikokujajutia?
Mjivuni njia fupi, na huona kaonewa.

Wednesday, October 19, 2011

Waandishi wa habari

Muamana hupotea, kama kufa na maisha,
Mwandishi akiolewa, na wakubwa wakumtisha,
Kazi yake hujifia, maiti ende kuosha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!


Rwanda kilichotokea, waandishi walizusha,
Njia mnayoelekea, huko mtakujatufikisha,
Halahala nawaambia, damu hamwezi iosha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Kila mtu ana njaa, wao sasa wazidisha,
Tumbo linawatumbukia, wana kifafa cha kuangusha,
Senti wakishapewa, waka'nga bila kuosha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Wahariri nahofia, hakuna wa kuwawajibisha,
Habari wanazitoa, mwandishi kaziegesha,
Upande zinalalia, akishapokea rushwa,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Yanini unazitoa, na gazeti kuchapisha,
Kidole hukunyookea, na hili linasikitisha,
Inafaa kupakuliwa, upya mwende kuoshwa,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Mauzo yanavyopungua, uongo ndio wazusha,
Uhuru wanaulilia, wa uongo kutupasha,
Jukumu mlilopewa, ndilo mnalotufundisha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!


Mwapika na kupakua, siasa za kupotosha,
Uchumi mnategemea, nani wa kuja unyoosha,
Kazi yenu mmekalia, umbeya na rasharasha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Juu nyie mwatakiwa, wanasiasa kuwapasha,
Wajibu kuwazindua, wasifanze ya kuchusha,
Nchi ipate endelea, kwenye dhiki kutuvusha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Wenye mali nawaambia, haya nyie mmezusha,
Wazee kuwaondoa, vijana mkawapandisha,
Busara imepotea, nyuzirumu zinaisha,
Mkiishanunuliwa, nani atatuwezesha,

Wazee wanatakiwa, ujinga kusimamisha,
Hekima wakaigawa, miiko kusimamisha,
Wale wanaochaguliwa, njaa kutowatingisha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Heshima najivunia, warithi wasikitisha,
Uzaini wahadaa, wafanya yanayochosha,
Nani wa kuwasaidia, kuyatakasa maisha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Mashehe nawausia, waandishi kuwapasha,
Dini yao kuijua, na moto kuwaepusha,
Dhamana yao ulua, dhambi nyingi kubebeshwa,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Watakiwa kuongoa, na sio kufarakisha,
Watakiwa kushuhudia, na sio kujakanusha,
Wahesabiwa wadaiwa, umma wanapoupotosha,
Mwandishi akiolewa na wanasiasa kesha!

Elimu bila kisomo

Kasomeshwa Uingereza, mtoto wa Mfalme,
Swaziland naiwaza, si Switzerland dume,
Miaka kaipoteza, ilisha kama umeme,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!


Kafaulu Kiingereza, na kujifanya mtume,
Kadhalika ameweza, kuwa wa wake wengi mume,
Uchumi kauupuza, nchi yafa kwa ukame,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Selemani atamweza, ni kwa vipi ajitume,
Nabii aliyaweza, kwa kuupata utume,
Mwenyezi alichoagiza, hakwenda nacho kinyume,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Shaka alishaongoza, akafanya ya kiume,
Dola aliisambaza, ufalme usimame,
Uzulu hakuidumaza, acha vibaraka waseme,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Ukimwi unaunguza, kulia hadi kuume,
Nchi inakuwa giza, mpaka wa nje waseme,
Afrika inaiza, vipofu wetu madume,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Uongozi ninawaza, tuwatume watutume?
Na mambo wanayofanza,hata wangekuwa watume,
Kuwavumilia twakwazwa,au huu mfumo dume?
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Kuongoza si kucheza, wanawake, wanaume,
Nchi kuiendeleza, hili kwalo msikwame,
Nafasi mkipotza, ni budi nasi tugome,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Hatuwapi kuongoza, ili nyie mjinome,
Sisi mnatupuuza, ni lazima tulalame,
Hasira zikipaaza, mtakuwa pakashume,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Tanzania naapiza, tabia mbaya msome,
Watu wao wanaokwaza, urafiki nao mkome,
Wanaizaya kuiza, nchi zisiwe mahame,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Ni lazima kuongoza, kwa mifano ya mitume,
Wabaya kupatiliza, Mola kazi atutume,
Wazungu kujigeuza, haifai tuwateme,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Na desturi za giza, ni lazima tuzichome,
Kila mtu anaweza, kuzaa jike na dume,
Balaa twazisogeza, twalaniwa na mitume,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Tuondoke kwenye giza, watu pumzi waheme,
Anasa kuzipuuza, wacheni watukoromee,
Ukweli naueleza, vinginevyo msiseme,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Hali inatutatiza, nchi zetu ni ukame,
Bei zinatuunguza, wanawake kwa waume,
Nyie bado mwatuteza, sasa wapi tukaseme?
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Mapinduzi twahimiza, wake na wanaume,
Afrika kuuguza, njaa, dhiki na ukame,
Ufukara watukwaza, viongozi si madume,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Vijana tutawaponza, waje watumie sime,
Nchi zinavyozidi oza, hakuna mswalie mtume,
Haya tuache puuza, sisi sote tujitume,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Tujitume kuongoza, tusiwe mapaka shume,
Maisha kuyapooza, tusigeuke magome,
Hatari kupatiliza,na amani isikome,
Elimu kwa Mfalme, haikubadili kitu!

Ustawi wa Jamii

Ustawi wa jamii, wallahi kama yatima,
Mie ninatoa rai, tufanyavyo sio vyema,
Kama hatufikirii, basi si watu wazima,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.



Fukara idara hii, siku zote iko nyuma,
Hupachikwa kwa nanihii, na hii ni kubwa dhuluma,
Sasa tumeyakinai, twataka wizara nzima,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.


Ni kubwa sana jamii, hili lataka hekima,
Jambo la kutanabahi, muhimu kuipa dhima,
Iweze kutustahi, kwa nyenzo pia huruma,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Wazee twaitumai, kuzipunguza dhuluma,
Endapo tukiwa hai, tusiwe zigo kwa umma,
Uzeeni kutustahi, tufe na yetu heshima,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Jamii haifurahi, kuteseka kwa vilema,
Majina ni usanii, tutakalo yenye hima,
Kuwanyaapa nishai, hawa ni wana wa umma,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Wakithiri majeruhi, waso baba au mama,
Twawanadi kisanii, majina ya takrima,
Watoto wa mitaani, huku bado wanakwama,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Wajane nao wadai, tutunze yao heshima,
Wizara iwastahi,tusiache ya karama,
Nao wapate furahi, kwa kutunzwa nao umma,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Masikini wazirai, kwa dhiki, njaa na homa,
Ustawi wa jamii, hawaoni wake wema,
Mchango wanaudai, serikali fanya hima,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Watoto watundu nai, kote wanavyorindima,
Jela zao hazifai, zinazo nyingi tuhuma,
Kuwaokoa sijui, kama tunayo neema,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Vijana hatuwatumii, JKT wanasema,
Waweza faa jamii, nao kujifunza dhima,
Ajira wazisabahi, kila wakifanya vyema,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Afya shughuli hii, iwe peke yasimama,
Upacha hautufai, upande unaegema,
Rais pokea rai, kwa heshima na taadhima,
Ustawi wa Jamii, unahitaji wizara.

Tuesday, October 18, 2011

Mo Ibrahim

Kama kasi ndio hii, kuipata tunzo kazi,
Tuamke asubuhi, kuifanza fumanizi,
Mipango tuisanii, na mikakati kuenzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.


Nchi yetu majeruhi, siasa zenye vitanzi,
Mitego twaikinai, wamezidi viongozi,
Ujanja mtu kuwahi, na wachache wa vitenzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Matatizo hatujui, kwisha hupanda ngazi,
Pia rushwa haifai, hutia jicho kibanzi,
Na waudhi usanii, hata pia kwa Mwenyezi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Matatizo tukinai, kama wizi na ujambazi,
Haki hatuitumii, dhuluma tunaienzi,
Vijiji tuvistahi, vipate bora majenzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Fursa tuzisabahi, za kiuchumi kumaizi,
Watu hamasa wadai, toka kwao viongozi,
Viwanda na ustawi, kila mtu apate kazi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Penye mbao natanabahi, kweli hakuna wajenzi,
Niitoe ipi rai, pawe na watangulizi,
Na tanzu za baibui, machoni zimeshajizi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Kasi isiwe ya chui, bali ya duma mkwezi,
Watu wanayo madai, kuyajibu tumaizi,
Ahadi hazitufai, tukishaenda kwa Mwenyezi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Tufaidi leo hii, kama hao viongozi,
La sivyo tunawarai, vipi hamuipunguzi,
Mishahara asubuhi, kwani kazi hamuwezi?
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Kila kitu ni nishai, sasa twazua majizi,
Vijana wa nchi hii, ajira kwao ni kazi,
Mikakati hatujui, kuondoa jinamizi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Wallahi hatujitambui, kama vile mabazazi,
Urithi wa nchi hii, unatosha kwa majenzi,
Ila tunayo nakisi, hawatimu viongozi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Vinara hawatufai, umaskini waenzi,
Ukwasi wakiuwahi, kutukumbuka ajizi,
Wabunge ni wasanii, majimbo yao hawaenzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Mikoani twastahi, wakupewa viongozi,
Mimi natoa rai, kuchagua sio kazi,
Tuwe na vinara hai, mkoani kwa mageuzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Mikoa uchumi hai, madaraka tuienzi,
Tusiifanye makarai, maji machafu kuhodhi,
Nchi ipate stawi, wawe huru viongozi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Nchi haiwezi stawi, mikoa tusipoenzi,
Ushindani kuudai, ni kitu chenye majazi,
Kubwa sana nchi hii, hatuhitaji wapagazi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Kama kasi ndio hii, mikoa hatutangulizi,
Nchi huja kuzirai, miundo ipate ganzi,
Viungo kama havifai, mwili hautavienzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Ukiritimba haufai, yatakwama mageuzi,
Hii ni kubwa jinai, umma katu hauenzi,
Na vingi vya nchi hii, hiki kikubw kitanzi,
Mo Ibrahim kazi, kama kasi ndio hii.

Chama au nchi

Chama kikundi cha watu, maslahi watafuta,
Kula yao sio yetu, kukosa kwao kupata,
Na kwao ujinga wetu, manufaa wanaita,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.


Angalia hali yetu, hakika ni ya ukata,
Wanavyopewa wenzetu, sisi twabaki twaota,
Twakimbilia upatu, matatani twajikuta,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Kama ni mtoto wetu, cheo hawezi kupata,
Wakwao akiwa butu, ni lazima atapeta,
Tumetupwa kwenye msitu, wa sahau na utata,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Hujiita ni wenzetu, sio katika kupata,
Cha kwao si cha kwetu, chao hatuwezi chota,
Ila wasomba cha kwetu,kwa mikwara na matuta,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Viongozi watukutu, chama wakishakipata,
Hujiaa kama kifutu, na kutisha kuwang'ata,
Serikali huwa butu, wachache watakaopata,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Mizania iwe yetu, viwili kujavipata,
Faida kwa nchi yetu, iwe sote tunapata,
Kisha viongozi wetu, pande zote kutafuta,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Na siasa kama kifutu, ukishika utajuta,
Hasa kama una kutu, huku bado unanata,
Kuna papa nao chatu, chakula wakikukuta,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Nimekwama kwenye gutu, msaada ninatafuta,
Na wa mbili si wa tatu, kutembea si kunyata,
Na wenye akili katu, uchama kwao husita,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Namsihi Muqsitu, nisije nami kudata,
Nivae vyake viatu, yenye kheri kuyapata,
Akinilinda na watu, shetani hatonipata,
Kuimarika kwa chama, si kuimarika nchi.

Uongozi si mgumu

Uongozi sio kazi, kama watu wasikia,
Na si mkubwa ujuzi, kama watu wafwatia,
Hii tarafu azizi, na watu huwasaidia,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Binadamu sio mbuzi, ila wakitaka huwa,
Ikawa kwako ni kazi, walipo kuwanyanyua,
Wakakuachia mashuzi, na uchafu uliojaa,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Ardhi pia makazi, wala hazina ghasia,
Mashine kwa mautmizi, kila kitu huridhia,
Fedha haina maudhi, kwa vyovyote huitumia,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Pale palipo na kazi, ni binadamu kumvaa,
Hata awe na ujuzi, bado hukuharibia,
Ajira huwa ajizi, wakazua na balaa,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Fadhila mwoneshe mbuzi, waswahili wakwambia,
Binadamu ni maudhi, hili kweli zingatia,
Bora kapu la viazi, haliwezi kusumbua,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Uongozi si matanuzi, watu watakuchukia,
Jamali za majahazi, shehena kuzichukua,
Kutumika faradhi, na suna ni kutumia,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Uongozi ni uzazi, kuzaa yaliyo mapya,
Wataka mengi uzuzi, watu wakafuatilia,
Maisha ni uvumbuzi, si ofisini kukaa,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Uongozi ni malezi, wa chini ukawalea,
Wapande za juu ngazi, na urithi kuchukua,
Mzee asiyemaizi, hili atalizuia,
Uongozi si mgumu, watu hawaongozeki!

Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

AUZAYE kura yake, wapaswa umdharau,
Anajali tumbo lake, maisha anadharau,
Muache abaki pweke, huyo mtu wa kusahau,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

Udugu usimshike, huyo sawa na mafuu,
Ili usalimike, umwepuke ni bahau,
Ni muhali mambo yake, kufanikiwa falau,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

Daima pembeni mweke, hana kichwani juzuu,
Vigumu aneemeke,utumwa wake tambuu,
Acha jiwe aeleke, huyu ana makuruhu,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

Demokrasi makeke, na miguu huwa juu,
Kichwa chini kizamike, na kipya huwa kikuu,
Zawadu yake mateke, mchuuzi kura yake,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.


Uweledi tuutake, kwa misemo na nahau,
Avujaye tumwezeke, sio mtu wa kunukuu,
Kisimamacho kianguke,kilo chini kije juu,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

Historia ina upweke, maana ni kuukuu,
Uzee kama mvuke,si wa chini waenda juu,
Sio yote tuwacheke, mengine dawa nafuu,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

Tuendako kuendeke, nguvu tutazisahau,
Tujengacho kijengeke, teknolojia tukubuhu,
Ili nasi tutajirike,tusijiuze bei nafuu,
Wapaswa kumdharau, auzaye kura yake.

Wednesday, October 12, 2011

Nyerere twakukumbuka

MBEGU iliyopandika, yenye za pekee sifa,
Tutakayoikumbuka, katika refu masafa,
Pasiwepo Tanganyika, kupata huu wadhifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Kimwili umeondoka, ila kiroho hujafa,
Mengi uliyotamka, ni kubwa kwetu sahifa,
Na kila tukizinduka, twaitafuta sharifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Ulihofia hakika, kujitokeza kwa nyufa,
Haya yamedhihirika, kabla kupiga chafya,
Na nchi wameishika, watu wasio na sifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Fisadi wamejazuka, na tena wana wadhifa,
Imekuwa patashika, wazidiana maarifa,
Richmond aliposhuka, halikuhitaji khalifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Kagoda wakamulika, faili lake kifafa,
Wengine wanaondoka, twakumbuka alfafa,
Dowans kuja kuzuka, haikuwa ni kashfa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Kulimbikiza wataka, hata walo na wadhifa,
Hisa kwenye mashirika, hivi leo si kashfa,
Lukuki wanalundika, mkoa hadi tarafa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Wanao hukuwaweka, kwenye yoyote nyadhifa,
Nyuma tunaweweseka, urithi sasa ni sifa,
Na wakubwa kupambika, kama mamisi hanifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Bongo zinatatizika, hakuna mweye falsafa,
Insha wanaoandika, huzikwiba maarifa,
Kisha wakayapachika, ili wapate wao sifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Nchi inatawanyika, imekosa makhalifa,
Dini zimeharibika, wamo wasio na sifa,
Wanasiasa wamechoka, na siasa zinakufa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Yashangaa Afrika, kurudi nyuma taifa,
Nchi ulipoishika, yalijaa maarifa,
Hivi leo twatishika, hakuna mwenye wasifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Mwalimu umeondoka, ujamaa umekufa,
Ubepari wajengeka, usio na maarifa,
Wazawa tunateseka, na wengine hata kufa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Chama kimebadilika, usanii ni wadhifa,
Gamba gumu kujavuka, kofia zawachachafya,
Imani imetutoka, tunachongoja ni kufa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Badiliyo hatafika, karne hii ya mofa,
Heshima imeondoka, zasema taarifa,
Hata wetu washirika, wahoji kimataifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Kalamu chini naweka, nikimwomba Raufa,
Busara kutoondoka, katika zote nyadhifa,
Na hekima kutukuka, katika hili taifa,
Nyerere twakukumbuka, baba yetu wa taifa.

Tuesday, October 11, 2011

Wapenda watu wachache

Wachache watu wapenda, watu ukubwa wataka,
Kila mtaka kupanda, si bure hushughulika,
Kuna linalomdunda, anataka kulishika,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Ya kwake yanamshinda, ya wengine atawika?
Na jamii ya kuvunda, harufu haitotoweka,
Ndio kote walotanda, kipya hakitashuka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Wateremka udenda, kwa ukata kufutika,
Au kujenga kiwanda, kwa fedha ya washirika,
Au shirika kuunda, kufilisi walochoka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Wengine wamevurunda, hakuna lililoitika,
Wataka chuma matunda, kwa wizi wa kuaminika,
Katika hilo huwatenda, hakuna mbwa kubweka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Viongozi kama nunda, mali hulimbikizika,
Ni Jetta wanajipenda, na hawana mshirika,
Na kwao kama kdonda, ni ndugu hadi kuzika,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Akili zao huganda, kwa ukubwa kuutaka,
Sifa wanavyozipenda, ndarahima hutumika,
Huwa radhi kula ganda, ilimradi kukubalika,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Wanapokosa hukonda, nyumbani hakutokalika,
Na akiwa mziwanda,kitindamimba hutaka,
Maajabu mwenye kenda,moja kwa nguvu kutaka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Hawa watu wamepinda, vigumu kueleweka,
Hutaka kunywa mafunda,ilhali wanabweka,
Mbwa hawezi kutenda,yale wanayoyataka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Waliliazo ni honda, za mchina nani ataka?
Hudai punda kupanda, sisi miguu imekatika,
Mahekalu huyaunda, sisi twashindwa ezeka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Ghorofa wanazipanda, sisi ngazi tunashuka,
Hata kama twawapenda, vipi mkono kuwashika?
Na katika yao ajenda,hili halijasomeka,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Wasanii wa kuwanda, mitaani wakifika,
Huku na huku huranda, na mikono kuwashika,
Vitoto vilivyobwanda, mikononi kuvishika,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Nyoyo zinavyowadunda, si dhiki kueleweka,
Kubwa wataka mkanda, televisheni kuweka,
Waonwe wanawapenda, wasiowapenda hakika,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Najenga changu kibanda, mchanga ninautaka,
Na mbele siwezi kwenda, bado daraja kuvuka,
Miguu imeniganda, naenda kupumzika,
Wapenda watu wachache, wapenda ukubwa wengi!

Ghorofa kwenye kinyesi

Nchi hii nchi gani, ulaji na makamasi,
Maudhi hatuyaoni, na hatuna wasiwasi,
Twakaribisha wageni, mitaa ina kinyesi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Ni ustaarabu gani, nauliza kadamnasi,
Kinyaa hatukioni, utadhani ibilisi,
Twamuaibisha nani, kama si sisi watesi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Mvua tukibaini, twafungulia vinyesi,
Mitaa na uchochoroni, zinafurika nuksi,
Wengine ni muumini, hawawezi hii kasi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Zinavyoota mjini, kama uyoga fususi,
Ila mazingira duni, na hewa yake nyeusi,
Maofisa hawabuni, lolote la kuasisi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Dar es salaam jijini, utadhania chunusi,
Ni mengi utafichua, ukifanya udamisi,
Na kisha kuyagungua, ya uchache ufanisi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Ninakuwa mashakani, eti tuna jiniasi,
Ni goli li kimiani, au tonge la msosi,
Halitoingia ndani, koromeo litaasi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Naona uhayawani, tena mkubwa utusi,
Mbona hatuamshani, tukakijua kiasi,
Kamwe hatutoki ndani, bila kuvaa libasi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?


Chai ikiwa tumboni, nje waweza ifosi,
Unapokuja mtaani, zikakufuma risasi,
Hali huwa abautani, motoni na firdausi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?


Wakubwa tuwaombeeni, walione na wahisi,
Na maneno wasemeni, wajione na nuksi,
Wasijifiche mwao ndani, hali nje kiharusi,
Ustaarabu gani wa ghorofa kwenye kinyesi?

Monday, October 10, 2011

Yuko wapi shujaa wa Afrika?

Twamsaka Afrika, yuwapi wetu shujaa,
Awezaye kuzizika, kasumba za kutawaliwa,
Na asiyeterereka, na njia anayejua,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Nchi zatia wahaka, kulogwa tunadhaniwa,
Na viongozi mizuka, ndio wanatuzingua,
Wakipangwa na mahoka, hawaoni hata njia,

Cheoni wababaika, wanashindwa kuamua,
Msukule watukuka, nao ukiwalingania,
Ulaya na Amerika, ndiko unga wanapewa,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Nafasi wamezishika, na vyote wang'ang'ania,
Hata vyoo wanashika,vigumu kuviachia,
Wengine wanatucheka,limbukeni tulivyokua,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Kila jamba tunataka, peke yetu kuamua,
Mabingwa walalamika, wanasesere wamekua.,
Na uzee ukifika, hatutaki kuyatua,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Vijana wa Afrika, sasa wanatuzomea,
NI mbali tulikotoka, na hatujapiga hatua,
Wana makubwa mashaka, kama tutawakomboa,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Vinginevyo wanataka, taifa kulichukua,
Ili tuweze kuvuka,tulikoishaazimia,
Na kulipia sadaka, tuloacha kutoa,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Tubadilike haraka, si magamba kujivua,
Watu wapya tunataka, na nchi mpya kuvumbua,
Hili halina wahaka, mwapaswa kulisikia,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Vinginevyo ni gharika, mkae mwategemea,
Hairudi Afrika, nyuma ilikotokea,
Mbele budi kuendeka, ima-fa-ima pigaua,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Kilichobaki hakika, kujitokeza shujaa,
Mjini anakotoka, kijijini kuingia,
Ikaanza kupangika, ufukara kukataa,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Kwanza hatotajirika, ila wa kwake raia,
Nao wakishajengeka, naye atajiinua,
Hapo ndipo Afrika, kumekucha itakua,
Yuwapi wetu shujaa, tumfate Afrika!

Sunday, October 9, 2011

Rais au raia?

Hivi mwenye nchi nani, rais au raia,
Hili sio yumkini, wananchi twapinduliwa,
Tunaoweka kazini, ubwana wanachukua,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Kati yao bosi nani, rais au rais,
Afrika mashakani, wote hili tunajua,
Mtu ukishamthamini, dharau anaingia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Tumegeuzwa manyani, nje wanatushangaa,
Uoga wetu wa nini, nafasi kuichukua,
Iweje mtu ofisini, mwenye mali kujitia?
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Hazina huwa shakani, fisadi wakiingia,
Mbawa noti hubaini, kwa watu zikaishia,
Na raia masikini, maneno waambulia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Ubinafsishaji baini, kitanzi wametutia,
Mashirika hatuoni, na fedha zimepotea,
Hakika hawa wahuni, siogopi kuwaambia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Uchangiaji nchini, jahazi lazidi waa,
Hatuoni kwa yakini, kitu tulichofanyiwa,
IMF wadaini, mtegoni kututia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Viongozi mikoani, sio wa kuwachagua,
Tunafanya ya utani, rais kuwateua,
Tutapata watu gani, mikoa kuendelea?
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Nchi yataka anwani, visheni au ruia,
Hivi leo twazaini, kwa mbwembwe na sanaa,
Hii jama nchi gani, iendako isojua?
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Ni watu wa mjini, umeme wanaolilia,
Huko kwetu vijijini, giza tumeshalizoea,
Na miaka hamsini, kwetu ni kama milenia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Hivi twajivuna nini, watu wetu kuwafanzia,
Mimi naona utani, tena mkubwa mzaha,
Akili ninaamini, sasa tungelitubia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Tumekwaza vijijini, na malengo kupotea,
Ni heri ya mkoloni, kwa hulka na tabia,
Ni bure tunajithamini, bila watu kuangalia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Nistahi ya Manani, kwa ulimi na nasaha,
Nimeshakiri moyoni, uongo nitakimbia,
Marufuku uzaini, kwangu kuukurubia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Najenga yangu medani, sifuati ya dunia,
Ila naomba yamini, kwa shahada na dua,
Wabaya ukibaini, wewe utamalizia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Watu wangu wathamini, na juu kuwanyanyua,
Ittunze yao amani, na umoja kuringia,
Ila watie shakani, wote wanaowahadaam
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Na leo hapa nchini, katiba twazungumzia,
Anastahili nani, mchakato kuamua?
Raia ninaamini, haki zote wanazoa,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Jishusheni chini jamani, kazi kutuachia,
Msiogope uhuni, wallahi hatutawafanzia,
Kuchinja kwetu amini, kunyonga hatukuzoea,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Tuepuke na udini, waumini kuhadaa,
Mtatutia usononi, nchi ikaja pagawa,
Oneni haya jamani, uozo kutuachia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Wito huu sikieni, na nyie wanasheria,
Juzuu mzibaini, ukweli kuwaambia,
Msikae utumwani, shari haitachagua,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Malenga nawaombeni, kizazi kuangalia,
Njia yao iwe laini, kesho watakakopitia,
Nafsi zenu dhibitini, urithi kujawaachia,
Rais au raia, kati yao nani bosi?

Monday, October 3, 2011

Mbunge mtetea chama

Mbunge mtetea chama, si mbunge wa raia,
Mdomo akiachama, aweza kuwashindilia,
Tumbo lake likisoma, hatajua yako njaa,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Toka mwanzo utamsoma, vifurushi akigawa,
Krediti huazima, kulipwa akitarajia,
Hukufanya muadhama, kura yako akingojea,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Unaweza kumpima, huko alikotokea,
Meli nyingi zilizama, nahodha alipokuwa,
Leo eti chake chama, vinginevyo chatwambia,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Hawa ni watu wa kalima, ya umimi wa kupaa,
Ni sume yenye heshima, maendeleo huua,
Zichunguzeni tuhuma, ukweli mtaujua,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Maisha yao kiama, tayari kishaingia,
Na kaumu hujakwama, nyuma wakijamfuatia,
Vipi ovu kuwa jema, hata upya likizaliwa?
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Macho nani kufungua, akawa kwa hili mjuzi,
Watu kujaendelea, tunataka viongozi,
Tafiri na kuchambua,yenye hadhi maamuzi,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Wananchi na wanachama, njaa kwetu ni kitanzi,
Wachache wanaojua, mumiani twawaenzi,
Wakijakufichuliwa, mmekwisha ni wa juzi,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Kifo tunakikumbatia, Nungwi hadi Mlandizi,
Makaburi twachimbia, hali wa hai wakazi,
Msiba twashangilia, sherehe kwetu majonzi,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Nguvu zimeniishia, niseme nini mzazi,
Nimebakia kulia, giza tunavyolienzi,
Laiti ningelijua, yaja kuwa ni majonzi,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Serikali yatakiwa, kufanya ya kwake kazi,
Na wabunge nao pia, wana ya kwao faradhi,
Vipi moja kuja kuwa, bila kuzusha majonzi?
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Jalali nakwangukia, mfalme mwenye enzi,
Nchi yetu kujalia, waje wema viongozi,
Na salama kuja kuwa, kijacho hicho kizazi,
Mbunge mtetea chama, si mbunge wa wananchi!

Ameshajilimbikizia

Ameshajilimbikizia, fisadi kushindwa kazi,
Nchi keshawauzia, wa jana pia wa juzi,
Raia hawathamini, nchi keshafanya uchuzi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Ndio wanaotufua, kwa maganda ya viazi,
Wanaotumiminia mafuta ya maandazi,
Mgongo kuutumia, wa chupa mafuta nazi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Pasi weshajipigia, suruali kama ngozi,
Njiani wakitembea, nawakumbuka manazi,
Nchi inakoelekea,imeanza panda ngazi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Ukuu huukimbilia, japo hawawezi kazi,
Mamlaka wakichukua, nchi hushikwa maradhi,
Na daima huugua, dawa hazifanyi kazi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Ni chama huwachagua, kinachotuchuna ngozi,
Wachache wanaosaidiwa,wengine twafanywa nzi,
Twazaliwa na kukua,pasi malezi na mapenzi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Ni wao na familia zao wanazozienzi,
Ni kisiwa wamekua, wengine kwa ushuzi,
Wanataka kujilia,bila yoyote maudhi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Haki hujakupotea, dhuluma kuwa azizi,
Mali watajajimegea, makwao washehenezi,
Wengi wakawa wakiwa, watu wasio na radhi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Tamaa hujapotea, kwa baadhi na baadhi,
Kura wakaikataa, na kuiona upuuzi,
Kujiandikisha pia, wasuse chao kizazi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Uchu ukishavamia, siasa huwa na ganzi,
Watu huona udhia, kura kujawapa wezi,
Mwishowe hujaamua, kuyafanya mapinduzi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Kinachofuatia, redio wani huwa wazi,
Na kitakachoendelea, hakitakuwa kwetu wazi,
Kusaga meno na kulia, yatakuwa maamkuzi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Dawa acha kutumiwa, acha riziki za wizi,
Wacha mungu kuchagua, haki yawe maamuzi,
Na nchi kuendelea, wapeni wachapa kazi,
Ameshajilimbikizia, fisadi hawezi shindwa.

Sunday, October 2, 2011

Nchi hii yetu sote

Yetu sote nchii hii, sio ya mtu mmoja,
Mchana na asubuhi, jumla si rejareja,
Tena tunawakinai, wanaojifanya waja,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Hisa zetu tanbihi, kila mtu kura moja,
Hao wanaojidai, eti sisi ni wakuja,
Twawaambia wazirai, kiama chao kinakuja,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Hamsini inadai, miaka waliofuja,
Watatupa ipi rai, kama wao si mateja,
Hata wasiotanabahi, hawaioni faraja,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Ukiritimba nishai, watu kazi kubwabwaja,
Misingi hawaijui, kanuni zao za kuja,
Na filimbi na nai, wadhani nazo zina hoja,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Wapemba na Waunguja, Waha na Wamasai,
Wamakonde na Wangazija, na wote tuliowahi,
Hakuna mtu wa kuja,sote ni raia hai,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Hakika kila mmoja, awezalo tumstahi,
Isiwe twaua umoja,kwa kudai hawafai,
Vikome navyo vioja,watoto kuwa warithi,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Tujengeni madaraja, ili sote tufurahi,
Budi kuwa na umoja, wakweli si wa maslahi,
Tuukimbie useja, na tando za baibui,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Hatuna muda wa kungoja, tuogope makarai,
Nchi kupanda daraja, mapinduzi inadai,
Wachapa kazi kutaja,na si wangoja chai,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Tutajengaje umoja, na wakubwa hawafai?
Tutapandaje daraja, watu kazi hawajui?
Udugu sumu ya umoja, makapi huwa adui,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Uswahiba wa lahaja, hakika huu jinai,
Jamaizesheni mrija,ukiyabeba makarai,
Inachosha ngojangoja,hasadikiki ndugu mui,
Nchi hii yetu sote,sio ya chama kimoja!

Saturday, October 1, 2011

Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Mjinga hutajirika, na mali kwake ikaja,
Hujenga kikajengeka, kishakikaja kuvuja,
Huzikwa pia mzika, sikuye naye ikija,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Maisha ya watajika, hayaji kwa rejareja,
Yataka watu kusuka, kwa ibada nazo hija,
Na kutovuka mipaka, ya Mola alo mmoja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Matajiri huzuzuka, neema inapokuja,
Wakajiita Rabuka, ma wala si tena waja,
Huamini wakitaka, lolole lile kwao huja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Uzima sio shirika, haiji na haijaja,
Muumba hana shirika, sirize ngumu kuvuja,
Vigumu kueleweka, kumpa asiyemtaja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Dunia hii hakika, inatawala mirija,
Hujiona wastahika, kula mia sio moja,
Kulimbikiza hutaka, na sio kufunga mkaja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Watu hawa huibuka, kila awamu zikija,
Na kile wanachoweka, ni mtaji unaovuja,
Utawala kuupaka, kwa mafuta ya Unguja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Waaminiwao wahaka, wavaa la dhambi koja,
Na kila wanachokishika, Midasi ana faraja,
Na jipu likitumbuka,usaa hauachi kuvuja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Utajiri bila shaka, hakika sio kioja,
Yetu makubwa mashaka, ni kidari na mapaja,
Huo wao ushirika, nchi unaoifuja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!

Inatutia mashaka, zuzu naye kuwa na hoja,
Na weledi wakashika, toka kwake lau moja,
Na nchi ikafunguka, ukajaisha uteja,
Utajiri si hoja, hata zuzu hutajirika!